Posts

RAIS. DKT. MWINYI AKUTANA NA MKURUGENZI WA TDB

Image
  Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Ally Mwinyi,  amekutana na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Trade and Development Bank (TDB), Bw. Admassu Tadesse, pamoja na ujumbe wake, kwa mazungumzo kuhusu fursa za kupata vyanzo vipya na vyenye unafuu vya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati Zanzibar. Ameeleza umuhimu wa kuangalia mifumo mbalimbali ya kifedha inayoweza kuendana na mahitaji yetu ya maendeleo, ikiwemo katika Bandari Jumuishi ya Mangapwani, nishati, mafuta na gesi, tafiti yakinifu pamoja na kuimarisha taasisi za fedha za ndani. Aidha, amezungumzia umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa umeme kupitia vyanzo vya nishati mbadala, pamoja na kupanua uwekezaji katika sekta ya makaazi, ikiwemo pendekezo la ujenzi wa nyumba 10,000 kupitia Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC). Ameeleza pia utayari wa Zanzibar kuangalia fursa za kupata wawekezaji kupitia mtandao wa TDB katika miradi yenye tija na umuhimu wa kimkakati.  TDB imemuhakikishia D...

MATUMIZI YA INTERNET NCHINI YAONGEZEKA KWA ASILIMIA 6.4 KATIKA KIPINDI CHA MIEZI MITATTU.

Image
  Matumizi ya huduma za intaneti yamezidi kuongezeka kutoka milioni 58.9 mwezi Machi 2026 hadi kufikia milioni 62.7 mwezi Juni 2026, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 6.4. Kwa mujibu wa ripoti ya Hali ya sekta ya Mawasiliano ya robo mwaka iliyoishia Juni 2026, inaonesha idadi ya utumiaji wa intaneti inatokana na laini/waya ambazo zimetumia huduma ya Intaneti angalau mara moja katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, bila kujali teknolojia iliyotumika. Ripoti hiyo imefafanua kuwa huduma ya intaneti kwa njia ya simu za mkononi inapendelewa zaidi ikiwa na jumla ya laini milioni 37.6 ikilinganishwa na huduma ya intaneti isiyohamishika. Kuongezeka kwa utumiaji wa intaneti kunatokana na ubora wa huduma na miundombinu inayowezesha upatikanaji wa mawasiliano kwa wananchi na kurahisisha utekelezaji wa shughuli za Uchumi wa kidijiti.

RAIS DKT. SAMIA ATEMBELEA MJI MKONGWE ZANZIBAR

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya mfano wa Mlango wa Zanzibar (Zanzibar door) baada ya kuwasalimia wazee wa Mji Mkongwe (Stone Town), Zanzibar, tarehe 10 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi ya mfano wa Jahazi wakati alipowatembelea Wananchi wa Jaws Corner katikati ya Mji Mkongwe, Zanzibar tarehe 10 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akicheza mchezo wa bao baada ya kuwasalimia wananchi wa Mji Mkongwe (Stone Town) katika eneo la Jaws Corner, Zanzibar, tarehe 10 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisikiliza nyimbo mbalimbali za Taarabu asilia baada ya kuwasili katika eneo la Jaws Corner katikati ya Mji Mkongwe (Stone Town), Zanzibar tarehe 10 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na vijana wa Makachu pemb...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMANNE TAREHE 11 AGOSTI 2026

Image
 

SAMIA AKUTANA NA MAASKOFU WA KATOLIKI, WAZUNGUMZA AMANI NA MUSTAKABALI WA TAIFA

Image
  Na Albert Kawogo RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekutana na kufanya mazungumzo na Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini kupitia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), katika hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na viongozi wa dini. Mazungumzo hayo yamefanyika leo, Agosti 10, 2026, katika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma, ambapo viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali ya kitaifa, yakiwemo siasa, imani, amani, mshikamano na maendeleo ya jamii. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu, mkutano huo umeangazia pia umuhimu wa kuendelea kuimarisha amani na mshikamano wa Taifa, pamoja na kujenga mustakabali wenye ustawi kwa Watanzania. Katika mazungumzo hayo, viongozi hao wamejadili nafasi ya madhehebu ya dini na viongozi wake katika kujenga jamii yenye maadili mema, uwajibikaji na mshikamano, sambamba na kuchangia juhudi za maendeleo endelevu ya Taifa. Rais Samia amewashuku...

BAGAMOYO: MJI WA KIHISTORIA UNAONGOJEA MAPINDUZI MAKUBWA YA KIUCHUMI KUPITIA BANDARI MPYA

Image
  Na Albert Kawogo BAGAMOYO, mji wenye historia kubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki, unaonekana kuelekea katika sura mpya ya maendeleo ya kiuchumi ikiwa mipango ya ujenzi na uendelezaji wa Bandari ya Bagamoyo itatekelezwa kwa ufanisi. Kwa miaka mingi, Bagamoyo imejulikana zaidi kwa historia yake ya biashara, utamaduni na urithi wa kihistoria.  Hata hivyo, mji huo sasa una nafasi ya kuongeza hadhi yake na kuwa moja ya vituo muhimu vya biashara, usafirishaji na uwekezaji nchini Tanzania. Bandsri ya Bagamoyo inatajwa kuwa miongoni mwa miradi yenye uwezo wa kubadili kwa kiasi kikubwa sura ya uchumi wa eneo hilo na kuongeza ushindani wa Tanzania katika biashara ya kimataifa. Kutoka mji wa historia hadi kitovu cha biashara Historia ya Bagamoyo imeifanya kuwa miongoni mwa miji muhimu zaidi katika historia ya Tanzania na Afrika Mashariki. Eneo hilo lilikuwa kituo muhimu cha biashara na lilihusishwa kwa karibu na safari za misafara iliyounganisha maeneo ya ndani ya Afrika na pwani ...

RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA MAASKOFU WA TEC.

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 10 Agosti 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini kupitia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.