SERIKALI YAFAFANUA GHARAMA ZA UPIMAJI WA ARDHI.
SERIKALI YAFAFANUA GHARAMA ZA UPIMAJI WA ARDHI. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya amesema gharama za kupanga na kupima kiwanja kimoja katika maeneo yaliyoendelezwa zimepunguzwa hadi Shilingi 130,000, hatua inayolenga kupunguza mzigo wa gharama kwa wananchi. Mhe. Mmuya amesema hayo Agosti 31, 2026, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele, aliyehoji kuhusu lini Serikali itaanzisha utaratibu wa kupima ardhi kwa gharama nafuu kwa wananchi wa Kata za Isalavanu, Bumilayinga, Rungemba na Saohill. Akifafanua kuhusu gharama za upimaji, Mhe. Mmuya amesema kwa maeneo yaliyoendelezwa, gharama za upimaji hutozwa kwa kuzingatia Mwongozo wa Urasimishaji wa Mwaka 2021. Amesema kupitia mwongozo huo, gharama ya kupanga na kupima kiwanja kimoja kwa sasa ni Shilingi 130,000, ikilinganishwa na gharama za awali ambazo zilikuwa kati ya Shilingi 250,000 hadi Shilingi 400,000. “Gharama ya kupanga na kup...