Na Omary Mngindo, Lugoba JUMUIA ya Wazazi Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, imewataka wakazi wilayani humo kuwa makini katika kipindi cha mvua za Elnino zinazotarajiwa kuanza wakati wowote. Rai hiyo imetolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Mohamed Mzimba akitoa salamu za Jumuiya kwenye mazishi ya Mke wa Mwenyekiti Mstaafu wa Kijiji cha Mindutulieni Letema Yangalai, yaliyofanyika kijijini humo. "Ukiwa na taarifa ya uwepo wa mvua hiyo unakuwa nwepesi kujua pia kujikinga, ukimuomba Mwenyeezimungu lazima ukalime na sio kukaa chini ya Mti ukisubiri chakula," alisema Mzimba. Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalumu Tarafa ya Msoga Debora Rashid aliwataka waTanzania kuendeleza upendo, huku akiwataka wapendane kuanzia kwa jirani na kwamba huo ndio upendo. "Tuangalie sisi wenyewe tupo wapi, tunafanya nini na yele tunayoyasema yanatoka kweli moyoni? Maana wengi wanajua dhambi ni unzinzi ru, hapana hata kutokumpenda jirani yako na ndugu yako hiyo pia ni dhambi," a...