THE ISLAMIC FOUNDATION YAMKABIDHI CHEREHANI ALIYEMALIZA KIFUNGO GEREZANI.
Taasisi ya The Islamic Foundation yenye Makao yake Makuu Mkoa wa Morogoro imetoa msaada wa cherehani kwa Issa Mohamed Kitambi, aliyemaliza kifungo cha miaka minane katika Gereza la Mahabusu Morogoro, ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono katika kuanza maisha mapya baada ya kutoka gerezani. Issa ambaye alipata mafunzo ya ushonaji akiwa gerezani, sasa anatarajiwa kutumia cherehani hiyo kuendeleza ujuzi alioupata na kujiajiri kupitia kazi ya ushonaji wa nguo. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa The Islamic Foundation, Arafat Badru, amesema wameguswa na jitihada zinazofanywa na Jeshi la Magereza za kuwapatia wafungwa mafunzo ya ujuzi, ili wanapomaliza vifungo vyao wawe na uwezo wa kujitegemea. Amesema cherehani hiyo imelenga kumpa Issa nyenzo ya kuanzia katika kazi yake na kumsaidia kuendesha maisha yake baada ya kumaliza kifungo. Akizungumza katika zoezi hilo, Mkuu wa Gereza la Mahabusu Morogoro, Mrakibu wa Jeshi la Magereza (SP) SabaS...