Sunday, October 13, 2019

MWENGE WA UHURU WAMALIZA MBIO ZAKE KILWA NA KUINGIA HALMASHAURI YA MANISPAA YA LINDI.

Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa 2019 mzee Mkongea Ally akiwasalimia wananchi wa mtaa wa mto mkavu kata ya Mbanja wakatai makabidhiano ya Mwenge huo kati ya Halmashauri ya wilaya ya Kilwa na Halmashauri ya manispaa ya Lindi Mkoani humo.
 ..............................................


 NA HDIJA HASSAN, LINDI.


Mwenge wa Uhuru uliokuwa unakimbizwa wilayani Kilwa Mkoni Lindi umemaliza mbio zake na kukabidhiwa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mkoani humo.


Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Mzee Mkongea Ally amesema miradi mitano ya maendeleo iliyopangwa kuzinduliwa wilayani humo, imeridhiwa na wataalamu wake.


Akizungumza na wananchi waliojitokeza kupokea mwenge huo leo asubuhi (jumapili, Oktoba 13, 2019) kwenye mtaa wa mto Mkavu kata ya Mbanja halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Mkongea aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kwa kuwa na miradi mizuri sambamba na kuwataka viongozi wa Manispaa ya Lindi kuhakikisha wanakuwa na Taarifa zote muhimu kwenye kila mradi utakaopitiwa na mwenge huo wa Uhuru sambamba na kuwataka wataalamu kuwa katika maeneo yao ya Miradi.


Mkongea pia aliwataka Viongozi kusimamia maadili pamoja na itifaki za mbio za mwenge wa Uhuru zinazotolewa na wakufunzi husika kwani Mwenge huo wa Uhuru sio wa mkimbiza Mwenge bali ni uwakulishi wa Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na tunu ya muasisi wa Taifa Mwalimu Julias kambalage Nyerere hivyo ni wajibu wa kila mtu kukiheshimu chombo hicho muhimu.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya kilwa Christopha Ngubiagai aliitaja miradi iliyopitiwa na Mwenge huo wa Uhuru ni pamoja na kutembelea na Kukabidhi mikopo kwa vikundi vya wajasiriamali katika kijiji cha Njinjo, kuweka jiwe la msingi Duka la Dawa na Chumba cha kuhifadhia maiti, kuzindua Mradi wa maji katika kijiji cha Mpara, kutembelea Mradi wa Barabara Masoko pamoja na kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa ukarabati na ujenzi wa Madarasa na Bwalo la chakula katika Chuo cha wananchi Kilwa Masoko ambayo inathamani ya shilingi bilioni 1 na milioni 900.


Mapema akipokea Mwenge huo wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shihibu Ndemanga alisema kuwa Mwenge huo wa Uhuru katika Manispaa ya Lindi utakimbizwa kwa urefu wa km 200 na utakagua miradi 6 yenye thamani ya shilingi bilioni 5.23.


Kesho (jumatatu, Oktoba 14) mbio hizo za mwenge wa uhuru zinatarajiwa kufikia tamati kwa kuzimwa ambapo katika sherehe hizo za kuitimisha zitafanyika katika viwanja vya Ilulu Manispaa ya Lindi Mkoani humo ambayo itaenda sambamba na kumbukizi ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambalage Nyerere.

No comments:

Post a Comment