Posts

MAKAMU WA RAIS AAGIZA HATUA ZA HARAKA KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MVUA ZA EL NIÑO

Image
  MAKAMU WA RAIS AAGIZA HATUA ZA HARAKA KUJIANDAA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MVUA ZA EL NIÑO   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameagiza Mamlaka na Taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2026.   Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo, mara baada ya kupokea taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kuhusu mvua za El- nino, katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam.   Akizungumza na Viongozi pamoja na timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizochini ya Wizara hizo, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa taasisi zote zinazohusika, kufanya kazi kwa pamoja na kuchukua hatua za tahadhari mapema ili kuzuia au ku...

WAZAZI BAGAMOYO WAPEWA ANGALIZO LA EL-NINO

Image
  Na Omary Mngindo, Lugoba JUMUIA ya Wazazi Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, imewataka wakazi wilayani humo kuwa makini katika kipindi cha mvua za Elnino zinazotarajiwa kuanza wakati wowote. Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Mohamed Mzimba akitoa salamu za Jumuiya kwenye mazishi ya Mke wa Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji cha Mindutulieni Letema Yangalai, yaliyofanyika kijijini humo. "Ukiwa na taarifa ya uwepo wa mvua hiyo unakuwa nwepesi kujua pia kujikinga, ukimuomba Mwenyeezimungu lazima ukalime na sio kukaa chini ya Mti ukisubiri chakula," alisema Mzimba. Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalumu Tarafa ya Msoga Debora Rashid aliwataka waTanzania kuendeleza upendo, huku akiwataka wapendane kuanzia kwa jirani na kwamba huo ndio upendo. "Tuangalie sisi wenyewe tupo wapi, tunafanya nini na yele tunayoyasema yanatoka kweli moyoni?  Maana wengi wanajua dhambi ni unzinzi ru, hapana hata kutokumpenda jirani yako na ndugu yako hiyo pia ni dhambi," a...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO TAREHE 11 SEPTEMBA 2026

Image