Posts

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAKUTANA NA WATENDAJI WA WIZARA YA MADINI.

Image
  Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wamekutana na Watendaji wa Wizara ya Madini wakiongozwa na Waziri wake. Mhe. Anthony Mavunde (Mb) leo Agosti 11, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Bunge. Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Wizara ya Madini kuhusu hali ya sekta ya madini nchini, ikijumuisha uzalishaji, biashara, masoko, uwekezaji, mauzo ya nje na makusanyo ya maduhuli ya Serikali. Baada ya kupokea na kujadili taarifa hiyo, Wajumbe wa Kamati walitoa maoni yao ya kuboresha sekta ya madini nchini kuanzia kwenye uchimbaji, uuzwaji na masuala ya kodi yanayohusika katika biashara ya madini.

WAFANYABIASHARA WASISITIZWA KUTOA NA KUDAI RISITI HALALI

Image
  13 Agosti 2026, KAGERA Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kagera imeendelea kuwakumbusha wafanyabiashara umuhimu wa kutoa na kudai risiti halali za mashine za kielektroniki (EFD) kila wanapofanya mauzo, huku ikisisitiza kuwa matumizi ya risiti bandia ni kinyume cha sheria. Akizungumza katika zoezi la Alhamisi ya Mlipakodi, Meneja wa TRA Mkoa wa Kagera, CPA Joseph Mtalemwa, amewataka wafanyabiashara kuzingatia sheria na taratibu za kodi kwa kuhakikisha wanatoa risiti halali kwa wateja wao na kudai risiti wanapofanya manunuzi. CPA Mtalemwa amesema utoaji wa risiti bandia ni kosa kisheria na umewataka wafanyabiashara kutekeleza wajibu wao wa kikodi kwa uaminifu, hatua ambayo itasaidia kuimarisha uwazi katika biashara na kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Katika zoezi hilo, wafanyabiashara walipata pia fursa ya kueleza changamoto zinazowakabili katika shughuli zao za biashara pamoja na kutoa maoni na mapendekezo kuhusu maeneo wanayoona yanahitaji kuboreshwa i...

UGANDA–TANZANIA OIL PIPELINE AND REFINERY PROJECT REFLECT THE SUCCESS OF ECONOMIC DIPLOMACY

Image
  By Albert Kawogo THE Uganda–Tanzania oil pipeline project, together with plans to construct an oil refinery, represents one of the clearest examples of how economic diplomacy can be transformed into tangible development opportunities.  The cooperation between the two neighbouring countries demonstrates that diplomacy is no longer limited to political relations, official visits and bilateral agreements, but can also become a powerful instrument for attracting investment, expanding trade, strengthening energy security and creating opportunities for sustainable economic growth. The development of the East African Crude Oil Pipeline and the proposed refinery reflects the growing strategic partnership between Uganda and Tanzania in the energy sector. Both countries have recognised that cooperation in strategic economic areas can generate benefits that extend beyond their respective national borders.  By working together, Tanzania and Uganda are creating an integrated energy ...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMATANO TAREHE 12 AGOSTI 2026

Image
 

MAKAMU WA RAIS DKT. NCHIMBI AFUNGUA DAKHALIA YA SKULI YA SEKONDARI YA HASNUU MAKAME ZANZIBAR.

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Serikali itaendelea kutenga rasilimali za kutosha ili kuhakikisha skuli zote zinakuwa na miundombinu ya kisasa, walimu wenye sifa, na vifaa stahiki vya kufundishia na kujifunzia. Makamu wa Rais amesema hayo, wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Jengo la Dakhalia katika Skuli ya Sekondari ya Hasnuu Makame iliyopo Kibuteni Unguja, Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra ya Tamasha la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026). Amesema jitihada za Serikali katika kuimarisha miundombinu ya elimu ni endelevu ambazo zinajumuisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia, samani na upatikanaji wa walimu wenye sifa. Makamu wa Rais amesema lengo la uwekezaji huo, ni kuandaa vijana wenye maarifa, ubunifu na ujuzi utakao wawezesha kujitegemea na kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa Taifa.  Amewasihi kutunza Dakhali hiyo na miundombinu mingine ya elimu kwa umakini mkubwa.  Ametoa rai kwa Wananchi, Wazazi na walezi w...