Posts

WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA

Image
  WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA Na WMA - MWANZA  Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Geita, Bi. Eva Ikula amesema usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo unaofanywa na WMA umewezesha bidhaa za Tanzania kuaminiwa na kukubalika zaidi katika soko la kimataifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 31, 2026 katika banda la WMA wakati wa Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, Bi. Ikula amesema mojawapo  ya sababu kubwa ya bidhaa za Tanzania kukubalika katika soko la kimataifa ni uhakika wa vipimo. "Kilo yetu ni kilo ya Kenya, ya India, na ya Ujerumani pia. Hiyo ndiyo nguvu ya matumizi ya vipimo sahihi." Amesema WMA inaendelea kutoa elimu kupitia kampeni mbalimbali ili kujenga uelewa kuwa "Kipimo sahihi ni pasipoti ya bidhaa yako kuingia soko lolote duniani." Amebainisha kuwa wanunuzi wa kimataifa wanaiamini Tanzania kwa sababu WMA  inatumia mfumo mmoja wa kimataifa wa vipimo ...

MWENGE WA UHURU, WAZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI YA MILIONI 900. BUKOBA

Image
  MWENGE WA UHURU, WAZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI YA MILIONI 900. BUKOBA Alodia Dominick,  Bukoba Mwenge wa uhuru umezindua, kuweka mawe ya msingi na kutembelea miradi saba yenye thamani ya sh. milioni 900 katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera. Mwenge wa Uhuru umewasili Manispaa ya Bukoba Augosti 31, 2026 ukitokea katika wilaya ya Muleba. Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Wazo Mwang'onda akiwa Manispaa ya Bukoba amesisitiza wananchi kuilinda amani, umoja na mshikamano kwani pasipo amani hakuna miradi ya maendeleo inayoweza kutekelezwa. "Ni wajibu wetu wananchi wa Taifa hili kuilinda amani ya nchi yetu chini ya kauli mbiu isemayo Tanzania ni yetu sote tushikamane kuleta maendeleo sambamba na hiyo inatukumbushwa mapambano dhidi ya rushwa, madawa ya kulevya,  mapambano dhidi ya virusi vya ukimwi na mapambano dhidi ya maralia" amesema Mwang'onda  Ameeleza kuwa, ujumbe huo unawataka wananchi kuendelea kulinda amani na utulivu uliohasisiwa na viongozi wa nchi hi...

MAKAMU WA RAIS, ATEMBELEA OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA

Image
  MAKAMU WA RAIS, ATEMBELEA OFISI YA MAKAMU WA RAIS MUUNGANO NA MAZINGIRA AWATAKA WATUMISHI KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA     Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amewataka watumishi wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kuongeza bidii, uwajibikaji na kuachana na utendaji wa kazi kwa mazoea ili kuhakikisha majukumu ya Serikali yanatekelezwa kwa ufanisi na kwa wakati.   Makamu wa Rais ametoa wito huo leo, alipofanya ziara yake ya kwanza katika Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), iliyopo Mtumba, jijini Dodoma, ambako alipokelewa na wafanyakazi pamoja na Menejimenti ya Wizara hiyo.   Amesisitiza umuhimu wa watumishi kubadili mitazamo na namna ya kufanya kazi, akitaka kila mmoja kuwa mbunifu na kuweka mipango inayolenga kuleta matokeo yanayoonekana kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.   Makamu wa Rais amewasihi watumishi kutumia nafasi zao kutoa huduma yenye thamani kwa watanzania na kutambua dhaman...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMATATU TAREHE 31 AGOSTI 2026

Image
 

MANISPAA TABORA KULIPA MIL 27 ZA BODI YA MIKOPO

Image
 MANISPAA TABORA KULIPA MIL 27 ZA BODI YA MIKOPO Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya manispaa Tabora imetenga jumla ya shilingi milioni 27 kwa ajili ya kuwalipia watumishi wake waliosoma vyuo vikuu kwa fedha za mkopo wa Bodi ya Elimu ya Juu (HELB) kabla ya kuajiriwa. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya manispaa hiyo Dkt John Pima alipokuwa akitoa taarifa ya hesabu za mwisho (final accounts) kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo  Amesema kuwa halmashauri imetenga kiasi hicho katika bajeti yake ya mwaka huu ili kuwezesha watumishi wake walionufaika na mkopo wa serikali unaotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELB) kurejesha mikopo yao kwa wakati. ‘Haya ni maelekezo ya serikali kwa waajiri wote nchini kuhakikisha wanatambua watumishi wao waliosoma kwa fedha za mkopo wa bodi hiyo na kurejesha sehemu ya mikopo yao kila mwaka’, ameeleza.   Dkt Pima amedokeza kuwa wamekuwa wakifanya hivyo kila mwaka ili kuhakikisha kila mtumish...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMAPILI TAREHE 30 AGOSTI 2026

Image