DC. BAGAMOYO AFANYA KIKAO NA KAMATI YA SENSA WILAYA.
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe Zainab Abdallah, akizungumza katika kikao alipokutana na Kamati za Sensa za Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze. ................................. Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe Zainab Abdallah Amefanya Kikao na kamati ya Sensa ya Wilaya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama (KUU) ya Wilaya kufuatia maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika tarehe 23/08/2022. Mkuu huyo wa Wilaya pia ameendelea kuwasisitiza Wananchi wa Bagamoyo, wawe tayari kuhesabiwa Tarehe 23 Mwezi huu itakapofika ili kusaidia serikali iweze kupanga Mipango ya maendeleo kwa Miaka 10 ijayo. Alisema ili serikali iweze kupanga mambo mbalimbali ya maendeleo inahitaji kuwa na idadi ya wananchi wake iliyo sahihi kwaajili ya kufikisha huduma za jamii mahitaji yaliyo sahihi. Kikao cha kamati ya sensa kimefanyika ili kufanya tathmini ya mwenendo mzima wa maandalizi ya zoezi la sensa na hali halisi ya mwenendo wa mafunzo ya wata...