Thursday, October 3, 2019

OLE NASHA ACHUKIZWA NA WAFUGAJI KUKATISHA MASOMO YA WATOTO

Naibu waziri wa elimu sayansi na teknolojia wa kati kati akipiga makofi katika halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika ofisi ya kijiji  cha kigoda kilichopo kata ya Gwata katika halmashauri ya Kibaha vijini kushoto kwake ni Mbunge wa Kibaha Vijijini Haoumd Jumaa, na viongozi wengine wa kijiji hicho.
Naibu waziri wa elimu William Ole Nasha kushoto akiwa katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi pamoja na kutembelea eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa shule mpya ya kata ya Gwata, kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha vijijini Haoumd Jumaa.
(PICHA NA VICTOR MASANGU)
............................................
NA VICTOR  MASANGU, PWANI
  

Naibu Waziri wa elimu sayansi na teknolojia  Williamu Ole Nasha amechukizwa kuona vitendo vya baaadhi ya wazazi wa jamii ya wafugaji kutothamini suala la elimu na kuamua kuwaozesha watoto wao mapema na kuwatumikisha katika kazi za kuchunga mifugo.

Pia amekemea  na kulaani vikali vitendo hivyo na kuwataka kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule ili  kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano katika sekta ya elimu ikiwemo utoaji wa elimu bure.

Ole Nasha ametoa kauli hiyo  wakati wa halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa ofisi ya serikalI ya kijiji cha Kigoda kilichopo katika kata ya Gwata Wilaya ya Kibaha  sambamba na  kutembelea eneo maalumu ambalo  limetengwa  kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari  ya kata ambayo itaweza kuwa mkombozi mkubwa  kwa wanafunzi ambao wamekuwa wakitembea umbari wa kilometa nane kwenda kutafuta huduma ya elimu  katika maeneo mengine.

Aliongeza kuwa  lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuboresha sekta ya elimu katika ngazi zote hivyo kitu kikubwa ni kuhakikisha watoto wanapatiwa malezi bora ikiwemo kuwapeleka shule lengo ikiwa ni kuwapatia ujuzi na maarifa ambayo yataweza kuliletea taifa maendeleo.

No comments:

Post a Comment