Posts

KAMISHNA WA MAGEREZA MALAWI AFANYA ZIARA MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI TANZANIA.

Image
  KAMISHNA WA MAGEREZA MALAWI AFANYA ZIARA MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI TANZANIA. Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania, Kamishna wa Polisi (CP) Tatu Jumbe, Septemba 09, 2026 amepokea ugeni kutoka Magereza nchini Malawi ukiongozwa na Kamishna Milda Salilika ambaye ni Kamishna wa Urekebu na utengamanisho huduma za Magereza Malawi, uliotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Tanzania mkoani Dodoma kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna Mtandao wa Polisi Wanawake Tanzania (TPF Net) unavyofanya kazi. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, CP Tatu Jumbe ameeleza umuhimu wa kubadilishana uzoefu baina ya taasisi za ulinzi na usalama za Tanzania na Malawi, akibainisha kuwa ushirikiano wa aina hiyo unatoa fursa ya kujifunza mifumo bora na kubaini maeneo ambayo yanaweza kuboreshwa kwa manufaa ya askari na taasisi kwa ujumla. Kwa upande wake, Kamishna Milda Salilika kutoka Magereza nchini Malawi, ameeleza namna a...

KIKWETE AITAKA TANZANIA NA JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO WA CHAKULA NA UCHUMI WA BULUU

Image
  KIKWETE AITAKA TANZANIA NA JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO WA CHAKULA NA UCHUMI WA BULUU Na Albert Kawogo Jumatano 9 Septemba 2026 RAIS wa awamu ya nne , Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta za uzalishaji na usalama wa chakula, teknolojia, uvuvi na uchumi wa buluu. Dkt. Kikwete ameyasema hayo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mtafiti Mkuu wa Taasisi ya Sasakawa Peace Foundation ya Japan, Bw. Masanori Kobayashi, katika ofisi yake ndogo iliyopo Masaki, Dar es Salaam. Mazungumzo hayo yalilenga kufuatilia utekelezaji wa masuala mbalimbali yaliyoibuliwa wakati wa ziara ya kikazi ambayo Dkt. Kikwete alifanya nchini Japan kuanzia Julai 23 hadi 24, 2025. Katika ziara hiyo, Dkt. Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi sita mashuhuri kutoka Afrika walioalikwa na Serikali ya Japan kupitia taasisi za Sasakawa Peace Foundation na Nippon Foundation. Viongozi hao walishiriki katika kutoa ushauri kuhusu namna bora ya...

MAKAMU WA RAIS AAGWA RASMI NA WIZARA YA NISHATI.

Image
  MAKAMU WA RAIS AAGWA RASMI NA WIZARA YA NISHATI. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameagwa rasmi na Menejimenti ya Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zilizo chini yake katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Kambarage Treasury Square, Dodoma. Jumatano Septemba 09, 2026. Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughukia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, Menejimenti ya Wizara na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo. Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amewaasa Viongozi na Watendaji hao kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wasaidizi wake ili waendelee kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia Watanzania. Aidha, Makamu wa Rais amewataka Viongozi na Watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uzalendo ili kutimiza matarajio ya wananchi kwa...

MBUNGE WA BAGAMOYO AKABIDHI TIKETI YA NDEGE KWA KIJANA MALICK SABABU

Image
  Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. CPA Subira Khamis Mgalu, amemkabidhi tiketi ya ndege kijana wa Bagamoyo, Ndg. Malick Sababu, kwa ajili ya safari yake ya kwenda nchini Urusi, ambako amepewa fursa ya kuendelea na masomo ya Shahada ya Uzamili (Master’s) katika fani ya Geolojia (Geology). Malick Sababu ni kijana mwenyeji mkazi wa Bagamoyo kata ya Kiromo, ambaye amepata elimu yake katika Shule ya Msingi Kiromo, Ramiya Islamic Education Center kwa elimu ya Sekondari, na Bagamoyo Secondary School kwa elimu ya Kidato cha Tano na Sita.  Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ambako alifanikiwa kupata Shahada yake ya kwanza. Kwa juhudi na mafanikio yake katika masomo, Malick amepata nafasi ya kwenda nchini Urusi kwa udhamini wa Serikali ya Urusi kwa kipindi cha miaka minne, kwa ajili ya kuendelea na masomo ya Geolojia. Hata hivyo, pamoja na kupata udhamini huo, safari ya kwenda Urusi ilihitaji baadhi ya gharama ambazo alipaswa kujigharamia, jambo lililomfanya ...

SHAIBU NDEMANGA, ACHANGIA CEMENT 50 SHULE YA SIRAJULMUNIR BAGAMOYO.

Image
  SHAIBU NDEMANGA, ACHANGIA CEMENT 50 SHULE YA SIRAJULMUNIR BAGAMOYO. Na Athumani Shomari Bagamoyo. Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga amechangia mifuko 50 ya Cement kwaajili ya ujenzi wa bwalo la chakula katika shule ya Msingi Sirajulmunir iliyopo kata ya Nianjema wilayni Bagamoyo. Mkuu huyo wa wilaya ametoa Ahadi hiyo hivi karibuni, alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 16 ya wahitimu wa darasa la saba, katika shule hiyo. Akizungumza kwa niaba yake, Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya, Ibrahim Gama amesema juhudi zinazo oneshwa na shule hiyo zinapaswa kuungwa mkono na kila mpenda maendeleo ndani na nje ya Bagamoyo. Amesema Watoto wanaosoma Shule ya Sirajulmunir wana uwezo mkubwa katika masomo hali inayopelekea kila mwaka kufanya vizuri katika mitihani yao ya kuhitimu elimu ya msingi na wanakuwa Watoto wenye maadili mema katika jamii. Aliongeza kwa kusema kuwa, ufasaha wa lugha ya kingereza, kiarabu, ufaulu mzuri na maadili mema ni Ishara kubwa ya ubora wa elimu inayotolewa s...

THE ISLAMIC FOUNDATION YAMKABIDHI CHEREHANI ALIYEMALIZA KIFUNGO GEREZANI.

Image
  Taasisi ya The Islamic Foundation yenye Makao yake Makuu Mkoa wa Morogoro imetoa msaada wa cherehani kwa Issa Mohamed Kitambi, aliyemaliza kifungo cha miaka minane katika Gereza la Mahabusu Morogoro, ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono katika kuanza maisha mapya baada ya kutoka gerezani. Issa ambaye alipata mafunzo ya ushonaji akiwa gerezani, sasa anatarajiwa kutumia cherehani hiyo kuendeleza ujuzi alioupata na kujiajiri kupitia kazi ya ushonaji wa nguo. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa The Islamic Foundation, Arafat Badru, amesema wameguswa na jitihada zinazofanywa na Jeshi la Magereza za kuwapatia wafungwa mafunzo ya ujuzi, ili wanapomaliza vifungo vyao wawe na uwezo wa kujitegemea. Amesema cherehani hiyo imelenga kumpa Issa nyenzo ya kuanzia katika kazi yake na kumsaidia kuendesha maisha yake baada ya kumaliza kifungo. Akizungumza katika zoezi hilo, Mkuu wa Gereza la Mahabusu Morogoro, Mrakibu wa Jeshi la Magereza (SP) SabaS...

RC PWANI KUENDELEZA AGENDA YA UWEKEZAJI NA KUWAJENGA VIJANA KIUCHUMI

Image
  RC PWANI KUENDELEZA AGENDA YA UWEKEZAJI NA KUWAJENGA VIJANA KIUCHUMI Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo, amesema ataendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji ili kukuza uwekezaji na uchumi wa Mkoa wa Pwani, huku akisisitiza umuhimu wa kuwawezesha vijana kiuchumi. Mhe. Nyongo amesema hayo leo, Septemba 8, 2026, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Abubakar Mussa Kunenge, ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe. Amesema Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa maeneo muhimu kwa uwekezaji nchini na kwamba atashirikiana na viongozi na wadau mbalimbali kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa rafiki kwa wawekezaji. “Mkoa huu ni wa uwekezaji. Nimezunguka maeneo mbalimbali kutafuta wawekezaji, kwa hiyo niwakaribishe kwa kuweka mazingira wezeshi,” amesema Mhe. Nyongo. Aidha, Mhe. Nyongo ameomba ushirikiano wa jamii katika kuwajenga na kuwawezesha vijana kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yanayo...