MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE
MWENYEKITI MBEYA DC ASHIRIKIANA NA WANANCHI KUCHIMBA MSINGI WA SHULE Wananchi wa Kitongoji cha Mbalizi, Kata ya Utengule Usongwe katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, wamejiunga pamoja na kuanza kuchimba msingi kwa ajili ya Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari katika Eneo la Shigamba Pipeline ambalo wananchi hao wamejitolea, ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 583, hatua inayotajwa itasaidia kuondoa adha ya watoto kuandikishwa katika shule nyingine za maeneo ya mbali. Diwani wa Kata ya Utengule Usongwe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Mhe. Aidda C. Haule, ambaye ameongoza zoezi hilo kwa kushirikiana na wananchi wa makundi mbalimbali ikiwemo vijana, wanawake, na hata wazee, amesema kuwa, uwepo wa shule ya sekondari katika eneo hilo, ilikuwa ni kiu ya muda mrefu, hali ambayo imewasukuma wananchi kujitokeza kwa wingi, na kujitolea kushiriki zoezi la kuchi...