RAIS. DKT. MWINYI AKUTANA NA MKURUGENZI WA TDB
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Ally Mwinyi, amekutana na Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Trade and Development Bank (TDB), Bw. Admassu Tadesse, pamoja na ujumbe wake, kwa mazungumzo kuhusu fursa za kupata vyanzo vipya na vyenye unafuu vya fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati Zanzibar. Ameeleza umuhimu wa kuangalia mifumo mbalimbali ya kifedha inayoweza kuendana na mahitaji yetu ya maendeleo, ikiwemo katika Bandari Jumuishi ya Mangapwani, nishati, mafuta na gesi, tafiti yakinifu pamoja na kuimarisha taasisi za fedha za ndani. Aidha, amezungumzia umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa umeme kupitia vyanzo vya nishati mbadala, pamoja na kupanua uwekezaji katika sekta ya makaazi, ikiwemo pendekezo la ujenzi wa nyumba 10,000 kupitia Shirika la Nyumba Zanzibar (ZHC). Ameeleza pia utayari wa Zanzibar kuangalia fursa za kupata wawekezaji kupitia mtandao wa TDB katika miradi yenye tija na umuhimu wa kimkakati. TDB imemuhakikishia D...