Posts

KAMPUNI YA ALGERIA KUWEKEZA VIWANDA VYA KOROSHO TANZANIA.

Image
  Kampuni ya ubanguaji wa korosho ya Sarl Anacard’Or ya Algeria inatarajia kutanua uwekezaji wake kwa kujenga viwanda vitatu nchini Tanzania ili kuongeza zaidi faida yake katika soko la dunia. Akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, wakati wa ziara yake kwenye kiwanda cha korosho cha kampuni hiyo jijini Oran, mmiliki na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Bw. Walid Dib, alielezea mpango wake wa kuwekeza viwanda vitatu vya kisasa vya ubanguaji wa korosho nchini ili kufaidika na fursa ya korosho ya Tanzania inayosifika kwa ubora wake duniani. “Korosho ya Tanzania ina ubora wa kipekee na tumeamua tujenge viwanda vitatu tukianzia na cha Masasi mkoani Mtwara kitakachotumia mashine za kisasa kutoka Vietnam,” alisema Bw. Dib ambaye tayari kwa kushirikiana na mbia wa ndani anakamilisha usajili wa kampuni ya kwanza itakayoitwa Kilimanjaro Nuts Limited. Akimpongeza Bw. Dib kwa kuanza mchakato wa uwekezaji nchini Tanzania, Balozi Matinyi alimuahidi kwamba seri...

JITIHADA ZA RAIS SAMIA KUIWEKA TANZANIA KAMA KITOVU CHA UCHUMI WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU KUPITIA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Image
  Na Albert Kawogo Tanzania inaendelea kujijengea nafasi muhimu katika uchumi wa Afrika Mashariki na Kati, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kuifanya nchi kuwa kitovu cha biashara na usafirishaji kwa nchi za ukanda wa Maziwa Makuu. Miongoni mwa nguzo muhimu katika kufanikisha azma hiyo ni Bandari ya Dar es Salaam, ambayo imekuwa lango kuu la biashara kwa Tanzania na nchi jirani zisizo na bandari, hususan Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia na Malawi. Uwekezaji katika kuboresha miundombinu ya bandari, kuongeza ufanisi wa upakuaji na upakiaji wa mizigo, kupunguza muda wa meli kukaa bandarini na kurahisisha taratibu za forodha ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuongeza ushindani wa Bandari ya Dar es Salaam. Rais Samia amekuwa akisisitiza umuhimu wa Tanzania kutumia nafasi yake ya kijiografia na miundombinu yake kuimarisha biashara ya kikanda. Kwa kuwa Tanzania ina mwambao mrefu...

GAZETI LA MWANA HALISI LAFUNGIWA MIEZI SITA.

Image
  Dodoma, Agosti 19, 2026: Idara ya Habari (MAELEZO) imesitisha kwa miezi sita, kuanzia Agosti 19, 2026, leseni ya gazeti la MwanaHALISI kwa kukiuka sharti la leseni linalotaka vyombo vya habari kuzingatia Sheria ya Huduma za Habari (Sura ya 229) na Kanuni zake.  Uamuzi huo umetokana na habari yenye kichwa “Nchimbi agoma kujiuzulu” iliyochapishwa katika toleo Na. 571 la tarehe 6–12 Agosti 2026 bila kuzingatia usahihi, mizania na uthibitishaji wa taarifa; miongoni mwa dosari zilizobainika ni kutumia picha ya Waziri Paul Makonda na kumtaja kama Dk. Emmanuel Nchimbi, kutowahoji wahusika na kutothibitisha madai yaliyotokana na vyanzo fiche. MAELEZO imesema hatua hiyo pia imezingatia mwenendo wa gazeti hilo kurudia makosa licha ya kupewa onyo la maandishi Mei 8, 2026  baada ya makosa kama hayo kubainika katika toleo Na. 557.  Kwa kutumia mamlaka chini ya Kifungu cha 9(b), leseni imesitishwa pia kwa uzalishaji na usambazaji wa gazeti kwa njia ya kielektroniki; MwanaHALISI ...

MAGAZETI YA TANZANIA LEO JUMATANO TAREHE 19 AGOSTI 2026

Image
 

TANZANIA NA DRC ZATOA MSUKUMO MPYA KATIKA MIUNDOMBINU YA USAFIRISHAJI

Image
  TANZANIA NA DRC ZATOA MSUKUMO MPYA KATIKA MIUNDOMBINU YA USAFIRISHAJI Na Albert Kawogo ZANZIBAR:  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zimeongeza msukumo katika utekelezaji wa mpango wa miundombinu jumuishi ya uchukuzi, hatua inayolenga kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya mataifa hayo mawili. Rais Samia amesema mpango huo unahusisha kuimarisha mtandao wa reli, barabara, bandari pamoja na vituo vya mizigo ili kuwezesha usafirishaji wa bidhaa kwa ufanisi zaidi kati ya Tanzania na DRC. Kwa mujibu wa Rais Samia, utekelezaji wa miundombinu hiyo ni sehemu muhimu ya juhudi za nchi hizo mbili kuhakikisha kuwa usafirishaji wa mizigo unakuwa rahisi, wa haraka na wenye gharama nafuu kwa wafanyabiashara na wawekezaji. Amesema Tanzania inaendelea kuweka mazingira bora ya miundombinu yatakayowezesha DRC kutumia kwa ufanisi njia za usafirishaji kupitia Tanzania, hususan kwa kuunganisha...

DKT. BASHIRU ALLY, AVITATKA VYAMA VYA USHIRIKA KUSAIDIA WAKULIMA.

Image
Waziri wa mifugo na uvuvi Dkt Bashiru Ally akizindua benki ya ushirika (Coop bank) tawi la Kagera ................................... Na Alodia Dominick, Bukoba Waziri wa Mifugo na Uvuvi Dkt Bashiru Ally Kakurwa amevitaka vyama vya ushirika nchini kwa kushirikiana na Coop Bank kusaidia wakulima katika kuongeza thamani ya mazao yao ili waweze kujiongezea uchumi. Dkt Kakurwa ameyasema hayo Augosti 18, 2026 wakati akizindua tawi la Benki ya ushirika (Coop Bank) mkoani Kagera ambapo amesema kuwa, mazao ya wakulima yanapaswa kuongezewa thamani ili yaweze kuwapa faida na kuongeza uchumi wao. "Tuangalie maeneo yaliyosahaulika kwenye mnyororo wa thamani tuweke nguvu, serikali inatoa fedha kwa vijana wanaofuga na kuvua kisasa, lakini mazao yao yako kwenye hatari kwa sababu hatujawaunganisha kwenye mfumo wa kuhifadhi mazao yao, mfano hawana vifaa vya kutunza ubaridi" amesema Dkt. Kakurwa Ameongeza kuwa, kwa vyama vya ushirika kuna fursa kwani wana magala na majumba mengi lakini hayana ...

TANZANIA KUWA KITOVU CHA UCHAKATAJI WA MADINI TEMBO

Image
  TANZANIA KUWA KITOVU CHA UCHAKATAJI WA MADINI TEMBO Dkt.Kiruswa Ataka Ujenzi Kuharakishwa, Asisitiza Uongezaji Thamani Nchini* Tayari WanaKigamboni 278 Wameajiriwa, Zaidi ya Asilimia 90 ni Watanzania* Mwezi Julai Pekee Mkoa wa Kimadini Dar/Pwani Umekusanya Bil 4.06 Kigamboni,Dar Es Salaam Tanzania imeingia katika Hatua Mpya ya Uendelezaji wa Madini Tembo (Heavy Mineral Sands), huku shughuli za uchimbaji zikiendelea kupitia Mradi wa Fungoni- Kigamboni na Tajiri sambamba na ujenzi wa Kiwanda cha Uchakataji wa Madini hayo Mkoani Tanga. Uchimbaji na uchakataji wa Madini Tembo unatekelezwa kupitia Kampuni ya Ubia ya Nyati Mineral Sands Limited, ambapo Serikali inamiliki hisa zisizofifishwa za asilimia 16. Akizungumza leo, Agosti 18, 2026, alipotembelea na kukagua shughuli za uzalishaji wa madini hayo katika Mradi wa Fungoni- Kigamboni, pamoja na kupata taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha uchakataji Tajiri- Tanga, Naibu Waziri wa Madini, Dkt. Steven Kiruswa, ameitaka kampuni ...