Posts

TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA

Image
  TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA  Na Allan Kitwe, Tabora WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani Tabora wametenga zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo mbalimbali ili kukabiliana na wingi wa mvua za el nino. Hayo yamebainishwa jana na Afisa wa Wakala huo, Mhandisi Nehemia Chacha kwa niaba ya Meneja wa TARURA Mkoa wa Tabora alipokuwa akitoa taarifa ya hali ya barabara kwenye kikao cha madiwani wa halmashauri ya manispaa. Ameeleza kuwa ili kuhakikisha miundombinu ya barabara katika manispaa hiyo inapitika wakati wote wamekamilisha ujenzi wa madaraja makubwa 2 ya kimkakati katika kata za Ndevelwa, Misha na Kabila. Mhandisi amefafanua kuwa daraja la Ndevelwa ambalo lilikuwa kero kubwa sana kwa wananchi limegharimu zaidi ya shilingi milioni 460 na limekamilika kwa asilimia 100 na sasawananchi wameanza kulitumia, kero imeisha Daraja la pili ni lile linalounganisha Kata za Misha na Kabila ambalo lil...

TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUJENGA VICHOMEA TAKA

Image
  TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUJENGA VICHOMEA TAKA   Na Allan Kitwe, Tabora TAASISI za umma na binafsi Mkoani Tabora zimetakiwa kutumia vichomea taka katika maeneo yao ili kuteketeza taka za kibaiolojia na kikemea na nyinginezo ili kulinda afya ya binadamu na mazingira yanayowazunguka. Wito huo umetolewa juzi na Meneja wa Wakala wa Maabara ya Mifugo Tanzania (TVLA) Kanda ya Magharibi, Dkt. Qwari Bura, kwenye uzinduzi wa mtambo wa kisasa wa kuchomea taka uliojengwa kwenye Ofisi za Maabara ya Mifugo. Alisema kuwa mtambo huo ni maalumu kwa ajili ya kuchomea taka hatarishi hivyo taasisi zote zinapaswa kuiga mfano huo, badala ya kuteketeza taka kwa njia za kawaida ambazo ni hatarishi kwa afya ya jamii na mazingira. Dkt. Qwari alibainisha kuwa mtambo huo una uwezo wa kuchoma hadi kilo 30 za taka ngumu na hatarishi kwa wakati mmoja. Dkt Bura alidokeza kuwa TVLA itatoa huduma hiyo bure kwa wananchi wote wanaohitaji kuchoma taka za kibaiolojia, ila taasisi za Serikali zitatakiwa kuc...

CCM YAPONGEZA MAFANIKIO MANISPAA TABORA

Image
CCM YAPONGEZA MAFANIKIO MANISPAA TABORA Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana hadi sasa ambayo yamekuwa kichocheo kikubwa cha kuboreshwa huduma za kijamii katika kata zote 29. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mjini Komredi Mohamed Katete alipokuwa akitoa salamu za chama kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichoketi leo katika ukumbi mpya wa manispaa hiyo. Katete ameeleza bayana kuwa manispaa hiyo imepiga hatua kubwa kimaendeleo kutokana na kazi nzuri iliyofanyika kwenye miradi ya maendeleo, hali ambayo imepelekea kutatuliwa changamoto za wananchi. ‘Nakupongeza sana Mstahiki Meya, ndugu yangu Gullam-Hussein Dewj, Mkurugenzi wa Manispaa Dkt John Pima, Mkuu wa Wilaya Upendo Wella, Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu wote, kwa kazi yenu njema’, amesema. Amebainisha wazi kuwa sasa hivi wananchi wanapata huduma bora za kijamii katika kata zote tofauti na hali ilivyokuwa huko nyuma, malalamiko yaliku...

BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI

Image
  BEI ZA MAFUTA SEPTEMBA ZASHUKA NCHINI Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta kwa mwezi Septemba 2026.  Bei ya petroli imeshuka kwa Shilingi 102 kwa lita, huku bei ya dizeli ikishuka kwa Shilingi 101 kwa lita. Bei hizo zitaanza kutumika kuanzia tarehe 2 Septemba 2026, saa 6:01 usiku. EWURA inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia, ambapo mabadiliko ya bei yanaendelea kuathiriwa pamoja na mambo mengine na hali ya kiusalama katika eneo la Mashariki ya Kati. Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya Mwaka 2015, bei za mafuta zinaendelea kupangwa kwa kuzingatia mfumo wa soko. Wafanyabiashara wote wa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zisizozidi bei elekezi, na wananchi wanashauriwa kutoa taarifa EWURA kwa kituo chochote cha mafuta kitakachouza zaidi ya bei elekezi.

MBUNGE WA JIMBO LA NZEGA VIJIJINI, MHESHIMIWA NETO PAUL KAPALATA AFANYA ZIARA NA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KATA YA UGEMBE.

Image
  MBUNGE WA JIMBO LA NZEGA VIJIJINI, MHESHIMIWA NETO PAUL KAPALATA AFANYA ZIARA NA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KATA YA UGEMBE. Nzega Vijijini, Nzega, Tabora. Mbunge wa Jimbo la Nzega Vijijini, Mheshimiwa Neto Paul Kapalata, ameendelea na ziara zake za kata kwa kata kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo. Katika ziara na mkutano wa hadhara wa kata uliofanyika katika kijiji cha Ugembe, mheshimiwa Kapalata aliambatana na Afisa wa tarafa ya Puge, wataalamu kutoka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA), Wakala wa Maji na Usafi Wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Kampuni ya Uzalishaji wa Umeme ya Tanzania (TANESCO) na wataalamu wa ngazi ya kata, vijiji na vitongoji husika ili kupokea kero, changamoto na maoni ya wananchi na kutoa ufafanuzi kuhusu hatua sahihi zitakazochukuliwa katika utatuzi. Akizungumza katika ziara na mkutano wa hadhara, Mheshimiwa Kapalata pamoja na wataalamu walijibu kero, changamoto na maoni ...

SERIKALI YAFAFANUA GHARAMA ZA UPIMAJI WA ARDHI.

Image
  SERIKALI YAFAFANUA GHARAMA ZA UPIMAJI WA ARDHI. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Kaspar Mmuya amesema gharama za kupanga na kupima kiwanja kimoja katika maeneo yaliyoendelezwa zimepunguzwa hadi Shilingi 130,000, hatua inayolenga kupunguza mzigo wa gharama kwa wananchi. Mhe. Mmuya amesema hayo Agosti 31, 2026, bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mafinga Mjini, Mheshimiwa Dickson Nathan Lutevele, aliyehoji kuhusu lini Serikali itaanzisha utaratibu wa kupima ardhi kwa gharama nafuu kwa wananchi wa Kata za Isalavanu, Bumilayinga, Rungemba na Saohill. Akifafanua kuhusu gharama za upimaji, Mhe. Mmuya amesema kwa maeneo yaliyoendelezwa, gharama za upimaji hutozwa kwa kuzingatia Mwongozo wa Urasimishaji wa Mwaka 2021. Amesema kupitia mwongozo huo, gharama ya kupanga na kupima kiwanja kimoja kwa sasa ni Shilingi 130,000, ikilinganishwa na gharama za awali ambazo zilikuwa kati ya Shilingi 250,000 hadi Shilingi 400,000. “Gharama ya kupanga na kup...

WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA

Image
  WMA: KILO NA LITA YA TANZANIA NI KILO NA LITA YA DUNIA Na WMA - MWANZA  Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Geita, Bi. Eva Ikula amesema usimamizi wa matumizi sahihi ya vipimo unaofanywa na WMA umewezesha bidhaa za Tanzania kuaminiwa na kukubalika zaidi katika soko la kimataifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 31, 2026 katika banda la WMA wakati wa Maonesho ya Biashara ya Afrika Mashariki yanayoendelea katika Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza, Bi. Ikula amesema mojawapo  ya sababu kubwa ya bidhaa za Tanzania kukubalika katika soko la kimataifa ni uhakika wa vipimo. "Kilo yetu ni kilo ya Kenya, ya India, na ya Ujerumani pia. Hiyo ndiyo nguvu ya matumizi ya vipimo sahihi." Amesema WMA inaendelea kutoa elimu kupitia kampeni mbalimbali ili kujenga uelewa kuwa "Kipimo sahihi ni pasipoti ya bidhaa yako kuingia soko lolote duniani." Amebainisha kuwa wanunuzi wa kimataifa wanaiamini Tanzania kwa sababu WMA  inatumia mfumo mmoja wa kimataifa wa vipimo ...