Posts

TANZANIA NA DRC ZATOA MSUKUMO MPYA KATIKA MIUNDOMBINU YA USAFIRISHAJI

Image
  TANZANIA NA DRC ZATOA MSUKUMO MPYA KATIKA MIUNDOMBINU YA USAFIRISHAJI Na Albert Kawogo ZANZIBAR:  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zimeongeza msukumo katika utekelezaji wa mpango wa miundombinu jumuishi ya uchukuzi, hatua inayolenga kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya mataifa hayo mawili. Rais Samia amesema mpango huo unahusisha kuimarisha mtandao wa reli, barabara, bandari pamoja na vituo vya mizigo ili kuwezesha usafirishaji wa bidhaa kwa ufanisi zaidi kati ya Tanzania na DRC. Kwa mujibu wa Rais Samia, utekelezaji wa miundombinu hiyo ni sehemu muhimu ya juhudi za nchi hizo mbili kuhakikisha kuwa usafirishaji wa mizigo unakuwa rahisi, wa haraka na wenye gharama nafuu kwa wafanyabiashara na wawekezaji. Amesema Tanzania inaendelea kuweka mazingira bora ya miundombinu yatakayowezesha DRC kutumia kwa ufanisi njia za usafirishaji kupitia Tanzania, hususan kwa kuunganisha...

DKT. BASHIRU ALLY, AVITATKA VYAMA VYA USHIRIKA KUSAIDIA WAKULIMA.

Image
Waziri wa mifugo na uvuvi Dkt Bashiru Ally akizindua benki ya ushirika (Coop bank) tawi la Kagera ................................... Na Alodia Dominick, Bukoba Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dkt Bashiru Ally Kakurwa amevitaka vyama vya ushirika nchini kwa kushirikiana na Coop Bank kusaidia wakulima katika kuongeza thamani ya mazao yao ili waweze kujiongezea uchumi. Dkt Kakurwa ameyasema hayo Augosti 18, 2026 wakati akizindua tawi la Benki ya ushirika (Coop Bank) mkoani Kagera ambapo amesema kuwa, mazao ya wakulima yanapaswa kuongezewa thamani ili yaweze kuwapa faida na kuongeza uchumi wao. "Tuangalie maeneo yaliyosahaulika kwenye mnyororo wa thamani tuweke nguvu, serikali inatoa fedha kwa vijana wanaofuga na kuvua kisasa, lakini mazao yao yako kwenye hatari kwa sababu hatujawaunganisha kwenye mfumo wa kuhifadhi mazao yao, mfano hawana vifaa vya kutunza ubaridi" amesema Dkt. Kakurwa Ameongeza kuwa, kwa vyama vya ushirika kuna fursa kwani wana magala na majumba mengi lakini hayana ...

TANZANIA KUWA KITOVU CHA UCHAKATAJI WA MADINI TEMBO

Image
  TANZANIA KUWA KITOVU CHA UCHAKATAJI WA MADINI TEMBO Dkt.Kiruswa Ataka Ujenzi Kuharakishwa, Asisitiza Uongezaji Thamani Nchini* Tayari WanaKigamboni 278 Wameajiriwa, Zaidi ya Asilimia 90 ni Watanzania* Mwezi Julai Pekee Mkoa wa Kimadini Dar/Pwani Umekusanya Bil 4.06 Kigamboni,Dar Es Salaam Tanzania imeingia katika Hatua Mpya ya Uendelezaji wa Madini Tembo (Heavy Mineral Sands), huku shughuli za uchimbaji zikiendelea kupitia Mradi wa Fungoni- Kigamboni na Tajiri sambamba na ujenzi wa Kiwanda cha Uchakataji wa Madini hayo Mkoani Tanga. Uchimbaji na uchakataji wa Madini Tembo unatekelezwa kupitia Kampuni ya Ubia ya Nyati Mineral Sands Limited, ambapo Serikali inamiliki hisa zisizofifishwa za asilimia 16. Akizungumza leo, Agosti 18, 2026, alipotembelea na kukagua shughuli za uzalishaji wa madini hayo katika Mradi wa Fungoni- Kigamboni, pamoja na kupata taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha uchakataji Tajiri- Tanga, Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, ameitaka kampuni ...

TANZANIA, DRC KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

Image
  Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii katika maeneo ya kimkakati ikiwemo biashara na uwekezaji, kilimo, madini, nishati, usafirishaji, miundombinu, afya na teknolojia ya kidijitali. Makubaliano hayo yamefikiwa leo tarehe 18 Agosti 2026, kufuatia mazungumzo kati ya Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa DRC, Mhe. FĂ©lix Antoine Tshisekedi Tshilombo, yaliyofanyika katika Ikulu Ndogo Zanzibar. Katika biashara na uwekezaji, Rais Samia amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na DRC kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji, kurahisisha biashara ya mipakani na kuongeza uzalishaji wa bidhaa zenye thamani. Nchi hizo pia zimekubaliana kuimarisha huduma za forodha na miundombinu ya mipakani. Katika sekta ya madini, Tanzania na DRC zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika utafiti wa kijiolojia, uchimbaji, uchakataji na kuongeza thamani ya rasilimali hizo ndani ya Afrika, sambamba...

TSHISEKEDI APOKELEWA ZANZIBAR NA RAIS SAMIA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. FĂ©lix Antoine Tshisekedi Tshilombo, akipokelewa na mwenyeji wake Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika Ikulu Ndogo Zanzibar, leo tarehe 18 Agosti 2026.