Friday, December 19, 2025

ITHIBATI YA WAANDISHI WA HABARI NI NGAO YA TAIFA KATIKA VITA.

 


Ithibati ya waandishi wa habari imeendelea kujidhihirisha kama nguzo muhimu ya ulinzi wa Taifa katika dunia ya sasa inayotawaliwa na vita ya taarifa.
 

Kupitia Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), inayotoa ithibati na vitambulisho vya uandishi wa habari kwa waandishi wenye vigezo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, Taifa linapata waandishi wanaotambulika, wanaowajibika na wanaofanya kazi kwa kufuata misingi ya taaluma, weledi na maadili. 


Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Greyson Msigwa, wakati akizungumza katika kikao kazi na waandishi wa habari kilichoratibiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) tarehe 18 Desemba 2025 jijini Dar es Salaam. 


Amesema kuwa hatua hiyo inasaidia kudhibiti upotoshaji wa taarifa na kulinda taswira ya nchi ndani na nje ya mipaka yake kwani dunia ya sasa haipigani tena vita kwa silaha za kijeshi pekee, bali kwa taarifa zinazozalishwa na kusambazwa kupitia mitandao ya kijamii.


Amesisitiza kuwa katika mazingira hayo, waandishi waliothibitishwa wanakuwa mstari wa mbele kulinda usalama wa Taifa kupitia taarifa sahihi, zenye weledi na uzalendo. 


Bw. Msigwa ameongeza kuwa kipindi kigumu kilichopita kimeonesha wazi jinsi taarifa potofu zinavyoweza kuchochea taharuki na kuathiri mshikamano wa kijamii.


Hata hivyo, amepongeza waandishi wa habari wa Tanzania, hususan wazalishaji wa maudhui mtandaoni, kwa kuonesha uzalendo na nidhamu ya taaluma kwa kutokutumia kalamu zao vibaya, licha ya shinikizo kubwa la mitandao na madai ya nje kwamba waandishi wa Tanzania ni dhaifu.


Kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali, ithibati si kikwazo cha uhuru wa habari bali ni nyenzo ya kulinda taaluma na waandishi wenyewe. Waandishi waliothibitishwa wanatambulika rasmi kama wadau wa ulinzi wa Taifa na taarifa wanazozalisha zinakuwa silaha ya kulinda amani, umoja na uthabiti wa nchi badala ya kuchochea migawanyiko.







SERIKALI YAAHIDI ULINZI NA USHIRIKIANO KWA WAANDISHI WA MTANDAONI.

 


Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kulea na kuwawezesha waandishi wa habari wa mitandaoni na mabloga, badala ya kuwashughulikia kwa mtazamo wa adhabu, ili kujenga tasnia imara na yenye tija ya habari nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, aliipongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa mwelekeo wake wa kulea wadau wa sekta ya habari badala ya kuchukua hatua kali za kinidhamu.

Msigwa alisema mwelekeo huo unaendana na falsafa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo inalenga kushirikiana na wadau mbalimbali kwa manufaa ya taifa.

Aliitaja Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jukwaa la Mitandao Tanzania (JUMIKITA) kuwa ni wadau wakubwa wa serikali katika tasnia ya habari, akisisitiza kuwa mchango wao ni muhimu katika kusambaza taarifa na kujenga mawasiliano kati ya serikali na wananchi.

“Serikali imewaamini waandishi wa mitandaoni, sasa nanyi muendelee kuonesha imani kwa serikali. Ushirikiano wetu umeendelea kuimarika na changamoto zinazojitokeza tunazitatua kwa pamoja,” alisema Msigwa.

Akikanusha madai kuwa waandishi wa habari wa mitandaoni ni dhaifu, Msigwa alisema wanatekeleza wajibu wao ipasavyo na wana nafasi kubwa ya kutumia kalamu zao kujenga taifa.

“Nimekuwa nikisisitiza waandishi tutumie kalamu zetu kujenga nchi. Mnafanya kazi sahihi na mnalinda maslahi ya taifa,” aliongeza.

Msigwa aliwahakikishia waandishi ulinzi wa serikali, akisema endapo sheria, kanuni au sera zitabainika kuwa kikwazo katika utendaji wao, zitafanyiwa marekebisho kwa maslahi mapana ya taifa.

Alitangaza pia kuanza kwa maandalizi ya mafunzo kwa waandishi wa habari kwa kushirikiana na TCRA, akiwataka kuyapokea kwa mtazamo chanya kama sehemu ya kuongeza weledi na taaluma.

Kuhusu masuala ya kodi, Msigwa alisema serikali itaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kutatua changamoto zinazowakabili waandishi wa mitandaoni, akitambua mchango wao katika kuitangaza nchi na kuvutia uwekezaji.

Aidha, alieleza kuwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ipo katika mchakato wa kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kuwawezesha waandishi wa habari, hususan wa mitandaoni.

Akizungumzia mazingira ya sasa ya kimataifa, Msigwa alisema vita vya dunia ya sasa vimehama kutoka silaha za kijeshi kwenda kwenye taarifa, akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda na kuipromote nchi.

Aliwahimiza waandishi kuhakikisha majukwaa yao yanatumika kulinda maslahi ya taifa na kuonya dhidi ya matumizi mabaya ya mitandao yanayoweza kuharibu taswira ya Tanzania.

Hata hivyo, Msigwa alionesha kusikitishwa na tabia ya baadhi ya waandishi kunyamaza wanapodhalilishwa, akiwataka kusimama na kulinda hadhi ya taaluma yao.




Thursday, December 18, 2025

HALMASHAURI YA MJI BAGAMOYO YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA WALIMU WAKUU.

 


Halmashauri ya mji wa Bagamoyo, imekabidhi vifaa vya TEHAMA kwa walimu wakuu wa shule za kata za Zinga, Dunda na Kata ya Yombo.



Makabidhiano hayo yameongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo Mhe Mohamedi Usinga  Desemba 17,2025.


Katika makabidhiano hayo Mhe Mwenyekiti amekabidhi jumla ya komputa (Desktop)44 katika Shule ya Msingi Yombo wamepata Komputa 20,shule ya Msingi Kizuiani 12 na Shule ya Zinga 12 pamoja na Komputa Mpakato moja kwa kila shule na vifaa vyake kwa ujumla.


Mhe Usinga ametoa wito kwa walimu hao kuhakikisha wanavitunza na kuvilinda vifaaa hivyo kwa ajili ya kujifunzia kwa wanafunzi mashuleni ili kuendana na kasi ya teknologia.


Vilevile Mhe Mwenyekiti ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anawezesha upatikanaji wa vifaa vya Tehama mashuleni lakini pia na kuwezesha miundombinu bora mashuleni.


Nae Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo Ndg Shauri Selenda amewasisitiza walimu hao kuhakikisha wanavitunza vifaa hivyo Pamoja na kuhakikisha wanatoa elimu iliyobora kwa wanafunzi ili kujenga msingi bora wa elimu katika Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo.


Aidha Ndg Selenda ametoa shukrani kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuhakikisha kila shule inakuwa na miundombinu bora lakini pia inapata vifaa vya kujifunzia mashuleni.


Kadhalika Afisa Elimu awali na Msingi Bi Wema Kajigili akitoa shukrani kwa niaba ya Walimu hao wote amesema kuwa “naendelea kutoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hassani Pamoja na wadau wote wa elimu nchini vifaa hivi tutahakikisha tunavitunza na kuvilinda na kuhakikisha mwanafunzi ananufaika na vifaa hivi kwa kuwapatia elimu bora”.Bi  Wema Kajigili.







Monday, December 15, 2025

RAIS SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA 9 WA CDF NA MAKAMANDA.

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekufungua mkutano wa 9 wa CDF na Makamanda uliofanyika katika Shule ya Kijeshi ya Ulinzi wa Anga (SKUA) mkoani Tanga leo tarehe 15 Desemba 2025. 







𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗬𝗔 𝗘𝗟𝗜𝗠𝗨 𝗜𝗡𝗔 𝗠𝗖𝗛𝗔𝗡𝗚𝗢 𝗠𝗞𝗨𝗕𝗪𝗔 𝗞𝗔𝗧𝗜𝗞𝗔 𝗨𝗖𝗛𝗨𝗠𝗜 𝗪𝗔 𝗧𝗔𝗜𝗙𝗔 - 𝗠𝗛𝗘. 𝗡𝗖𝗛𝗜𝗠𝗕𝗜


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa sekta ya Elimu, hususan elimu ya Juu ina mchango mkubwa  katika uchumi wa Taifa, kutokana na kuzalisha nguvukazi inayoshiriki kutoa huduma katika sekta mbalimbali.  

Mhe. Nchimbi ametoa kauli hiyo Disemba 15, 2025 Mkoani Kagera baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kampasi ya Kagera ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kutokana na mchango huo, Serikali imejizatiti kuleta mageuzi ya elimu katika ngazi zote, ili kuhakikisha kuwa wahitimu wanapata ujuzi, stadi na maarifa yanayoendana na soko la ajira. 


‘’ Rai yangu kwa UDSM, hakikisheni Kampasi hii mpya inakuwa kitovu cha uvumbuzi na ubunifu; kuwawezesha vijana wetu kuibua mawazo mapya, kufanya ubunifu, na kutumia fursa za soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki’’ Ameseama Mhe. Nchimbi.


Mhe. Nchimbi ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuratibu mradi mkubwa wa HEET kwa kuhakikisha matumizi adili ya  fedha na kwa kuzingatia thamani ya fedha. Ameitaka Wizara kushirikiana na wadau kuandaa mapema mahitaji kama vile ithibati, vifaa na rasilimaliwatu, ili kuwezesha shughuli za mafunzo katika Kampasi hiyo kuanza kama ilivyopangwa bila kuchelewa 


Pia ameipongeza UDSM, kwa kusimamia mchakato wa ujenzi wa Kampasi hiyo, ameitaka kuendelea kuwa mfano wa kuigwa katika matumizi bora ya rasilimali na utoaji wa elimu yenye tija kwa kizazi cha leo na kesho. 


" hapa niwatake wasimamizi mkabdarasi na wote wanauhusika kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa wakati uliopangwa hatutavumilia ucheleqaji wowote" anesema Mhe. Nchinbi

 

Ameishukuru Benki ya Dunia kwa kushikiriana na Serikali kufadhili utekelezaji wa mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) , ambao umewezesha ujenzi wa Kampasi ya Kagera hukua akiahidi uwekezaji katika kukamilisha jengo la abweni la wanafunzi wa kiume na miundombinu mingine muhimu.









DKT. NCHIMBI ASHIRIKI MKUTANO WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA UTATU WA ASASI YA SIASA, UKINZI NA USALAMA

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Utatu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ Troika) uliofanyika kwa njia ya mtandao akiwa Bukoba mkoani Kagera leo tarehe 15 Desemba 2025.

 


Mkutano huo umejadiili hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika kurejesha amani na usalama katika Jamhuri ya Madagascar.




Mkutano huo pia umehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe.

UN Secretary-General: Tanzania is a ‘Reference Point for Peace’, Calls for Meaningful National Dialogue Post-Election

 


"Tanzania continues to stand as a reference point for peace and social cohesion in Africa and the world."


These were the words of the United Nations Secretary-General, H.E. António Guterres, today upon receiving a Special Envoy carrying a message from the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan.


The message was delivered by the Special Envoy, H.E. Ambassador Mahmoud Kombo, the Minister of Foreign Affairs and East African Cooperation, who led the Tanzanian delegation to the United Nations Headquarters in New York.


Secretary-General Guterres noted that Tanzania’s reputation as an icon of peace was tested during the General Elections held on 29 October 2025, and acknowledged the country’s resilience in maintaining national unity and stability.


He expressed the United Nations’ strong interest in seeing Tanzania continue to remain united and serve as a positive example.


The UN Secretary-General emphasized the importance of a meaningful and inclusive national dialogue aimed at addressing the root causes of the violent incidents that occurred on 29 October 2025, and at putting in place measures to prevent their recurrence.


He also reaffirmed the United Nations’ full support to Tanzania’s ongoing efforts, including support during and after the completion of the mandate of the Commission of Inquiry established in the United Republic of Tanzania.

GUTERRES: TANZANIA NI MFANO WA AMANI DUNIANI.

 

"Tanzania inaendelea kuwa mfano wa amani na mshikamano wa kijamii barani Afrika na duniani kote."


Hayo ni maneno ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa António Guterres, alipokuwa akipokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo.


Ujumbe huo uliwasilishwa na Mjumbe Maalum, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Kombo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Katibu Mkuu Guterres alitambua kuwa sifa ya Tanzania kama nembo ya amani ilipimwa wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025. Hata hivyo, alipongeza uthabiti wa nchi katika kudumisha umoja na utulivu wa kitaifa.
Alisisitiza ni maslahi ya Umoja wa Mataifa kuiona Tanzania ikiendelea kubaki imara na kutumika kama mfano chanya.


Katibu Mkuu huyo wa UN pia alisisitiza umuhimu wa mazungumzo ya kitaifa yenye maana na jumuishi. Lengo la mazungumzo hayo ni kushughulikia mizizi ya matukio ya vurugu yaliyotokea tarehe 29 Oktoba 2025, na kuweka mikakati ya kuzuia kujirudia kwa matukio kama hayo.


Alihitimisha kwa kuthibitisha msaada kamili wa Umoja wa Mataifa kwa jitihada zinazoendelea za Tanzania, ikiwemo kutoa msaada wakati na baada ya kukamilika kwa kazi ya Tume ya Uchunguzi iliyoanzishwa nchini humo.


Tuesday, December 9, 2025

MIAKA 64 YA UHURU, TBN YATOA WITO KUDUMISHA AMANI.

 


Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa letu lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.


Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:


"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."

 

Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania


Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.


Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:


"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."


Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.

Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi


Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:


"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."


Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.


Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.

 

TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!


Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!


Beda Msimbe

Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)

Monday, December 8, 2025

KENYA YAWAKATAA WACHOCHEZI WA MAANDAMANO YA TANZANIA

 







Mkuu wa Wilaya ya Oloililai, Rift Valley nchini Kenya Mhe. Andrew Mwiti Mathew amesema serikali ya Kenya haiungi Mkono wachochezi wa vurugu, ghasia na maandamano nchini Tanzania, akiahidi kuzuia Wakenya kuchochea na kushiriki kwenye vurugu na maandamano haramu.


Mhe. Mwiti amebainisha hayo leo Disemba 08, 2025 mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, wakati wa Kikao cha ujirani mwema kilichofanyika Wilayani Longido, ikihusisha Kamati za Ulinzi za Mkoa wa Rift Valley na Mkoa wa Arusha, kama sehemu ya kuimarisha usalama na biashara kwenye eneo la mpaka wa Namanga.


"Sisi tuwahakikishie kuwa tumejipanga vizuri kuzuia wachochezi na mtu yeyote ambaye anaweza kuwa na nia ya kuja kujiunga na wale watakaokuwa wanapanga kufanya maandamano ambayo tayari tumehakikishiwa kuwa ni haramu kwani hayajaruhusiwa kisheria." Amesisitiza Mhe. Mwiti.


Awali katika maelezo yake,  Mhe. Makalla ameihakikishia Kenya kuwa serikali ya Tanzania imejipanga kikamilifu kuhakikisha hakuna vurugu wala matukio ya uvunjifu wa amani yatakayojitokeza kesho Jumanne Disemba 09, 2025, akiwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi na kijamii bila ya kuwa na wasiwasi wowote.


Mhe. Makalla kadhalika katika kikao hicho ameahidi kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kuhakikisha mpaka wa Namanga unaendelea kuwa salama pamoja na kuheshimu mipaka iliyopo na kuimarisha ufanyaji wa biashara kupitia mpaka huo ili kuleta tija kwa wananchi wa nchi hizo mbili.