Sunday, June 30, 2019

PROF KABUDI ZIARANI FALME ZA KIARABU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akisalimiana na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan,Abu Dhabi,Umoja wa Falme za Kiarabu. June 30,2019. 

Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu zimekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika masuala ya usalama wa eneo la Ghuba na bahari ya Hindi pia kusaidia kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan,Abu Dhabi,Umoja wa Falme za Kiarabu. June 30,2019.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi,akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Umoja wa Falme za Kiarabu, Abu Dhabi. June 30,2019.
........................................


Tanzania na Nchi ya Falme za Kiarabu zimekubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika masuala ya usalama wa eneo la Ghuba na bahari ya Hindi pia kusaidia kuimarisha hali ya usalama katika nchi za Somalia na Sudan.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi alipomtembelea na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan.

Katika Mazungumzo hayo wawili hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha udugu wa muda mrefu baina ya mataifa hayo mawili ikiwa ni pamoja na kufufua mazungumzo ya Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (JPC) ambayo kwa mara ya mwisho yalifanyika katika Mji wa Abu Dhabikatika Umoja wa Falme za Kiarabu ili kufufua na kutekeleza makubaliano ikiwa ni pamoja na kuangalia fursa za kiuchumi kwa faida ya pande zote mbili.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo Waziri Palamgamba John Kabudi amesema pamoja na masuala mbalimbali waliyokubaliana pia Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Umoja wa Falme za kiarabu Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan ameahidi kufanya mazungumzo na Ubalozi wa Falme za Kiarabu uliopo Nchini Tanzania ili kuharakisha matayarisho ya Ubalozi huo kuhamia Dodoma baada ya serikali ya Tanzania kuupatia ubalozi huo eneo la kujenga ubalozi wa Nchi hiyo mjini Dodoma bure.

Waziri Kabudi ameongeza kuwa mazungumzo hayo yamekuwa ya manufaa kwa pande zote mbili na kwamba yataendelea kuimarisha mahusiano baina ya Nchi hizo mbili ikiwa ni pamoja na kufungua fursa za kibiashara kwa ajili ya maendeleo ya mataifa hayo.

Katika hatua nyingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Palamagamba John Kabudi akizungumza wakati akihitimisha ziara yake Nchini China,amesema ziara hiyo imekuwa ya manufaa kiuchumi kwa Tanzania ambapo tayari wawekezaji takribani 150 wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kwa nia ya kuangalia maeneo mbalimbali ya uwekezaji mapema mwezi septemba wakitanguliwa na ujumbe wa watu 10 mwezi Julai 2019,hii ikiwa ni kipindi kifupi sana mara baada ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuhudhuria mkutano wa kwanza wa maonesho ya uchumi na biashara kati ya China na Afrika uliofanyika katika mji wa Chanshang katika jimbo la Hunan,Nchini China.

Aidha ametanabaisha kuwa tayari wamepatikana wawekezaji wanaotaka kujenga nyumba ya kulala wageni yenye vyumba mia tatu katika mji wa Karatu ulioko mkoani Manyara kwa nia ya kuhamasisha watalii hususani kutoka China ambao wanatarajiwa kuongezeka maradufu kufuatia hatua ya Tanzania kuweka msisitizo katika kutangaza vivutio vyake vya Utalii.

Pia Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Beijing kimekubali ombi la Waziri Kabudi la kutaka kuongeza idadi ya wanafunzi watakaokwenda kusoma chuoni hapo kutoka 20 hadi kufikia idadi 40 nafasi zitakazotolewa kwa ufadhili wa chuo hicho kila mwaka ili kuandaa nguvu kazi ya kutosha wakati Tanzania ikijiandaa kuingia katika uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

MAJI SAFI NA SALAMA CHANGAMOTO KWA WATOTO WENGI MASHULENI

Eng.Patrik Kibasa Mkurugenzi Souwasa


Joyce Joliga

Songea. Bado kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa maji safi na salama katika shule za msingi hali ambayo inachangia watoto kunywa maji yasiyosalama kwa afya zao hivyo kujikuta wakiugua mara    kwa mara homa za matumbo,kuharisha ,UTI .

Tatizo la ukosefu maji safi na salama mashuleni limekuwa likiwasababishia adha wanafunzi wengi kwani baadhi wamejikuta wakishindwa kuhudhulia masomo kutokana na kuumwa   na wengine wamejikuta wakishindwa kufanya vizuri  kwenye masomo yao.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa Juni 19 2019  kwa ushirikiano wa shirika la afya duniani WHO, na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, mabilioni ya watu duniani wanaendelea kutaabika kutokana na kukosa huduma bora za maji na masuala ya usafi.

Ripoti hiyo imeainisha takwimu mpya zikionyesha kwamba mwaka 2017 watu bilioni 3 walikosa huduma za msingi kama sabuni na mahali pa kunawa mikono nyumbani , wakiwemo karibu robo tatu yao wanapatikana katika nchi zenye maendeleo duni.
Kila mwaka watoto 297,000 wa chini ya umri wa miaka mitano kufariki diunia kutokana na kuhara kunakochangiwa na ukosefu wa huduma za WASH. 

Kwa upande wake  Diwani kata ya Ruhuwiko Wilbert Mahundi , anasema tatizo la maji katika shule za msingi za kata yake ni kubwa na limechangiwa na baadhi ya shule kukatiwa maji na zingine kutokuwa na maji ya bomba  na zipo ambazo zinatumia  maji ya visima.

Anasema tayari ameziagiza kamati za shule  kujadili namna ya kuhakikisha upatikanaji wa  Vifaa vya kunywea maji wanafunzi na  kuwekea maji safi na salama shuleni ili kuweza kuwanusuru watoto dhidi ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu,tumbo ,taifodi na UTI

Anasema,Kamati hizo zijadili n .kamati za shule zimetakiwa kujadili namna ya kuhakikisha upatikanaji wa  Vifaa vya kunywea maji wanafunzi na  kuwekea maji safi na salama shuleni ili kuweza kuwanusuru watoto dhidi ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu,tumbo ,taifodi na UTI amna bora na kupeleka maazimio yao kama agenda kwenye vikao vya baraza la Kata ilizijadiliwe na kupelekwa kwenye vikao Vya baraza la madiwani zijadiliwe na kupangiwa bajeti kwa ajili ya utekelezaji huo
Aidha ,amewataka walimu wakuu na maafisa Elimu Msingi na sekondari waangalie changamoto za upatikanaji wa bili za maji ili ziingizwe kwenye capitation na kwa ajili ya kupata fedha za kulipia ili kuweza kukwepa adha ya kukatiwa  maji mara kwa mara na kuwasababishia watoto kukosa maji safi na salama shuleni.
" Huduma ya maji safi na salama ni muhimu kwa watoto wetu ilikuweza kuwaepusha na milipuko ya magonja ya kipindu pindu ,homa za matumbo,UTI na hivyo tunapaswa kuwalinda na kuwasaidia wakiwa shuleni,"Alisema Mahundi
Aidha amewataka wazazi kupitia kamati na Bodi za shule kusimamia upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na Vifaa vya kutunzia maji na vikombe Vya kunywea maji badala ya kutumia mikono
Kwa upande wake Mwanafunzi Fatuma Ally wa shule ya Msingi Ruhuwiko anasema kwa sasa wanafunzi hawapati maji safi kwani yamekatwa na hakuna vikombe vya kunywea maji hivyo wanatumia mikono pia hakuna utaratibu mzuri wa upatikanaji maji safi shuleni hapo hivyo ameuomba uongozi wa shule kuwasaidia wanafunzi wakiwa shule kupata huduma hiyo ilikuwaepusha na maradhi ya kuharisha na kuumwa ugonjwa wa matumbo.
Naye Ibrahim Hyella mkazi wa Ruhuwiko amepongeza jitihada ambazo zimeanza kuchukuliwa na  kamati ya shule kwa kushirikiana na Diwani huyo kuwa zitasaidia watoto kupata maji safi na salama na hivyo kujikinga na maradhi ya mlipuko.

Mamlaka imetumia kiasi cha Tshs 117,448,700.00 kwa ununuzi wa bomba chache, viungio vya bomba na gharama za uchimbaji naulazaji bomba kutoka kwenye mapato yake ya ndani ili kuwafikia wateja wengi waliokuwa hawapati huduma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafina Usafi wa Mazingira Manispaa ya Songea (SOUWASA) Mhandisi Patrick Kibasa,amesemawateja hao wameweza kuunganishwakatika kipindi kifupi kwa kuwa Mamlaka ilitoa punguzo maalumu kwa wateja ili kuweza kujiunga kwa gharama nafuu kisha kuendelea kulipia gharama za maunganisho zilizobaki kwa makubaliano maalumu ya kulipia katika kipindi cha miezi sita kwa kuwa huduma ilikuwa imekwisha fika katika maeneo yao.Hii ni katika kuhakikisha wananchi wote wa Manispaa ya Songea wanapata huduma ya majisafi inayotolewa na SOUWASA kwa kuangalia kipato halisi cha Mtanzania.

Mkurugenzi Mtendaji aliongezea kufafanua kuwa Serikaliya awamu ya tano imedhamiria kumtua mama ndoo ya maji kichwani hivyo Mamlaka inahakikisha wakazi wa Manispaa ya Songea wanapata huduma ya majisafi na salama uhakika.

Katika kipindi hicho cha muda mfupi, Mamlaka imeweza kuwafikia wananchi ambao maeneo yao hayakuwahi kupata huduma ya majisafi kwa kuwaunganisha kwenye mtandao wa majisafi nakuweza kuondokanana kero ya kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta maji au kutumia maji yasiyo salama ambayo yaliwasababisha magonjwa mbalimbali yaliyotokana na kutumia maji yasiyo safi na salama.

Mhandisi Patrick Kibasa amesema, wateja hao wameunganishwa kati ya Julai naDesemba 2018. Lengo ni kutoa huduma kwaasilimia 95 ifikapo mwaka 2020na kwa sasa huduma hiyo inatolewakwa asilimia 80 kwa kata za mjini zilizopo ndani ya Manispaa ya Songea.

Ili kuhakikisha upatikanaji wa maji unakua endelevu katika Manispaa ya Songea Mkurugenzi Mtendaji amesema kuwa Mamlaka inahakikisha kuwa vyanzo vya maji vinatunzwa. Mpaka sasa jumla ya miti 2,500 imepandwa katika bonde la mto Luhira na takribani zaidi ya miti 5,000 inategemewa kupandwa katika vyanzo vya mlima Matogoro katika kipindi hiki cha masika.
  zikiwemo shule  na taasisi mbalimbali