Saturday, February 26, 2022

ULEGA ATAKA VIKUNDI VYA BAGAMOYO VIKOPESHWE FEDHA ZA HALMASHAURI, KWA KUTUMIA VIZURI FURSA YA UCHUMI WA BLUU.

 No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza na wana kikundi cha ufugaji wa Majongoo Bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo, kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge.

................................................ 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kuvipatia fedha vikundi viwili vilivyopo Bagamoyo ambavyo vinajishughulisha na ufugaji wa Majongoo Bahari na kilimo cha Mwani.

Ulega ametoa agizo hilo Tarehe 25 Februari 2022 alipotembelea vikundi hivyo ili kujionea shughuli zinazofanywa na vikundi hivyo.

Naibu waziri huyo alifika Bagamoyo kufungua  kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe Bahari ambacho kilijumuisha wataalamu kutoka mikoa ya Dar es salaam na Pwani lengo likiwa ni kutoa elimu juu ya fursa zilizopo kwenye uchumi wa bluu ambao unjumuisha mazao ya Bahari ikiwemo ufugaji wa Majongoo Bahari, Ufugaji wa Kaa, ukuzaji wa Kamba kochi na kilimo cha mwani.

Kikao kazi hicho kilijumuisha kutembelea vikundi vilivyopo Kaole na Mlingotini ambavyo tayari vinatumia fursa ya uchumi wa bluu kwa kutekeleza ufugaji wa majongoo Bahari na kilimo cha mwani.

Kufuatia kazi nzuri alizoziona Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kuwapatia fedha za Halmashauri zilizotengwa kwaajili ya vikundi ili waweze kuzitumia kuendesha miradi yao.

Alisema serikali inapotoa fedha inapenda kujiridhisha juu ya utendaji kazi wa hicho kikundi ambapo kwa kikundi cha ufugaji Majongoo Bahari cha Kaole tayari kimeonyesha juhudi kwa kufanya kazi inyoonekana pamoja na kikundi cha Msichoke cha Mlingotini kinachojishughulisha na kilimo cha mwani pamoja na utengezaji wa bidhaa mbalimbali.

Wakati huo huo amemuomba mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Muharami Mkenge kuwasaidia kufuatilia upatikanaji wa nembo ya tbs kwaajili ya bidhaa wanazozalisha ili waweze kutafuta masoko nchi nzima na nje ya nchi.

Pia amemuagiza Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo kurudi Bagamoyo baada ya wiki moja ili kuwasikiliza wana vikundi hao na kuwapa ushauri wa kitaalamu na baadae kuwakopesha fedha ambazo zitatua changamoto zao.

Awali kikundi cha ufugaji majongoo bahari cha kaole kimesema kinabiliwa na changamoto ya wizi wa majongoo hivyo wanaomba kupatiwa Boti itakayowasaidia kufanya doria eneo la mradi, huku kikundi cha Msichoke cha Mlingotini nacho kimesema wanahitaji fedha zitakazowaongezea kupata mashine ya kukaushia Mwani na kusindika, pamoja na boti itakayowasidia katika shughuli za ulimaji wa mwani hasa pale maji yanapojaa.

Vikundi vyote hivyo vimeishukuru serikali ya wilaya kwa kuwapa ushirikiano wa karibu ili kufanikisha kazi zao.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa ameshika jongoo bahari wanaofugwa na kikundi cha ufugaji wa majongoo bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akisikilza taarifa ya kikundi cha ufugaji wa majongoo bahari kilichopo Kaole kata ya Dunda Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa anakunywa juisi ya Mwani iliyotengenezwa na kikundi cha Msichoke kilichopo kijiji cha Mlingotini kata ya Zinga Halmashauri ya Bagamoyo, Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, na kulia ni Katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Bagamoyo, John Francis (Bolizozo)

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza na wana kikundi cha Msichoke ambacho kinaajishughulisha na kilimo cha Mwani na utengenezaji wa bidhaa zinazotokana na zao la Mwani.

No description available.No description available.

Hizi ni baadhi ya bidhaa zinazotokana na zao Mwani, ambazo zinatenezwa na kikundi cha Msichoke kilichopo kijiji cha Mlingotini kata ya Zinga Halmashauri ya Bagamoyo.

 

Thursday, February 24, 2022

ULEGA AWATAKA VIONGOZI KUHAMASISHA WANANCHI KUHUSU UCHUMI WA BLUU.

 No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

........................................................................ 

Na Athumani Shomari, Bagamoyo.

 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka viongo mbalimbali wakiwemo wakuu wa Mikoa iliyopo ukanda wa Bahari ya hindi, kuwahamasisha wananchi ili watumie fursa za mazao ya bahari kujiongezea kipato.

 

Ulega ameyasema hayo mjini Bagamoyo leo February 24, 2022. Alipokuwa akifungua kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

 

Amesema miongoni mwa vipaumbele vya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ni pamoja na uchumi wa Bluu ambacho ni kipaumbele cha nane, na kwamba utekelezaji wake ni kusaidia kufikia kwa malengo ya Rais kukuza uchumi kwa wananchi.

 

Alifafanua kuwa uchumi wa bluu ni pamoja na kutumia mazao ya Baharini ikiwemo ufugaji wa Majongoo Bahari, ufugaji wa Kaa na Kilimo cha Mwani, ambvyo vyote hivyo soko lake ni kubwa kimataifa licha ya kuwa watu wengi wa ukanda wa Pwani hawafahamu.

 

Aliongeza kuwa, lengo la wizara ni kuona wananchi wanazifahamu fursa zinazotokana na Bahari ili wazitumie ipasavyo na kuwataka wataalamu waendelee kutoa elimu ya ufugaji wa viumbe hao wa maji ya bahari kwa wananchi.

 

Alisema mkakati uliopo wa serikali ni kutoa fedha kwa vikundi vitakavyojishughulisha na mazao hayo ili waweze kutekeleza miradi hiyo kwa ufanisi na kujiongezea kipato huku kukiwa na elimu ya namna ya utunzaji wa mazingira ya Bahari.

 

Aliendelea kusema kuwa, fursa za uchumi wa bluu katika kipengele cha Bahari ni nyingi sana lakini zinahitaji maandalizi ya namna ya kuzitumia fursa hizo ambapo amewaeleza viongozi hao kuwa, miongoni mwa maandalizi hayo ni pamoja kuwapa elimu wananchi juu ya fursa hizo huku akiwataka kuwa na vikundi vitakavyokuwa na mipango madhubuti ya maendeleo.

 

Aliongeza kwa kusema kuwa, fedha za miradi hiyo zitakapokuwa tayari hawatapewa watu ambao hawakujiandaa kitaaluma na badala yake watapewa wale ambao wamepata elimu, wameunda kikundi na kuanza utekelezaji wa mfano.

 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu waziri, amewataka wataalamu walioajiriwa na serikali kutimiza wajibu wao kwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo huku wakitoa umuhimu kwenye vipaumbele vya Rais Samia Suluhu Hassan katika kufikia malengo ya serikali.

 

Alisema wataalamu wengi wamekuwa ni wakukaa ofisini wanashindwa kutekeleza majukumu yao kwa vitendo hali inayokatisha tama hata kwa wananchi wa kawaida huku akiwataka kubadilika ili waendane na kasi Rais Samia Suluhu Hassan.

 

Aliwataka washiriki wa kikao hicho kutoka na mikakati ya utekelezaji wa majukumu ilia waweze kufikia malengo ya kuondoa umasikini kwa wananchi, kuongeza mapato ya serikali ambayo yatapelekea kufikisha huduma bora kwa wananchi.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo, akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah.

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo, wanaofuata kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga. 

No description available.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akizungumza katika ufunguzi wa kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo.

No description available. 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, akizungumza wakati wa kumkaribisha Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi katika kikao kazi cha mkakati na kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe vya baharini kwa viongozi na wataalam wa Mikoa ya Pwani na Dar es salaam kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo. kushoto ni Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga.

No description available.No description available.

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah akizungumza wakati wa kumkaribisha Mkuu wa Mkoa waPwani, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.

No description available.

No description available.

Washiriki katika kikao kazi hicho ni viongozi kutoka Dar es salaam na Pwani wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo mkoani Pwani.

 No description available.

No description available.

Washiriki katika kikao kazi hicho ni viongozi kutoka Dar es salaam na Pwani wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Bagamoyo mkoani Pwani.

No description available. 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Madiwani wa Halmashauri ya Bagamoyo na watendaji kata, kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.

No description available. 

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, akiwa katika picha ya pamoja na maafisa uvuvi, kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamed Usinga, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Muharami Mkenge, na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Shauri Selenda.