Posts

KIKWETE: KARAKANA ZA SHULE ZITUMIKE KUKUZA UBUNIFU NA UJUZI WA VIJANA

Image
  Na Albert Kawogo, BAGAMOYO: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amezitaka shule kutumia ipasavyo karakana zinazojengwa katika utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa ili kuwawezesha vijana kupata ujuzi, kukuza vipaji na kujenga uwezo wa kujiajiri. Kikwete amesema karakana hizo hazipaswi kufunguliwa au kutumika wakati wa ziara za viongozi pekee, bali zinapaswa kuwa sehemu muhimu ya mazingira ya kujifunzia na kuwaandaa vijana kwa maisha ya baadaye. Amesema Taifa haliwezi kujengwa kwa kutegemea vyeti pekee, bali linahitaji watu wenye uwezo wa kutumia maarifa yao kutatua changamoto na kubadilisha changamoto hizo kuwa fursa za kiuchumi. “Endapo karakana hizi zitatumika vizuri, zitaibua fani na vipaji vya watoto na kuwafanya kuwa wabunifu, jambo ambalo litawasaidia kujiajiri na kuajirika katika maeneo mbalimbali hapa nchini,” amesema Kikwete. Waziri huyo ameyasema hayo Agosti 15 alipokuwa akizungumza katika sherehe za maadhimish...

BIL 31 KUKAMILISHA BARABARA YA LAMI KIBONDO MJINI

Image
  Na Allan Kitwe, Kibondo SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imepeleka shilingi bil 31.9 kukamilisha matengenezo ya km 25.9 za barabara ya lami ambayo ni mchepuko wa barabara kuu inayoingia Kibondo Mjini. Ujenzi wa barabara hii inayoanzia eneo la Nduta Junction kupitia vijiji vya Malolegwa, Kitahana na Twabagondozi hadi Kibondo Mjini ambayo awali iliishia kwenye makutano ya barabara ya Mabamba unatarajia kukamilika Desemba 2026. Akizungumzia na Mwandishi wa habari hizi hivi karibuni, Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Edson Edward amesema kuwa barabara hiyo ni muhimu sana kwa kuwa itarahisisha usafiri na usafirishaji bidhaa na mazao ya wananchi. Ametaja mazao makuu yanayolimwa katika Wilaya hiyo kuwa ni maharage, mahindi, parachichi na mihogo na kudokeza kuwa kukamilika kwake kutawezesha wakulima kufikisha mazao yao sokoni kwa haraka na kwa gharama nafuu zaidi. ‘Kukamilika kwa mradi huu unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 31.9 k...

DKT. MWIGULU NCHEMBA ATATUA MGOGORO MWINGINE WA ARDHI.

Image
  DKT. MWIGULU NCHEMBA ATATUA MGOGORO MWINGINE WA ARDHI. UMEDUMU MIAKA 28 GOBA DAR ES SALAAM Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba  leo Agosti 15, 2026 ameendelea kutatua  kwa njia ya maridhiano migogoro sugu  inayowakabili wananchi  na mara hii ametatua mgogoro wa ardhi  kati ya Bi. Alia Shariff na Bi Devotha  Delfina Elisei uliodumu  miaka 28 katika eneo la Goba jijini Dar es salaam . Bi. Alia Shariff, mkazi wa Dar es Salaam, alimwandikia barua  Mheshimiwa Waziri Mkuu tarehe 20 Januari 2026, akiomba amsaidie  kutatua mgogoro huo na  katika barua hiyo, alieleza kuwa eneo analolalamikia   limemilikiwa na wanae  tangu mwaka 1998 na  kwa muda wote huo ametafuta suluhu ya jambo hilo bila mafanikio.  Waziri Mkuu alituma Timu ya Watalaam kutoka Ofisini kwake ikiongozwa na Mwenyekiti ambaye pia ni Msaidizi wa Waziri Mkuu – Mahusiano, Asasi za Kiraia na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Bw. Tryphone Mkolokoti, na Katibu w...

SERIKALI YAPELEKA BIL 370 KUKARABATI RELI YA TABORA-MPANDA

Image
  Na Allan Kitwe, Kaliua SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imetoa kiasi cha shilingi bilioni 379.3 kwa ajili ya kuifanyia maboresho makubwa njia ya reli ya Tabora-Mpanda ili kumaliza kero ya usafiri kwa wananchi. Hayo yamebainishwa na Meneja wa Mradi huo, Mhandisi Paschal Kashenshe alipokuwa akitoa taarifa kwa Wajumbe wa  Kamati ya Siasa ya Mkoa waliotembelea mradi huo  Alisema kuwa mradi huo wa MGS (Meter Gauge Railway) unaanzia Wilaya ya Kaliua kwenda Mpanda ukihusisha uwekaji reli mpya ya zege yenye urefu wa km 210 za njia kuu na km 8 za kupishana. ‘Lengo la mradi huu ni kuongeza uwezo wa reli kupitisha tani 18.5 za mizigo kwa ekseli moja kutoka tani 13.5 za sasa, na kuongeza mwendo kasi kutoka km 30 kwa saa hadi 70’, alieleza. Alieleza kuwa kwa sasa treni hiyo inatumia muda wa masaa 12 kutoka Tabora kwenda Mpanda na masaa 9 kutoka Kaliua hadi Mpanda lakini utakapokamilika itatumia muda mfupi sana. ‘Tayari tumekamilisha ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza mata...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMAMOSI TAREHE 15 AGOSTI 2026

Image