Posts

MAIMAMU NA WALIMU WA MADRASA WAWEZESHWA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

Image
  Maimamu na walimu wa madrasa nchini wamepewa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao. Uwezeshaji huo umetolewa na Umoja wa Maimamu na Walimu wa Madrasa Tanzania (UMATA), kwa kushirikiana na taasisi ya Humanity Without Borders kutoka Uingereza. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kitaifa wa UMATA, Sheikh Arif Surya, amesema baadhi ya maimamu wamepewa friji kwa ajili ya biashara ya juisi na maji. Amesema wengine wamepatiwa vifaa vya kuanzisha biashara ndogondogo, ikiwemo biashara ya dawa za asili, huku wakulima wakipewa pampu na vifaa vya umwagiliaji. Sheikh Surya amesema UMATA inaendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali ndani na nje ya Tanzania katika kuwawezesha maimamu na walimu wa madrasa. Amesema kuwawezesha maimamu ni muhimu kutokana na nafasi yao katika kuwaongoza waumini katika ibada, malezi na maendeleo ya jamii.

PAUL CHACHA APIGA MARUFUKU WANAOFANYA KAMPENI MAPEMA

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewataka wanachama wake wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani au nje ya chama kutofanya kampeni za aina yoyote kabla ya wakati na kuonya kuwa atakayebainika jina lake litaondolewa. Onyo hilo limetolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Oganaizesheni, Paulo Chacha alipokuwa akihutubia umati wa wana CCM, Viongozi na wakazi wa Mkoa wa Tabora katika uwanja wa TBC mjini hapa hivi karibuni. Amesisitiza kuwa huu sio wakati wa kufanya kampeni, bali ni wakati wa kutumikia wananchi na kujenga chama, hivyo akawataka wale wote wanaoendelea kujipitisha kwa wananchi na kutoa misaada ya kijamii kuacha mara moja tabia hiyo. ‘CCM haikatazi wanachama wake kutoa misaada kwa jamii, ila imeweka utaratibu wa namna bora ya kutoa misaada hiyo ili isionekane kama ni rushwa, kama unataka kusaidia wananchi peleka kwenye Chama, chama kitawagawia’, ameeleza. Chacha ameelekeza Wenyeviti na Makatibu wa CCM wa Wilaya na Mikoa ku...

ZIARA YA RAIS TSHISEKEDI WA DRC TANZANIA, INA MAANA GANI KWA NCHI HIZI MBILI?

Image
 Na Albert Kawogo  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), FĂ©lix Antoine Tshisekedi Tshilombo ameanza ziara ya kiserikali  nchini Tanzania  kuanzia  Agosti 17, 2026  Ziara hiyo ya siku mbili ni ziara ya kimkakati inayolenga kuimarisha ushirikiano wa Tanzania na DRC, hususan katika biashara, uwekezaji, usalama na masuala ya kikanda. Kwa mtazamo mpana, ziara hii inakuja wakati ambapo DRC inaendelea kutafuta fursa zaidi za kuimarisha uchumi wake na kuboresha njia za usafirishaji wa bidhaa kutoka maeneo yake ya ndani kwenda kwenye masoko ya kimataifa.  Tanzania, kupitia bandari zake na miundombinu ya usafirishaji, ina nafasi muhimu katika kufanikisha azma hiyo. Kwa Tanzania, DRC ni soko kubwa lenye fursa nyingi katika biashara, madini, nishati, ujenzi na huduma.  Kuimarika kwa mahusiano ya kiuchumi kunaweza kuongeza biashara kati ya nchi hizi mbili na kutoa nafasi kwa wafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania kushiriki zaidi katika uchumi wa D...

BAKWATA YATANGAZA SIKUKUU YA MAULIDI NI TAREHE 25 AGOSTI 2026

Image
  Baraza Kuu la waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limetangaza sikukuu ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammadi Swala Allahu Alayhi Wasalam, kuwa ni siku ya jumanne ya tarehe 25 Agosti 2026. Katika Taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Katibu Mkuu BAKWATA, Alhaji, Nuhu Jabiri Mruma, imesema Maulidi itasomwa usiku wa siku ya jumatatu ya tarehe 24 Agosti 2026 katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es salaam.

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMATATU TAREHE 17 AGOSTI 2026

Image