Posts

OFISI YA RAIS, UTUMISHI NA UTAWALA BORA, YAMPONGEZA NDEJEMBI.

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,  Mhe.  Rdhiwani Kikwete na Ofisi yake, wampongeza Mhe. Deogratius John Ndejembi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuteuliwa kwake kuwa Makamu wa Rais na kuandika ujumbe huu. Salamu nyingi za pongezi na Dua njema toka kwangu Binafsi na Menejiment nzima ya Ofisi ya Rais , Utumishi na Utawala Bora  kuja kwako Mh. Deo Ndejembi, Makamu wa Rais wa JMT katika siku hii muhimu Unapoapa kuanza kazi kubwa ya kuisaidia Nchi yako na kumsaidia Mh. Rais kutimiza ahadi zake za Ilani kwa Watanzania. Ahadi yetu ni ushirikiano mkubwa na kuchapa Kazi kwa kiwango kikubwa sana. Kazi na utu Tunasonga mbele Kazi iendelee

GLOBAL YASAFIRISHA KUNDI LINGINE LA WANAFUNZI KWENDA NJE YA NCHI.

Image
  GLOBAL YASAFIRISHA KUNDI LINGINE LA WANAFUNZI KWENDA NJE YA NCHI. Na  Mwandishi wetu. KUNDI lingine la mamia ya wanafunzi  wa Kitanzania wameondoka nchini Jumamosi kuelekea vyuo vikuu mbalimbali kuanza masomo ya elimu ya juu kupitia Global Education Link (GEL). Wanafunzi hao walioondoka jana kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Terminal 3, jijini Dar es Salaam, wengi wao wamechagua programu zinazohusiana na sayansi, teknolojia na taaluma zinazohitajika katika dunia ya sasa, zikiwemo Computer Engineering, Cyber Security, Artificial Intelligence, Civil Engineering, programu mbalimbali za afya, sheria na biashara. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Meneja wa Tawi la Dar es Salaam, Micky Musa, amesema kuondoka kwa wanafunzi hao ni sehemu ya mpango mpana wa kuwaunganisha vijana wa Tanzania na fursa za elimu ya kimataifa. Alisema mbali na India, Global Education Link inaendelea kuwaandaa wanafunzi wengine wanaotarajiwa ku...

RAIS DKT. SAMIA AKIWA PAMOJA NA MAKAMU WA RAIS DEOGRATIUS NDEJEMBI.

Image
  Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiteta jambo na Mhe. Deogratius John Ndejembi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 29 Agosti, 2026. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye picha na Mhe. Deogratius John Ndejembi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 29 Agosti, 2026. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye picha na Mhe. Deogratius John Ndejembi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya hafla ya uapisho iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 29 Agosti, 2026. ...

MAKAMU WA RAIS AWASALIMU WANANCHI WA CHAMWINO

Image
  MAKAMU WA RAIS AWASALIMU WANANCHI WA CHAMWINO AAHIDI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU, UTII NA UZALENDO Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa dhamana ya kuwa msaidizi namba moja na kuahidi utii, uadilifu, uzalendo na uchapaji kazi.   Makamu wa Rais amesema hayo, wakati akiwasalimu wananchi wa Jimbo la Chamwino, waliojitokeza kumpokea kwa wingi nje ya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, mara baada ya kuapishwa kuwa Makamu wa Rais. Amesema ataendelea kufanya kazi ya kumsaidia Mhe.  Rais kwa uadilifu na kuwatumikia watanzania wote ili kuharakisha maendeleo.   Aidha Makamu wa Rais amesema ataendelea kuwawakilisha vyema vijana hapa nchini na kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha Tanzania inazidi kusonga mbele katika nyanja mbalimbali za maendeleo.   Akitoa salamu zake kwa wananchi hao, Makamu wa Rais amewahakikishia kuendelea kutekeleza majukumu yake...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMAMOSI TAREHE 29 AGOSTI 2026

Image
 

WATUMISHI WA AFYA KAGERA WAFANYA ZOEZI LA UTAYARI KUKABILIANA NA EBOLA

Image
  Alodia Dominick,  Bukoba,  Kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola ambao umeendelea kushambulia wananchi nchini Congo, watumishi wa afya mkoani Kagera wamepatiwa mafunzo ya utayari kwa ajili ya kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo Ebola ili ikitokea  hapa nchini wawe na uelewa mpana. Mafunzo hayo ya utayari yamefanyika Augosti 26, 2026 katika hospital ya wilaya halmashauri ya Bukoba ambapo wamefanya tukio la utayari na wataalamu wa afya  wameelezwa maswala mbalimbali ikiwemo mapokezi ya mhisiwa au mgonjwa endapo akitokea katika vituo vyao. Mafunzo ya utayari yaliyotolewa kwa wataalamu wa afya ni pamoja na jinsi ya kupokea mhisiwa wa mlipuko wa ebola na wataalamu wanapopokea mhisiwa jinsi ya kumpatia matibabu/vipimo na baada ya kutoa huduma namna ya kuvua mavazi.  Baada ya kutoa mafunzo ya utayari baadhi ya wataalamu kutoka wizara ya afya na wadau wengine wa afya wamezungumza na waandishi wa habari na kueleza maelengo ya mafunzo hayo. Afisa Muuguzi w...