Posts

MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE

Image
  MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE Wananchi wa Kitongoji cha Mbalizi, Kata ya Utengule Usongwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, wamejiunga pamoja na kuanza kuchimba msingi kwa ajili ya Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Eneo la Shigamba Pipeline ambalo wananchi hao wamejitolea, ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 583, hatua inayotajwa itasaidia kuondoa adha ya watoto kuandikishwa katika shule nyingine za maeneo ya mbali. Diwani wa Kata ya Utengule Usongwe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mhe. Aidda C. Haule, ambaye ameongoza zoezi hilo kwa kushirikiana na wananchi wa makundi mbalimbali ikiwemo vijana, wanawake, na hata wazee, amesema kuwa, uwepo wa shule ya sekondari katika eneo hilo, ilikuwa ni kiu ya muda mrefu, hali ambayo imewasukuma wananchi kujitokeza kwa wingi, na kujitolea kushiriki zoezi la kuchi...

MANISPAA TABORA YAASWA KUONGEZA MAPATO

Image
  MANISPAA TABORA YAASWA KUONGEZA MAPATO Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imetakiwa kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato katika vyanzo vyake ili kufanikisha utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata zake zote. Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Upendo Wella alipokuwa akizungumza na watalaamu, watendaji, madiwani, viongozi wa chama, wawakilishi wa taasisi na vyombo vya ulinzi na usalama. Wella ameeleza kuwa licha ya kwamba serikali inapeleka fedha nyingi katika halmashauri zote kwa ajili ya utekelezaji miradi ya maendeleo, halmashauri hazipaswi kubweteka, zinatakiwa kujiongeza kwa kukusanya mapato zaidi. ‘Mapato ya halmashauri ni muhimu sana kwa kuwa yanasaidia kuharakisha utekelezaji miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ikiwemo kukamilisha miradi yote inayoanzishwa katika kila kata’, amedokeza. Amesisitiza kuwa kusuasua kwa baadhi ya miradi katika vijiji, mitaa na kata kunachagiwa na ufinyu wa bajeti lakini kama halmashauri it...

DC BAGAMOYO ATOA TAHADHARI MVUA ZA EL NINO.

Image
  DC BAGAMOYO ATOA TAHADHARI  MVUA ZA EL NINO. Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga, amewataka Viongozi na Wananchi wote kwa ujumla kuwa na Tahadhali katika maeneo Yao pamoja na kuweka mazingira katika hali ya Usafi ili kukabiliana na mvua za elinino Mhe Mkuu wa Wilaya amewataka maafisa Afya kuchukua tahadhari dhidi ya magonjwa ya Mlipuko hususani Kipindupindu ili kuepuka madhara ya mvua za Elnino  Sambamba na Hilo amewahimiza Tanesco kukagua miundombinu ya Umeme pamoja na kusimika Nguzo Mpya katika maeneo ambayo nguzo zake zimeanza kuharibika ili kukabiliana na changamoto za mvua ya elinino Pia Mkuu wa Wilaya Amewataka maafisa afya kuhakikisha wanafanya ukaguzi katika maeneo Yao pamoja na kuhakikisha maeneo yote yenye mashimo yafukwe mara moja Kama mashimo hayo hayana matumizi kwa muda huu Kwa upande wa Wazabuni wa uzoaji wa Taka kuhakikisha wanaondoa taka hizo hasa kwenye Maeneo ya mifereji na kwenda kutupa kwenye Maeneo husika  Pia Mhe Ndemanga amesema kuwa ...

MEYA MANISPAA YA KIBAHA AWATAKA WAZAZI KUIMARISHA NA KUBORESHA ELIMU KWA KUSHIRIKIANA NA WALIMU

Image
  Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dr Nicas Mawazo amewataka wazazi wa Shule zilizopo Manispaa ya Kibaha kuiga  jitihada zinazofanywa na Shule zingine katika kuimarisha na kuboresha elimu kwenye Shule zao kwa kushirikiana na walimu. Hayo ameyasema wakati wa kikao na Kamati ya Shule ya Sekondari ya Mwambisi, iliyofika katika Ofisi ya Mstahiki Meya kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimbali. Akizungumza baada ya Kamati hiyo kuwasilisha mapendekezo yao, Mstahiki Meya Dr Nicas ameipongeza Kamati hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wanafunzi wa Shule yaSekondari Mwambisi wanaendelea kufanya vizuri kwenye mitihani yao. "Nawapongeza sana Kamati ya Shule kwa jitihada kubwa mnazofanya , Shule zingine wangekuwa wanafuata utaratibu huu ina maana tungekuwa tunafanya vizuri zaidi  na zipo baadhi ya Shule zinafanya hivyo na matokeo yao yanakuwa ni mazuri," amesema Dr Nicas. Ameongeza kuwa,, Ofisi ya Mstahiki Meya itaongezea hela ya ununuzi wa mashine ya P...

MAONESHO YA MADINI YAIPAISHA LINDI KIMAPATO - MAKUSANYO YAFIKIA BILIONI 10.5

Image
  MAONESHO YA MADINI YAIPAISHA LINDI KIMAPATO - MAKUSANYO YAFIKIA BILIONI 10.5 Na Hadija omary  LINDI. Mkoa wa Lindi umeandikisha mafanikio makubwa katika Sekta ya Madini baada ya makusanyo ya maduhuli ya Serikali kuongezeka kwa zaidi ya mara nne ndani ya kipindi cha miaka sita. Hayo yamebainishwa na Afisa Madini Mkoa wa Lindi, Mhandisi Emmanuel Shija, alipozungumza kuhusu mwenendo wa sekta hiyo na maandalizi ya Maonesho Makubwa ya Kimataifa ya Madini yanayotarajiwa kufanyika Wilayani Ruangwa. Mhandisi Shija amesema kuwa kwa miaka sita iliyopita, Mkoa wa Lindi ulikuwa unakusanya maduhuli ya wastani wa Shilingi Bilioni 2.5 pekee, lakini katika mwaka wa fedha wa 2025/2026, makusanyo hayo yamepanda hadi kufikia takribani Bilioni 10.5. "Mkoa wetu wa Lindi ulikuwa unakusanya maduhuli ya Serikali Bilioni 2.5 lakini mpaka kufika mwaka uliopita wa fedha Mkoa wetu wa Lindi umeweza kukusanya Bilioni takribani 10.5," amesema Mhandisi Shija. Ameeleza kuwa ongezeko hilo linatokana na ukua...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO TAREHE 04 SEPTEMBA 2026

Image