Posts

MWENGE WA UHURU KUWASILI KAGERA AGOSTI 30, 2026

Image
  Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Yahya Kido akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo ................... MWENGE WA UHURU KUWASILI KAGERA AGOSTI 30, 2026 Na Alodia Dominick Bukoba Miradi ya maendeleo ipatayo 54 yenye thamani ya sh bilioni 23 inatarajiwa, kuwekewa mawe ya msingi, kuzinduliwa, kukaguliwa na kufunguliwa na mbio za mwenge wa uhuru mwaka huu mkoani Kagera. Akizungumza na waandishi wa habari leo Augosti 26, 2026 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Yahya Kido amesema,  mwenge wa uhuru utapokelewa wilaya ya Muleba kutokea mkoa wa Geita Agosti 30,2026 na kukimbizwa katika halmadhauri nane za mkoa huo kwa umbali wa kilomita 1,230 ambapo miradi 54 yenye thamani ya sh bilioni 23 itafikiwa na mwenge huo. Kanali Kido amesema, miradi 25 itawekewa mawe ya msingi, miradi mitano itafunguliwa, miradi 11 itazinduliwa na miradi 13 itakaguliwa na miradi hiyo inajikita katika sekta ya maji, afya, elimu, miundombinu, nishati, uwezeshaji vijana kiuchumi na mazingira wezeshi kwa uwekezaj...

SAMIA: MAULID ITUKUMBUSHE KUISHI KWA UPENDO NA AMANI

Image
  SAMIA: MAULID ITUKUMBUSHE KUISHI KWA UPENDO NA AMANI Na Rashid Mtagaluka DAR ES SALAAM:  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kutumia maadhimisho ya Maulidi kutafakari maisha ya Mtume Muhammad (S.A.W) na kujifunza misingi ya upendo, wema na amani. Ujumbe huo wa Rais Samia umetolewa leo, Agosti 25, 2026, na Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, aliyemwakilisha Rais katika Baraza la Maulidi lililofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam. Katika ujumbe huo, Rais Samia amesema maadhimisho ya mazazi ya Mtume Muhammad yanapaswa kuwa fursa ya kuwakumbusha waumini umuhimu wa kuishi kwa upendo, amani na kutendeana mema. Amesema kutafakari maisha ya Mtume Muhammad kutawasaidia Watanzania kuona uzuri wa mafundisho yake na kuyaweka katika maisha ya kila siku. Akizungumza kwa niaba ya Rais, Dkt. Nchemba amesema serikali imedhamiria kuendelea kushirikiana na taasisi za dini katika kujenga jamii yenye maadili, ...

RAIS, DKT. SAMIA, ARIDHIA KUJIUZULU MAKAMU WA RAIS.

Image
  RAIS, DKT. SAMIA, ARIDHIA KUJIUZULU MAKAMU WA RAIS. Kufauatia kusambaa kwa Taarifa ya kujiuzu Makamu wa Rais Dkt. Emanuel Nchimbi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameridhia ombi la kujiuzulu kwake. Katika Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu kiongozi leo tarehe 25 Agosti 2026, imesema taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwingine zitachukuliwa. Mapema hii leo tarehe 25 Agosti 2026 zimesambaa taarifa ya kujiuzulu kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi.

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMAMOSI TAREHE 22 AGOSTI 2026

Image
 

WATU 16 JELA KWA MAKOSA YA WIZI, UBAKAJI.

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora JESHI la Polisi Mkoani Tabora limekamata jumla ya watuhumiwa 128 na kuwafikisha mahakamani kwa makosa mbalimbali ikiwemo wizi, ubakaji, mauaji, kujeruhi na kuharibu mali, ambapo 16 kati yao wamehukumiwa kifungo. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Twaha Lulengelule amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao na kufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.  Amefafanua kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa katika oparesheni maalumu iliyofanywa na askari polisi kuanzia Julai 1 mwaka huu hadi sasa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo kwa lengo la kuimarisha amani na usalama. Kamanda Lulengelule, amebainisha kuwa miongoni mwa watuhumiwa hao, 16 walioswekwa jela wapo waliohusika na makosa ya mauaji, ubakaji, wizi wa mali za watu, kujeruhi, kuharibu mali, kutishia kuua kwa silaha, shambulio la mwili na kutelekeza mtoto. Ametaja aliyehukumiwa kwa kosa la kubaka kuwa ni Shaban Haruna Kilingo ambaye amefungwa miaka 30 jela huku Isack Ma...

KISARAWE YAJA NA SULUHU MAHITAJI YA BARUTI, VILIPUZI NCHINI

Image
  Kiwanda Kikubwa Afrika Mashariki Kuanza Uzalishaji Septemba,2026 Dkt. Kiruswa Aahidi Serikali Kushughulikia Changamoto za Wawekezaji  DC Magoti: Kisarawe Tayari kwa Mapinduzi ya Viwanda  Kisarawe Wilaya ya Kisarawe inaendelea kujijenga kuwa kitovu cha uzalishaji wa baruti na vilipuzi nchini, kufuatia kuanzishwa kwa viwanda viwili vinavyolenga kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo ndani ya nchi na kupunguza utegemezi wa uagizaji kutoka nje. Viwanda hivyo ni Ideal Detonators Tanzania Limited, kinachotarajiwa kuwa miongoni mwa viwanda vikubwa vya aina hiyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki, na Solar Intracom Chemicals Limited. Ideal kina uwezo wa kuzalisha tani 84,000 za baruti na vipande 50,000 vya vilipuzi kwa mwaka, huku Solar kikiwa na uwezo wa kuzalisha tani 25,000 za baruti na vipande 15,000 vya vilipuzi kwa mwaka. Akizungumza wakati wa ziara yake Wilayani Kisarawe iliyolenga kukagua shughuli za madini, kufahamu changamoto za wawekezaji na kufuatilia utekelezaji wa mira...

NEEMA YAWASHUKIA WAKULIMA WA TUMBAKU

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora BODI ya Tumbaku nchini (TTB) imetangaza kuwa bei ya tumbaku msimu ujao wa kilimo itakuwa Dola za Kimarekani 2.5 kwa kilo sawa na shilingi 6,000 au zaidi kutokana na kiwango cha kubadilishia fedha (exchange rate) cha wakati huo. Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Bodi hiyo Stanley Nozya alipokuwa akiongea na Wataalamu, Wakuu wa Taasisi, Madiwani, Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ngazi ya Mkoa. Ameeleza kuwa katika msimu uliopita wakulima hawakufurahishwa na bei ya soko ambayo ilikuwa Dola za Kimarekani 1.92 sawa na shilingi 4,800 hadi 4,900 kwa kilo hali iliyoibua malalamiko mengi na wengine kugoma kuuza tumbaku yao. ‘Zao hili limekuwa likikabiliwa na changamoto nyingi kwenye soko la dunia, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, lakini serikali imeendelea kufanya juhudi kubwa, ili kuhakikisha zao hili linakuwa na tija kubwa kwa mkulima’, ameongeza. Baada ya juhudi hizo, habari njema ni hii, katika ms...