Wednesday, August 10, 2022

DC. BAGAMOYO AFANYA KIKAO NA KAMATI YA SENSA WILAYA.

 May be an image of 2 people, people sitting and indoor

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe Zainab Abdallah, akizungumza katika kikao alipokutana na Kamati za Sensa za Halmashauri za Bagamoyo na Chalinze.

.................................

 

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe Zainab Abdallah Amefanya Kikao na kamati ya Sensa ya Wilaya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama (KUU) ya Wilaya kufuatia maandalizi ya Sensa ya Watu na Makazi inayotarajiwa kufanyika tarehe 23/08/2022.

 

Mkuu huyo wa Wilaya pia ameendelea kuwasisitiza Wananchi wa Bagamoyo, wawe tayari kuhesabiwa Tarehe 23 Mwezi huu itakapofika ili kusaidia serikali iweze kupanga Mipango ya maendeleo kwa Miaka 10 ijayo.

 

Alisema ili serikali iweze kupanga mambo mbalimbali ya maendeleo inahitaji kuwa na idadi ya wananchi wake iliyo sahihi kwaajili ya kufikisha huduma za jamii mahitaji yaliyo sahihi.

 

Kikao cha kamati ya sensa kimefanyika ili kufanya tathmini ya mwenendo mzima wa maandalizi ya zoezi la sensa na hali halisi ya mwenendo wa mafunzo ya wataalam na makarani watakao shiriki zoezi hilo adhimu la serikali siku ya tarehe 23 Agosti mwaka huu.

Wakitoa taarifa ya zoezi hilo waratibu wa sensa ya watu na makazi kwa halmashauri zote mbili ya Chalinze na Bagamoyo, walieleza jumla ya makarani 991 wanaendelea na mafunzo kwa siku 15 katika halmashauri ya Chalinze na makarani 418 wanaendelea na mafunzo kwa hamashauri ya Bagamoyo.

 

Katika kikao hicho wajumbe wamekubaliana kwa pamoja kuhakikisha wananchi wanahamasishwa kushiriki katika zoezi la sensa kupitia michezo mbalimbali pia kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Aidha katika kikao hicho wajumbe walikubaliana kuwa wenyeviti wa vitongoji wahakikishe wanahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika zoezi la sensa na kutoa ushirikiano wa hali ya juu kwa makarani katika kuwaongoza kuwafikia wananchi.

 

Ikumbukwe kuwa Sensa ya Watu na Makazi hufanyika kila baada ya Miaka 10 ambapo Sensa ya Mwaka huu 2022 ni Sensa ya watu na makazi.

May be an image of 3 people and people sitting

 

May be an image of 7 people, people sitting and indoor

 

RC KUNENGE AMEITAKA NDC KUANDAA MCHORO ENEO LA KONGANI YA UWEKEZAJI KIBAHA KWA AJILI YA KUVUTIA WAWEKEZAJI

No description available.

Na Mwamvua Mwinyi, Pwani

 

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge amekutana na uongozi wa Shirika la Maendelo la Taifa – NDC kwa mazungumzo ya kuitangaza Kongani ya Viwanda inayomilikiwa na Shirika hilo, Mjini Kibaha na kuhakikisha inaandaa mchoro wa eneo hilo kwa ajili wawekezaji.

 

Mazungumzo hayo yalifanyika kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa huo ambapo Kunenge amemshauri Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Nicolaus Shombe  kuhakikisha ofisi yake inaandaa mchoro huo ili kuinua uwekezaji.

 

“Ni wajibu wangu kuzisemea taasisi zote zilizopo mkoani kwangu, hivyo mnapaswa kuandaa mchoro wa eneo hilo, mnipatie ili tuweze kulitangaza kwa wawekezaji wanaotafuta maeneo ya uwekezaji,” alisema Kunenge.

 Akifafanua faida za uwekezaji, Kunenge ameeleza kuwa unasaidia katika kufanikisha malengo ya mkakati mkubwa wa mkoa uliolenga kuongeza vyanzo vya mapato, hivyo eneo hilo la NDC ni muhimu na litasaidia kuongeza mapato.

 

Katika Hatua nyingine, amewapongeza watendaji wote wa Sekretarieti ya Mkoa na wa Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kwa utendaji wa kazi na kupelekea mkoa kushika nafasi ya tatu nchini kwa kigezo cha makusanyo yanayotokana na mapato ya ndani.

 

Nae Mkurugenzi Mtendaji Wa shirika la Maendeleo ya Taifa NDC  Dr. Nicolaus Shombe alifafanua kuwa Kongane la Viwanda TAMCO, Kibaha lina eneo lenye ukubwa wa ekari 201.63 na limeteuliwa kujenga Viwanda katika Makundi matatu aliyoyataja kuwa ni Viwanda vya madawa na vifaa tiba, viwanda vya kuunganisha magari na mitambo pamoja na viwanda vya nguo.

 

Alisema eneo hilo linahitaji miundombinu ya barabara kama kilomita 4.8 na tayari Kilomita 1.6 imeshajengwa.

 

Dr. Shombe  alieleza ,tayari eneo hilo limepelekewa umeme wa Kv 33 na TANESCO huku miundombinu ya maji ikiwa inaendelea kuboreshwa.

 

RAIS SAMIA AWATAKA VIONGOZI KUWAHUDUMIA WANANCHI

 No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Njombe katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba Mkoani humo tarehe 10 Agosti, 2022.

******************************

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imezuia kukata na kupandisha hadhi maeneo ya utawala kwa sababu yanaongeza gharama kwa Serikali.

Rais Samia amesema hayo leo wakati akihutubia wananchi wa Njombe katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba.

Aidha, Rais Samia amesema mwelekeo wa Serikali ni kunyanyua hali ya uchumi wa nchi ili kuinua hali ya maisha ya mwananchi mmoja mmoja.  

Rais Samia pia ametoa wito kwa Viongozi nchini kusimamia ipasavyo miradi inayotekelezwa na Serikali ili kuwajengea fursa Watanzania kufanya shughuli za maendeleo na kuinua kipato.

Vile vile, Rais Samia amewataka Viongozi wa Kata, Wilaya na Mikoa kuhudumia wananchi na kutatua kero zao kwa kuzingatia utawala bora.

No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria kuzindua rasmi Soko Kuu la Njombe Mjini mkoani Njombe tarehe 10 Agosti, 2022.

No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya kuzindua rasmi Soko Kuu la Njombe Mjini katika hafla iliyofanyika mkoani Njombe tarehe 10 Agosti, 2022.

 No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Njombe mara baada ya kuzindua Soko Kuu la Njombe Mjini tarehe 10 Agosti, 2022.

No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mwenyekiti wa Kampuni ya Tanganyika Wattle ltd Jaswant Singh Rai kuhusu utendaji kazi wa kiwanda hicho ikiwemo uzalishaji wa umeme ambao hutumika kiwandani hapo pamoja na kuiuzia Tanesco kwa ajili ya matumizi ya Wananchi tarehe 10 Agosti, 2022.

No description available.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wafanyabiashara wa matunda na viatu katika Soko Kuu la Njombe mara baada ya kulizindua Soko hilo tarehe 10 Agosti, 2022