WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA
WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA Na WMA - MWANZA Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Geita, Bi. Eva Ikula amesema usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo unaofanywa na WMA umewezesha bidhaa za Tanzania kuaminiwa na kukubalika zaidi katika soko la kimataifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 31, 2026 katika banda la WMA wakati wa Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, Bi. Ikula amesema mojawapo ya sababu kubwa ya bidhaa za Tanzania kukubalika katika soko la kimataifa ni uhakika wa vipimo. "Kilo yetu ni kilo ya Kenya, ya India, na ya Ujerumani pia. Hiyo ndiyo nguvu ya matumizi ya vipimo sahihi." Amesema WMA inaendelea kutoa elimu kupitia kampeni mbalimbali ili kujenga uelewa kuwa "Kipimo sahihi ni pasipoti ya bidhaa yako kuingia soko lolote duniani." Amebainisha kuwa wanunuzi wa kimataifa wanaiamini Tanzania kwa sababu WMA inatumia mfumo mmoja wa kimataifa wa vipimo ...