Posts

WATU 16 JELA KWA MAKOSA YA WIZI, UBAKAJI.

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora JESHI la Polisi Mkoani Tabora limekamata jumla ya watuhumiwa 128 na kuwafikisha mahakamani kwa makosa mbalimbali ikiwemo wizi, ubakaji, mauaji, kujeruhi na kuharibu mali, ambapo 16 kati yao wamehukumiwa kifungo. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Twaha Lulengelule amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao na kufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.  Amefafanua kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa katika oparesheni maalumu iliyofanywa na askari polisi kuanzia Julai 1 mwaka huu hadi sasa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo kwa lengo la kuimarisha amani na usalama. Kamanda Lulengelule, amebainisha kuwa miongoni mwa watuhumiwa hao, 16 walioswekwa jela wapo waliohusika na makosa ya mauaji, ubakaji, wizi wa mali za watu, kujeruhi, kuharibu mali, kutishia kuua kwa silaha, shambulio la mwili na kutelekeza mtoto. Ametaja aliyehukumiwa kwa kosa la kubaka kuwa ni Shaban Haruna Kilingo ambaye amefungwa miaka 30 jela huku Isack Ma...

KISARAWE YAJA NA SULUHU MAHITAJI YA BARUTI, VILIPUZI NCHINI

Image
  Kiwanda Kikubwa Afrika Mashariki Kuanza Uzalishaji Septemba,2026 Dkt. Kiruswa Aahidi Serikali Kushughulikia Changamoto za Wawekezaji  DC Magoti: Kisarawe Tayari kwa Mapinduzi ya Viwanda  Kisarawe Wilaya ya Kisarawe inaendelea kujijenga kuwa kitovu cha uzalishaji wa baruti na vilipuzi nchini, kufuatia kuanzishwa kwa viwanda viwili vinavyolenga kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo ndani ya nchi na kupunguza utegemezi wa uagizaji kutoka nje. Viwanda hivyo ni Ideal Detonators Tanzania Limited, kinachotarajiwa kuwa miongoni mwa viwanda vikubwa vya aina hiyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki, na Solar Intracom Chemicals Limited. Ideal kina uwezo wa kuzalisha tani 84,000 za baruti na vipande 50,000 vya vilipuzi kwa mwaka, huku Solar kikiwa na uwezo wa kuzalisha tani 25,000 za baruti na vipande 15,000 vya vilipuzi kwa mwaka. Akizungumza wakati wa ziara yake Wilayani Kisarawe iliyolenga kukagua shughuli za madini, kufahamu changamoto za wawekezaji na kufuatilia utekelezaji wa mira...

NEEMA YAWASHUKIA WAKULIMA WA TUMBAKU

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora BODI ya Tumbaku nchini (TTB) imetangaza kuwa bei ya tumbaku msimu ujao wa kilimo itakuwa Dola za Kimarekani 2.5 kwa kilo sawa na shilingi 6,000 au zaidi kutokana na kiwango cha kubadilishia fedha (exchange rate) cha wakati huo. Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Bodi hiyo Stanley Nozya alipokuwa akiongea na Wataalamu, Wakuu wa Taasisi, Madiwani, Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ngazi ya Mkoa. Ameeleza kuwa katika msimu uliopita wakulima hawakufurahishwa na bei ya soko ambayo ilikuwa Dola za Kimarekani 1.92 sawa na shilingi 4,800 hadi 4,900 kwa kilo hali iliyoibua malalamiko mengi na wengine kugoma kuuza tumbaku yao. ‘Zao hili limekuwa likikabiliwa na changamoto nyingi kwenye soko la dunia, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, lakini serikali imeendelea kufanya juhudi kubwa, ili kuhakikisha zao hili linakuwa na tija kubwa kwa mkulima’, ameongeza. Baada ya juhudi hizo, habari njema ni hii, katika ms...

LISU AKUTWA NA KESI YA KUJIBU.

Image
  MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imemkuta Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, ana kesi ya kujibu katika shauri la uhaini linalomkabili. Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 21 Agosti 2026  baada ya Mahakama kupitia ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka unaoongozwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), na kujiridhisha kuwa ushahidi huo unatosha kumtaka mshtakiwa kutoa utetezi wake. Akisoma uamuzi huo, Jaji Ndunguru, anayeongoza jopo la majaji linalosikiliza shauri hilo, amesema Mahakama imechambua ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka na kubaini kuwa umefikia kiwango kinachomhitaji Lissu kujibu tuhuma zinazomkabili. Uamuzi huo unaashiria kuingia kwa kesi hiyo katika hatua muhimu ya utetezi, ambapo Lissu atapata fursa ya kueleza upande wake wa jambo mbele ya Mahakama. Katika hatua hiyo, upande wa utetezi utakuwa na nafasi ya kuwasilisha ushahidi wake, kutoa maelezo kuhusu tuhuma zinazomkabili pamoja na...

KAMPUNI YA ALGERIA KUWEKEZA VIWANDA VYA KOROSHO TANZANIA.

Image
  Kampuni ya ubanguaji wa korosho ya Sarl Anacard’Or ya Algeria inatarajia kutanua uwekezaji wake kwa kujenga viwanda vitatu nchini Tanzania ili kuongeza zaidi faida yake katika soko la dunia. Akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, wakati wa ziara yake kwenye kiwanda cha korosho cha kampuni hiyo jijini Oran, mmiliki na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Bw. Walid Dib, alielezea mpango wake wa kuwekeza viwanda vitatu vya kisasa vya ubanguaji wa korosho nchini ili kufaidika na fursa ya korosho ya Tanzania inayosifika kwa ubora wake duniani. “Korosho ya Tanzania ina ubora wa kipekee na tumeamua tujenge viwanda vitatu tukianzia na cha Masasi mkoani Mtwara kitakachotumia mashine za kisasa kutoka Vietnam,” alisema Bw. Dib ambaye tayari kwa kushirikiana na mbia wa ndani anakamilisha usajili wa kampuni ya kwanza itakayoitwa Kilimanjaro Nuts Limited. Akimpongeza Bw. Dib kwa kuanza mchakato wa uwekezaji nchini Tanzania, Balozi Matinyi alimuahidi kwamba seri...

JITIHADA ZA RAIS SAMIA KUIWEKA TANZANIA KAMA KITOVU CHA UCHUMI WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU KUPITIA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Image
  Na Albert Kawogo Tanzania inaendelea kujijengea nafasi muhimu katika uchumi wa Afrika Mashariki na Kati, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kuifanya nchi kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji kwa nchi za ukanda wa Maziwa Makuu. Miongoni mwa nguzo muhimu katika kufanikisha azma hiyo ni Bandari ya Dar es Salaam, ambayo imekuwa lango kuu la biashara kwa Tanzania na nchi jirani zisizo na bandari, hususan Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia na Malawi. Uwekezaji katika kuboresha miundombinu ya bandari, kuongeza ufanisi wa upakuaji na upakiaji wa mizigo, kupunguza muda wa meli kukaa bandarini na kurahisisha taratibu za forodha ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuongeza ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam. Rais Samia amekuwa akisisitiza umuhimu wa Tanzania kutumia nafasi yake ya kijiografia na miundombinu yake kuimarisha biashara ya kikanda. Kwa kuwa Tanzania ina mwambao mrefu...