Posts

MWENYEKITI WA CCM BAGAMOYO ASHIRIKI MAZISHI YA ALIYEKUWA KATIBU WA MBUNGE JIMBO LA CHALINZE MAREHEMU IDDI SWALA

Image
  Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bagamoyo  Cde. Abubakar Mlawa, ameungana na Viongozi mbalimbali wa Siasa, Serikali, Dini, Michezo, Ndugu, jamaa na mamia ya wombolezaji katika kushiriki Mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bagamoyo, Katibu wa Uchumi Wilaya na Katibu wa Mbunge Jimbo la Chalinze,  Marehemu Iddi Said Swala nyumbani kwa marehemu  Vigwaza Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani. Mwili wa marehemu Iddi Said Swala umepumzishwa leo Katika Makaburi ya familia Vigwaza. Mlawa aliwapa pole familia kwa msiba Mzito uliowapata na kuwataka wawe na uvumilivu kipindi hiki Kigumu na amewaasa waombelezaji kuendelea kushirikiana na kumuommbea marehemu Duwa ili aweze kupumzika kwa amani na Mwenyezimungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Pia aliwashukuru familia ya Marehemu Iddi Said Swala, pamoja na Wananchi wa Vigwaza, Chalinze na Bagamoyo kwa ushirikiano walioutoa wakati wa uhai wake. Aidha Mazishi hayo yalihudhuriwa na Viongozi mbalimbali...

ASKARI WA STPU PWANI WAASWA KUENDELEA KUTOA ELIMU, ILI KUPUNGUZA WIZI WA MIFUGO.

Image
  Askari wa Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo (STPU) Mkoa wa Pwani wameaswa kuendelea kujikita katika utoaji elimu hususani katika jamii za wafugaji, hatimaye kupunguza matukio ya wizi wa mifugo Mkoani humo. Akizungumza katika kikao kazi na Askari hao leo Agosti 14, 2026 Kamanda wa Polisi Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Nchini (STPU) Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Simon Pasua amesema kuwa ni vyema Askari hao wakazidi kuimarisha ulinzi katika maeneo ya ufugaji mkoani humo, huku akiwataka kujikita katika utoaji wa elimu ambayo itasaidia kupunguza uhalifu. Kamanda Pasua amesema kuwa baadhi ya wafugaji wamekuwa hawana uelewa juu ya faida ya  kuripoti kwa wakati matukio ya wizi wa mifugo, huku akiwataka askari hao kutoa elimu hiyo pamoja na kutoa elimu ya mazizi salama na ufugaji wa kisasa ambao utachangia kupunguza matukio ya wizi wa mifugo. Aidha Kamanda huyo amewaagiza Maafisa wa Polisi mkoani humo, kusimamia nidhamu ya Askari wakati wote huku akiwataka askari kujitambua...

WAKILI PETER MADELEKA ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUDHARAU AMRI YA MAHAKAMA.

Image
 

HALMASHAURI YA BAGAMOYO YATENGA SHILINGI BILIONI 2, KWA MWAKA 2026/2027.

Image
  Na Mwandishi wetu, Bagamoyo Halmashauri ya mji wa Bagamoyo kwa mwaka wa fedha 2026/2027 imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 2 ili kutekeleza miradi ya maendeleo kwa fedha za mapato ya ndani.   Akizungumza na waandishi wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya mji wa Bagamoyo, Shauri Selenda, amesema pia inatarajia kupokea fedha kiasi cha shilingi Bilioni 7 kutoka Serikali kuu, huku zaidi ya milioni 474 kutoka kwa wafadhili kwaajili ya miradi mbalimbali.   Amesema fedha hizo za mapato ya ndani zitatumika kutekeleza miradi mbalimbali kwa mwaka wa 2026/2027 huku miongoni mwa miradi hiyo ikienda kuunga juhudi za kutekeleza Dira ya Taifa ya mwaka 2050.   Alifafanua kuwa, miradi yote hiyo inalenga Kwenda kuwakwamua wananchi wakazi wa Bagamoyo katika kuboresha huduma mbalimbali na miundombinu ya mji wa Bagamoyo.   Selenda alisema mwaka 2021/2022 Halmashauri ya Bagamoyo ilikuwa inatenga fedha kiasi cha shilingi Milioni mia nane 800 lakini kwa ...

KAMATI YA BUNGE (PIC) YAITAKA TANAPA KUBORESHA UWEKEZAJI KATIKA HIFADHI ZA TAIFA.

Image
  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) Agosti 13, 2026, imelielekeza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeleza mikakati ya kuboresha uwekezaji katika maeneo ya Hifadhi za Taifa nchini, Kuboresha miundombinu, na kuongeza mazao mapya ya utalii ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania pamoja na mapato yatokanayo na shughuli za utalii. Maelekezo hayo yametolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Rashid A. Shangazi (Mb) katika kikao kilichofanyika Bungeni Dodoma kikiwa na lengo la kupitia na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa miradi ya uwekezaji katika Hifadhi za Taifa, uhifadhi, utalii pamoja na mikakati ya kuongeza mchango wa sekta ya utalii katika kukuza uchumi wa Taifa. Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba E. Mabula, viongozi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na Men...

CCM TABORA YATOA MAAGIZO KWA BODI YA TUMBAKU KUMALIZA KERO ZA WAKULIMA

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Tabora kimeitaka Bodi ya Tumbaku nchini (TTB) kuja na mikakati thabiti itakayosaidia kumaliza kero za wakulima wa zao hilo Mkoani humo na Mikoa mingine hapa nchini. Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Said Juma Nkumba alipokuwa akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa kilichofanyika jana Wilayani Kaliua Mkoani hapa. Amesema kuwa zao la tumbaku ni zao muhimu sana kwa uchumi wa wakazi wa Mkoa huo na Mikoa mingine, lakini limekuwa likikabiliwa na changamoto kadha wa kadha hali ambayo imekuwa ikilalamikiwa mno na wananchi. 'Naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali ambazo imekuwa ikichukua ili kuhakikisha kilimo kinaboreshwa na masoko ya uhakika yanapatikana’, ameeleza. Komredi Nkumba amedokeza kuwa CCM inajivunia mafanikio makubwa ambayo yameendelea kupatikana katika sekta ya kilimo na sekta nyingine na kuongeza kuwa kero w...