Thursday, October 10, 2019

WATANZANIA WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA WAPIGA KURA.

 
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Mzee Ally Mkongea akizungumza katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru wilayani Ruangwa yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Nangumbu wilayani humo, Oktoba 9, 2019, kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilwa.

.....................................

Na Hdija Hassan, Lindi.


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Mzee Mkongea Ally amewataka Watanzania waliokuwa na sifa ya kupiga Kura kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye dafutari la kupiga kura ili waweza kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za mitaa.


Mkongea ametoa wito huo alipokuwa akitoa ujumbe wa Mwenge wa uhuru kitaifa katika kijiji cha Nangumbu Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi kwa wananchi wa Wilaya hiyo.


Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika November 24 utahusisha wenyeviti wa mitaa, vijiji, vitongoji, wajumbe wa Halmashauri kuu na wajumbe wa Viti maalumu.


Mzee alisema swala la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni suala la kikatiba na kisheria kwamba ni haki ya kila mwananchi aliekuwa na sifa kushiriki katika Uchaguzi huo.


"Serikali za mitaa zinatambulika kutokana na Katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 , Serikali za mitaa zimekuwa zikifanya Kazi muhimu Sana katika maeneo yetu ikiwemo kushajihisha shughuli za maendeleo, kuhamasisha Wananchi kutunza mazingira, pamoja na kuhakikisha Wananchi wanaishi katika hali ya usalama na amani" Alisema Mkongea.


Awali akiwasalimia wananchi, Mbunge wa Jimbo hilo la Ruangwa ambae pia ni Waziri Mkuu wa Jmahuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, Alitumia fursa hiyo kutoa taarifa ya wananchi waliojitokeza kujiandikisha katika dafutari la kupigia kura katika Wilaya hiyo ya Ruangwa Ambapo alisema kuwa kwa siku ya Tarehe 8 Pekee jumla ya wananchi 28 elfu waliojitokeza kujiandikisha.


Pamoja na mambo mengine Majaliwa pia, aliwataka wananchi ambao wanasifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kujitokeza kugombea pamoja na kuwataka kuwaasa wapiga Kura kuchagua viongozi Bora, wachapa Kazi na waadilifu.
 

No comments:

Post a Comment