Tuesday, October 22, 2019

WAKULIMA 5,000 BUKOBA KUFIKIWA NA MRADI WA KILIMO BORA CHA MIGOMBA.



Moja ya shamba darasa katika eneo la Ziwa Ikimba.
......................................
Na Alodia Dominick, Bukoba.


Wakulima wapatao 5,000 wanatarajiwa kufikiwa katika mradi wa kilimo bora cha migomba katika kata zilizopo kandokando ya ziwa Ikimba katika halmashauri ya Bukoba vijjini.

Afisa ugani Deusdedith Rweyemamu anayesimamia eneo la Ziwa Ikimba amesema kuwa mradi huo umeanza Februari mwaka huu na kwamba lengo la mradi ni kuongeza ubora katika zao la mgomba.

Rweyemamu amezitaja, kata zenye mradi huo kuwa ni Kata ya Izimbya, Rubale, Kaibanja, Kyamulaile, Ruhunga, Kikomero na Buterankuzi.


Aidha, ameongeza kwa kusema kuwa, katika kata ya Buterankuzi kuna mashamba darasa 27, ambayo husaidia wakulima kwenda kujifunza kilimo bora cha migomba na kisha kwenda kuboresha mashamba yao.

Baadhi ya wakulima ambao wako katika mradi huo wamesema kabla ya mradi huo migomba yao ilikuwa inastawisha chane mbili za ndizi lakini kwa sasa kutokana na elimu waliyoipata tayari wameanza kustawisha migomba mizuri ambayo wanatarajia itakuwa na chane kuanzia kumi na kuendelea.

Mradi huo wa ustawishaji wa migomba bora unasimamiwa na shirika la Matumaini Mapya lililopo Bukoba kupitia mradi wa life long learning for farmers (L3F) kwa kushirikiana na kituo cha utafiti Maruku

No comments:

Post a Comment