Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bagamoyo Cde. Abubakar Mlawa, ameungana na Viongozi mbalimbali wa Siasa, Serikali, Dini, Michezo, Ndugu, jamaa na mamia ya wombolezaji katika kushiriki Mazishi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bagamoyo, Katibu wa Uchumi Wilaya na Katibu wa Mbunge Jimbo la Chalinze, Marehemu Iddi Said Swala nyumbani kwa marehemu Vigwaza Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani. Mwili wa marehemu Iddi Said Swala umepumzishwa leo Katika Makaburi ya familia Vigwaza. Mlawa aliwapa pole familia kwa msiba Mzito uliowapata na kuwataka wawe na uvumilivu kipindi hiki Kigumu na amewaasa waombelezaji kuendelea kushirikiana na kumuommbea marehemu Duwa ili aweze kupumzika kwa amani na Mwenyezimungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Pia aliwashukuru familia ya Marehemu Iddi Said Swala, pamoja na Wananchi wa Vigwaza, Chalinze na Bagamoyo kwa ushirikiano walioutoa wakati wa uhai wake. Aidha Mazishi hayo yalihudhuriwa na Viongozi mbalimbali...