MWENGE WA UHURU KUWASILI KAGERA AGOSTI 30, 2026
Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Yahya Kido akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo ................... MWENGE WA UHURU KUWASILI KAGERA AGOSTI 30, 2026 Na Alodia Dominick Bukoba Miradi ya maendeleo ipatayo 54 yenye thamani ya sh bilioni 23 inatarajiwa, kuwekewa mawe ya msingi, kuzinduliwa, kukaguliwa na kufunguliwa na mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu mkoani Kagera. Akizungumza na waandishi wa habari leo Augosti 26, 2026 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Yahya Kido amesema, mwenge wa uhuru utapokelewa wilaya ya Muleba kutokea mkoa wa Geita Agosti 30,2026 na kukimbizwa katika halmadhauri nane za mkoa huo kwa umbali wa kilomita 1,230 ambapo miradi 54 yenye thamani ya sh bilioni 23 itafikiwa na mwenge huo. Kanali Kido amesema, miradi 25 itawekewa mawe ya msingi, miradi mitano itafunguliwa, miradi 11 itazinduliwa na miradi 13 itakaguliwa na miradi hiyo inajikita katika sekta ya maji, afya, elimu, miundombinu, nishati, uwezeshaji vijana kiuchumi na mazingira wezeshi kwa uwekezaj...