Tuesday, April 30, 2019

RIDHIWANI APONGEZWA CHALINZE KWA KUTEKELEZA AHADI.


Na Shushu Joel, Chalice.

MBUNGE wa jimbo la chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete amekuwa gumzo jimboni humo mara baada ya kutimiza moja ya ndoto zake alizokuwa akizifikilia kuwatimizia wananchi wake.


Ujasili wake na uthubutu wake katika kuhakikisha wananchi wake wa chalinze wanakuwa na neema ndio umepelekea kuwa Gumzo kila kona ya jimbo la chalinze.


Akizungumza na wananchi wa kata ya Miono Mbunge wa jimbo hilo aliwahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa hakuna kijiji kitakachorukwa na mradi wa Usambazaji umeme vijijini (Rea).


Alisema kuwa wakati anaanza ubunge alikuwa akijiuliza ni lini changamoto ya upatikanaji wa nishati ya umeme itamalizika ingawa nilijua kuna siku wananchi wangu wote kuna siku watakuwa nuruni. 


"Umeme ni ajira hivyo ukitumika ipasavyo utapunguza tatizo la ajira kwa vijana na hata kuchangia kwa ongezeko la pato katika Halmashaur yetu kupitia kuanzishwa kwa fursa mbalimbali kwa kupitia upatikanaji wa umeme chalinze.


Alisema kuwa nchi hii kuna wabunge wengi hivyo mwenye kuishawishi serikali anafanikiwa mapema na kufanikisha maendeleo katika eneo lake,lingine ni ukaribu na wadau mbalimbali wenye dhamira chanya ili kufanikisha miradi Aidha alisema kuwa jimbo la chalinze lina jumla ya vijiji 74 na vyenye umeme ni vijiji 34 na vijiji 40 vitakamilika muda si mrefu kwa agizo la serikali ya awamu ya tano.


Mbali na hayo Kikwete amempongeza Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa juhudi zake anazozifanya katika jimbo hilo kwa kuhakikisha wananchalinze wananufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo.


"Nakumbuka siku unakuja kuomba kura kwa wananchi na kuwaambia utawaletea maendeleo na watashangaa pia uliwataka wananchi kumwagalia Mbunge wa jimbo Lao Ridhiwani Kikwete kwani ni Jembe linalolima usiku na mchana pasipo kusubili mvua"Alisema Ridhiwani .


Kwa upande wake waziri wa nishati Dk Medad Kalemani amempongeza Mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete kwa utendaji wake wa kazi katika jimbo la chalinze ambalo ni kubwa lakini ni jimbo lenye maendeleo mbalimbali.


Alisema kuwa kutokana na jinsi gani Mbunge huyo anavyomsumbua juu ya suala la umeme ameagiza kuwekwa kwa umeme katika vijiji vyote vya kata ya Miono bila kurukwa kwa nyumba ya aina yeyote ile.


 Aidha waziri huyo amemhakikishia Mbunge huyo kuwa serikali kupitia wizara yake imekubaliana kupeleka umeme katika vijiji vyote vilivyobaki katika jimbo hilo na jambo hilo lianze mara moja. "Serikali ya awamu ya tano iko makini kuhakikisha wananchi wake wanapatiwa huduma zote pasipo kuangalia itikadi ya kisiasa" 


Aidha Dk Kalemani amewataka wakandarasi kote nchi ni kuhakikisha wanawapatia ajira vijana wanaozunguka miradi ili kurahisisha utendaji wa kazi pia kuwapatia fursa vijana wa maeneo husika ambako miradi inapita.


Aliongeza kuwa anatoa onyo kwa wakandarasi wanaochelewesha kuwaunganishia wananchi umeme huku wakiwa wamesha maliza kulipia fedha zao za kuunganishiwa umeme ambazo ni shilingi elfu 27 iwe Rea au Tanesco.

WEKA HATA MTI UWEKEWE UMEME- DKT. KALEMANI

Na Omary Mngindo, Miono

WAZIRI wa Nishati DKT. Medard Kalemani amewataka wakazi katika vijiji vilivyopo Kata ya Miono Jimbo la Chalinze Mkoa wa Pwani, ambao havijapatiwa huduma huku wakiwa na maeneo ambayo hawajajenga, kuweke hata mti, ili washushiwe huduma hiyo.

Waziri Dkt. Kalemani ametoa kauli hiyo juzi alipofanya ziara ya siku moja ya kuwasha umeme katika nyumba mbili za wakazi katika Kijiji cha Makao Makuu katani humo, akiambatana na mwenyeji wake Ridhiwani Kikwete mbunge wa jimbo la Chalinze mkoani hapa.

Aidha Waziri huyo ametoa mwezi mmoja kwa Meneja wa shirikanla umeme nchini Tanesco (tawi la Chalinze) na Mkandarasi kuhakikisha wanamalizia kusambaza huduma hiyo katika vijiji vyote vilivyosalia, huku akiahidi kurejea hapo mwezi ujao kufuatilia agizo lake.

"Sijaridhishwa na kazi inayofanywa ndani ya Kata hii ya Miono, haiwezekani mradi huu ndani ya miezi 11viunganishwe vijiji viwili tu, serikali imewekeza kiasi cha shilingi bilioni 29, kazi yenyewe haieleweki, kuanzia kesho wekeni kambi hapa Miono, kazi ifanywe na vijana wa hapa," alisema Waziri huyo.

Pia Waziri Kalemani amewaambia wananchi hao kuwa, kuanzia sasa uunganishwaji wa umeme ni sh. 27,000 tu, uwe wa Tanesco au Rea huku akiahidi kupiga mnada wa kuku wa mkazi ambaye atashindwa kulipia kiasi hicho kwa ajili ya kuunganishiwa huduma hiyo.

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani hakusita kumpongeza Waziri kwa namna wanavyosambaza huduma hiyo, huku akisema kuwa anaridhishwa na juhudi hizo na kuongeza kuwa kwenye maeneo kadhaa jimboni humo bado kuna uhitaji mkubwa wa upatikanaji wa umeme.

"Hapa kuna baadhi ya maeneo bado hayajafikiwa na huduma hii, leo asubuhi nimezungumza na wasaidizi wako wamenieleza kwamba kuna mradi wa ujazilizi, imani yangu ni kwamba mpango huo utayapitia maeneo hayo, pia kuna vijiji vingi ndani ya jimbo zima la Chalinze," alisema Ridhiwani.

Diwani wa Kata hiyo Juma Mpwimbwi amemuomba Waziri Kalemani kuwaongezwa nguzo japo 40 zitazopelekwa katika vitongoji vya Mwanakibungo na mifugoni ambavyo havijapitiwa kabisa na huduma hiyo.

Mmoja wa wakazi kijijini hapo Salumu Helman akizungumza baada ya mkutano huo alielezea furaha yake ya kupunguzwa kwa gharama ya uunganishwaji wa huduma hiyo pasipokujali unatokea Rea au Tanesco.
 Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwaniakizungumza mbele ya waziri wa Nishati kata ya Miono.

MBUNGE VITI MAALUM LINDI AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA MKUU WA MKOA WA LINDI.

 BUNGE Viti maalum Mkoani Lindi {CCM} Hamida Abdallah Mohamedi, (kushoto) amkimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi, Jezi pamoja na mpira kwaajili ya timu ya Namungo FC ya wilaya ya Rungwa Mkonai Lindi.
 
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi, Katibu wa Namungo FC, Johanes Bukine {Mustachi} Jezi pamoja na mpira
............................. 

Na Hadija Hassan, Lindi.

BUNGE Viti maalum Mkoani Lindi {CCM} Hamida Abdallah Mohamedi, ameipatia Klabu ya Namungo FC ya Ruangwa, Msaada wa Vifaa vya Michezo vitakavyowawezesha kufanyia Mazoezi.

Vifaa walivyoyopatiwa ni Jezi Jozi mbili na Mpira mmoja, vyenye thamani ya Tsh, 350,000/-vimekabidhiwa kwa uongozi wa Mkoa na baadae kwa viongozi wa timu husika.

Mbunge Hamida akizungumza katika Mapokezi na kukabidhi kwa Vifaa hivyo, kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo, alisema kupanda kwa Namungo FC, kumerejesha furaha ya wananchi wa Lindi katika Medani ya Michezo, kwani kutawafanya  kuziona timu mbalimbali zikiwemo Yanga, Simba, Azam, Mtibwa na nyinginezo.

“Kwa kuliona hili, mimi binafsi nimeguswa na ninaiunga mkono kwa kuipatia  timu yetu Jezi na Mpira, ambazo zitawasaidia kufanyia mazoezi” Alisema Hamida.

Pia, alisema ushindi walioupata timu ya Namungo FC ni wa wana-Lindi wote, baada ya kupotea furaha hiyo, waliyokuwa wakiipata kutoka kwa timu ya Kariakoo FC, kupotea katika Medani ya Michezo takribani miaka {15} sasa.

Akipokea msaada huo, Katibu wa Namungo FC, Johanes Bukine {Mustachi} amemshukuru Mbunge Hamida kwa msaada huo wa Vifaa, huku akiwaomba wadau wengine wa Maendeleo kuiga mfano wa kiongozi huyo kwa manufaa ya timu yao.

Bukine alisema Namungo FC ni timu ya wananchi wote wa Mkoa wa Lindi, hivyo ni vema wakaiunga mkono kwa kuichangia ili iweze kupiga hatua kwa maendeleo ya Soka.

VULU NA MGALU KUTIMIZA AHADI ZAO MAFIA.


 Pichani Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Zaynab Vulu akizingumza na viongozi wa Umoja wa Wanawake (UWT) wilaya ya Mafia mkoani Pwani alipokuwa kwenye ziara ya siku moja. Meza Kuu wa mwisho kutoka kushoto Arafa Kisela Mjumbe wa Mkoa, Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mafia Mtumwa Geo na Mwenyekiti wa CCM Hassani Pango. 

Picha na Omary Mngindo.

 .................................................

Na Omary Mngindo, Mafia.


WABUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Zaynabu Vulu na Subira Mgalu ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati wanataraji kutimiza ahadi walizozitoa wilayani Mafia.


Hayo yamebainishwa na Vulu alipokuwa kwenye ziara ya siku mbili wilayani hapa, iliyolenga kukutana na wana- Jumuia zinazounda Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo akiwa Mafia amekabidhi kitanda kimoja kwenye Zahanati ya Maalimbani Kata ya Kiegeani jimboni hapa.

Akizungumza na wana-Jumuia ya Wanawake (UWT) wilayani hapa mbele ya Mwenyekiti Mtuma Ahmad, Katibu Khadija Geo, Mwenyekiti wa CCM Hassani Pango, wa Wazazi Mohamed Fakhi na Katibu Mashaka Milimila, VULU alisema kuwa wakiwa katika ziara wilayani humo kuna ahadi ambazo wameziahidi.

"Wana-Jumuia wenzangu wakati tukiwa kwenye ziara wilayani hapa nikiwa na mbunge mwenzangu Subira Mgalu kuna mazungumzo mengi ambayo yumezungumza ikiwa ahadi ambazo tumezitoa ikiwemo viti 100, tunajipanga wakati wowote tutatimiza ahadi hizo," alisema Vulu.

Aidha mbunge huyo alipokea taarifa za utekelezaji wa ilani ya chama hicho ikiwemo wa ugawaji wa taa za sola kwenye zahanati mbalimbali zinazotolewa na Naibu Waziri Mgalu zinazolenga kuwaboreshea huduma hiyo maeneo hayo.

"Nimepokea shukrani za mbunge mwenzangu Subira Mgalu anbaye ni Naibu Waziri wa Nishati, mmesema amekabidhi taa za sola katika zahanati mbalimbali, nitazifikisha kwake, nasi tupo pamoja katika kuhakikisha tunaisaidia serikali kwenye sekta mbalimbali," alisema Vulu.

Katika ziara hiyo Vulu amekabidhi kitanda kimoja, shuka pamoja na vifaa Tiba katika zahanati ya Malimbani iliyopo Kata ya Kiegeani, huku akiahidi kuchangia pesa taslimu kwenye ujenzi wa jengo la ofisi ya Jumuia hiyo wilayani hapa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT wilayani hapa Mtumwa alisema kuwa Jumuia yao inaendelea na uhamasishaji wa Jumuia pamoja na chama ili kuhakikisha wanaisaidia serikali katika maendeleo ya nyanja zote.

Kwa upande wake Mjumbe wa jumuia hiyo wilayani Mafia Arafa Kisela, amemshukuru Vulu kwa ushirikiano aliowapatia wa gari kwenye uchaguzi wa mwaka 2015, huku akiwataka wana-CCM kuendeleza umoja upendo na mshikamano.