Posts

THE ISLAMIC FOUNDATION YAMKABIDHI CHEREHANI ALIYEMALIZA KIFUNGO GEREZANI.

Image
  Taasisi ya The Islamic Foundation yenye Makao yake Makuu Mkoa wa Morogoro imetoa msaada wa cherehani kwa Issa Mohamed Kitambi, aliyemaliza kifungo cha miaka minane katika Gereza la Mahabusu Morogoro, ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono katika kuanza maisha mapya baada ya kutoka gerezani. Issa ambaye alipata mafunzo ya ushonaji akiwa gerezani, sasa anatarajiwa kutumia cherehani hiyo kuendeleza ujuzi alioupata na kujiajiri kupitia kazi ya ushonaji wa nguo. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa The Islamic Foundation, Arafat Badru, amesema wameguswa na jitihada zinazofanywa na Jeshi la Magereza za kuwapatia wafungwa mafunzo ya ujuzi, ili wanapomaliza vifungo vyao wawe na uwezo wa kujitegemea. Amesema cherehani hiyo imelenga kumpa Issa nyenzo ya kuanzia katika kazi yake na kumsaidia kuendesha maisha yake baada ya kumaliza kifungo. Akizungumza katika zoezi hilo, Mkuu wa Gereza la Mahabusu Morogoro, Mrakibu wa Jeshi la Magereza (SP) SabaS...

RC PWANI KUENDELEZA AGENDA YA UWEKEZAJI NA KUWAJENGA VIJANA KIUCHUMI

Image
  RC PWANI KUENDELEZA AGENDA YA UWEKEZAJI NA KUWAJENGA VIJANA KIUCHUMI Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo, amesema ataendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji ili kukuza uwekezaji na uchumi wa Mkoa wa Pwani, huku akisisitiza umuhimu wa kuwawezesha vijana kiuchumi. Mhe. Nyongo amesema hayo leo, Septemba 8, 2026, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Abubakar Mussa Kunenge, ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe. Amesema Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa maeneo muhimu kwa uwekezaji nchini na kwamba atashirikiana na viongozi na wadau mbalimbali kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa rafiki kwa wawekezaji. “Mkoa huu ni wa uwekezaji. Nimezunguka maeneo mbalimbali kutafuta wawekezaji, kwa hiyo niwakaribishe kwa kuweka mazingira wezeshi,” amesema Mhe. Nyongo. Aidha, Mhe. Nyongo ameomba ushirikiano wa jamii katika kuwajenga na kuwawezesha vijana kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yanayo...

RAIS SAMIA AKIPEWA POLE NA VIONGOZI MBALIMBALI

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi, Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba pamona na Viongozi mbali mbali wa Vyama na Serikali na Wananchi,  wakimfariji  Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walipofika nyumbani kwake Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja, kufuatia kufiwa na Mume wake Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki Dunia katika Hospitali ya Mzena Zanzibar,  tarehe 07 Sept, 2026.

PSSSF NA MTANDAO WA WANABLOGU TANZANIA (TBN) WAJENGA USHIRIKIANO WA KUONGEZA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII

Image
  Dar es Salaam Katika kile kinachoelezwa kuwa ni hatua madhubuti ya kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika Makao Makuu ya Tanzania Bloggers Network (TBN) yaliyopo Dar es Salaam, Kijitonyama na kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wakuu wa mtandao huo. Mazungumzo hayo yaliyolenga kujenga ushirikiano wa manufaa ya pande zote mbili  yamejikita katika kuimarisha uhusiano wa kisekta kwenye masuala ya habari, uelimishaji wa umma, na usambazaji wa maarifa sahihi kuhusu mifumo ya pensheni na uwekezaji nchini. Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alieleza utayari wa mtandao huo kusimama kidete kama chombo cha kutoa elimu na kusambaza maarifa sahihi kwa umma na katika nyanja za kidijitali. Hata hivyo, alisisitiza kuwa ili kufikia malengo hayo kwa ufanisi zaidi, ni muhimu wanachama wa TBN wenyewe wakapatiwa kwanza mafunzo ya kina na ya...

DC WELLA APONGEZA USIMAMIZI MZURI MIRADI YA AFYA

Image
  DC WELLA APONGEZA USIMAMIZI MZURI MIRADI YA AFYA Na Allan Kitwe, Tabora MKUU wa Wilaya ya Tabora Upendo Wella ameeleza kufurahishwa na usimamizi mzuri wa miradi ya afya iliyotekelezwa katika Kata za Ipuli na Itonjanda katika halmashauri ya manispaa ya Tabora yenye thamani ya zaidi ya shilingi mil 700. Akiongea na Wataalamu na Watendaji wa manispaa hiyo juzi DC ameeleza kuwa miradi ya afya iliyopelekwa katika Kata hizo imesimamiwa kwa weledi mkubwa na kukamilika kwa wakati na sasa wananchi wameanza kunufaika. Amebainisha kuwa serikali inaleta fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji miradi ya maendeleo ambayo hugharimu mabilioni ya fedha, lakini utekelezaji umekuwa ukisuasua kwa baadhi ya miradi kwa sababu ya usimamizi mbovu. ‘Nawapongeza sana Wataalamu wetu akiwemo Mhandisi kwa kusimamia ipasavyo miradi hii iliyotekelezwa katika Zahanati ya Manoleo (Kata ya Itonjanda) na Kituo cha Afya Maili tano katika Kata ya Ipuli, mmefanya kazi nzuri sana’, ameongeza. DC ametoa zawadi ya shiling...

MUME WA RAIS DKT. SAMIA AFARIKI DUNIA.

Image
 MUME WA RAIS DKT. SAMIA AFARIKI DUNIA. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi ametangaza kifo cha Mhe. Hafidh Ameir Hassan ambaye ni mume wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kilichotokea leo Septemba 07, 2026 majira ya saa mbili  asubuhi katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa moyo. Mipango ya mazishi inaendelea kufanyika Kizimkazi Zanzibar 

MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE

Image
  MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE Wananchi wa Kitongoji cha Mbalizi, Kata ya Utengule Usongwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, wamejiunga pamoja na kuanza kuchimba msingi kwa ajili ya Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Eneo la Shigamba Pipeline ambalo wananchi hao wamejitolea, ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 583, hatua inayotajwa itasaidia kuondoa adha ya watoto kuandikishwa katika shule nyingine za maeneo ya mbali. Diwani wa Kata ya Utengule Usongwe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mhe. Aidda C. Haule, ambaye ameongoza zoezi hilo kwa kushirikiana na wananchi wa makundi mbalimbali ikiwemo vijana, wanawake, na hata wazee, amesema kuwa, uwepo wa shule ya sekondari katika eneo hilo, ilikuwa ni kiu ya muda mrefu, hali ambayo imewasukuma wananchi kujitokeza kwa wingi, na kujitolea kushiriki zoezi la kuchi...