KAMPUNI YA ALGERIA KUWEKEZA VIWANDA VYA KOROSHO TANZANIA.
Kampuni ya ubanguaji wa korosho ya Sarl Anacard’Or ya Algeria inatarajia kutanua uwekezaji wake kwa kujenga viwanda vitatu nchini Tanzania ili kuongeza zaidi faida yake katika soko la dunia. Akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, wakati wa ziara yake kwenye kiwanda cha korosho cha kampuni hiyo jijini Oran, mmiliki na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Bw. Walid Dib, alielezea mpango wake wa kuwekeza viwanda vitatu vya kisasa vya ubanguaji wa korosho nchini ili kufaidika na fursa ya korosho ya Tanzania inayosifika kwa ubora wake duniani. “Korosho ya Tanzania ina ubora wa kipekee na tumeamua tujenge viwanda vitatu tukianzia na cha Masasi mkoani Mtwara kitakachotumia mashine za kisasa kutoka Vietnam,” alisema Bw. Dib ambaye tayari kwa kushirikiana na mbia wa ndani anakamilisha usajili wa kampuni ya kwanza itakayoitwa Kilimanjaro Nuts Limited. Akimpongeza Bw. Dib kwa kuanza mchakato wa uwekezaji nchini Tanzania, Balozi Matinyi alimuahidi kwamba seri...