Monday, July 11, 2022

TAASISI YA JAI YAWAFARIJI WAGONJWA KWA MISAADA, SHEIKH MKOA SINGIDA ANENA MAZITO.

 No description available.

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro akimuombea dua mmoja wa wagonjwa aliyelazwa kwenye hospitali hiyo.

...............................................

Na Dotto Mwaibale, Singida

SHEIKH wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro amewaongoza wanajumuiya wa Taasisi Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) kwa kuwapatia msaada wa chakula na vinywaji wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Mkoa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa.

Taasisi hiyo ambayo inajihusisha  kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima imetoa misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Sikukuu ya Eid Al-Adha ilyofanyika leo.

Akizungumza kabla ya kutoa msaada huo, Sheikh Nassoro alisema jambo linalofanywa na taasisi hiyo ni jambo jema kwani limejaa ucha Mungu na kila mwanajumuiya hiya malipo yake yapo kwa Mwenyezi Mungu.

“Hiki mnacho kifanya ni chema mmeacha shughuli zenu, waume zenu, watoto na marafiki badala ya kusherehekea nao sikukuu hii mmeona mje kutoa faraja kwa kuwatembelea hawa wagonjwa kwa kuwaletea chakula na vinywaji hongereni sana na dhawabu yenu mtaipata,” alisema Nassoro.

Naye Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Singida, Ramadhani Mtipa alisema kila sherehe za Eid wamekuwa wakiwatembelea wagonjwa na kuwafariji kwa kuwapa chakula, vinywaji  na vitu vingine kama saburi na kuwa jumuiya hiya hiyo inaendesha shughuli zake nchi nzima.

Amirat wa Taasisi hiyo Aisha Asi alisema wamekuwa wakitoka msaada wa kuwatembelea wagonjwa, yatima na wale wasio na ndugu kwa kuwapatia msaada wa chakula bila ya kubagua  dini na kuwa kazi hiyo wamekuwa wakiifanya asubuhi na jioni.

No description available.

Wanajumuiya wa Taasisi inayojihusisha na kutoa huduma kwa wagonjwa na yatima ya  Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) wakiwa na bidhaa mbalimbali na vyakula walivyotoa msaada kwa wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Sikukuu ya Eid al-Adha 2022.

No description available.

Wanajumuiya wa Taasisi inayojihusisha na kutoa huduma kwawagonjwa na yatima ya  Jamiyatul Akhlaaqul Islam (JAI) wakiwa na bidhaa mbalimbali na vyakula walivyotoa msaada kwa wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Sikukuu ya Eid al-Adha, 2022.

No description available.

Amirat wa Taasisi hiyo Aisha Asi akitoa msaada kwa mmoja wa wagonjwa.

No description available.

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro akitoa msaada wa chakula kwa ndugu wa mgonjwa aliyelazwa kwenye hospitali hiyo.

 No description available.

Mmoja wa mtoto kutoka Taasisi hiyo (kulia) akionesha upendo wa kumpatia maji mtoto mwenzake aliyelazwa kwenye Hospitali hiyo kwa matibabu.

No description available.

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro (katikati) akiwaongoza wanajumuiya hao kwenda kutoa msaada huo