Tuesday, October 15, 2019

RAIS MAGUFULI AKABIDHI RIPOTI YA MWENGE WA UHURU 2019 KWA TAKUKURU.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Naibu Kamishna wa TAKUKURU Brigedia Jenerali john Mbungo ripoti aliyokabidhiwa na kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa wakati wa hotubia  yake kwenye sherehe  za Kilele za Mbio za Mwenge, Wiki ya Vijana na Kumbukizi ya Miaka 20  ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere zilizofanyika katika Uwanja wa Michezo wa Ilulu Mjini Lindi. Oktoba 14, 2019.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihotubia  kwenye sherehe  za Kilele za Mbio za Mwenge, Wiki ya Vijana na Kumbukizi ya Miaka 20  ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika Uwanja wa Michezo wa Ilulu Mjini Lindi. Oktoba 14, 2019.
..........................................


Na Hadija Hassan, Lindi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amkabidhi mkurugenzi wa TAKUKURU Nchini Brigedia General John Mbugo, Ripoti ya miradi 107 yenye thamani ya Shilingi bilioni 90.2 ambayo ilibainika kuwa na kasoro mbalimbali na kukataliwa kuzinduliwa, kuonwa pamoja na kuwekwa mawe ya msingi na mbio za Mwenge wa Uhuru 2019.

Magufuli amekabidhi Ripoti hiyo mapema leo Oktoba14/2019 alipokuwa akiwahutubia wananchi katika hafla ya maadhimisho ya kilele cha mwenge wa Uhuru, kumbukizi ya miaka 20 ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambalage Nyerere na wiki ya Vijana kitaifa iliyofanyika katika Viwanja vya Ilulu Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi.

Rais Magufuli alimtaka Mkuu huyo wa TAKUKURU Nchini kufanya ufuatiliaji kwa kina wa taarifa hizo za miradi ikiwa ni pamoja na kumpelekea mapendekezo na namna atakavyoshughulika na watu ambao miradi yao ilibainika kuwa chini ya kiwango.

“Nakukabidhi hii ripoti ya miradi ambayo imeonekana imekuwa na dosari ambapo mbio hizi za mwenge wa Uhuru zimekataa kuzindua, kukagua pamoja na kuiwekea mawe ya msingi, kwako ukafanye uchambuzi wa kila ukurasa, kila nukta, ukachambue na wale wote watakao husika usisite kuwapeleka mahakamani na wale wengine utakaowaona wakubwa wakubwa unafikiri ni vigumu niletee ripoti yao nitashugulikanao mimi mwenyewe” Alieleza Dkt Magufuli “

"Lengo la kufanya hivi tunataka Tanzania inyooke hatuwezi tukawa tunapeleka fedha halafu wengine wanachezea tuu na ndio maana nawapongeza vijana hawa wakimbiza mwenge wa Uhuru, hawa ndio Taifa la kesho ni lazima tujenge Taifa lao, tuwaandalie mazingira ya kutawala vizuri” alisisitiza Dkt, Magufuli.

"Mara zote mbio za mwenge wa Uhuru pamoja na mambo mengine unatumika katika kufanya Tathmini ya ubora wa miradi mbali mbali ya Maendeleo pamoja na matumizi ya fedha za Umma kwenye miradi hiyo na hiyo kazi imefanyika vizuri, tumepewa taarifa ya miradi yenye dosari mbali mbali ikiwemo yenye viashiria vya ubadhilifu wa fedha na ni matumaini yangu kwamba ofisi ya Waziri Mkuu pia itafuatilia miradi hii” aliongeza Dkt Mgufuli.

Awali waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera , vijana na Watu wenye ulemavu Jenista Muhagama alisema miradi 107 yenye thamani ya Shilingi bilioni 90.2 katika halmashauri za wilaya 82 ilitiliwa mashaka na hatimae kushindwa kuzinduliwa ama kutowekewa mawe ya msingi.


Mhagama alizitaja baadhi ya kasoro zilizoainishwa na mbio za mwenge wa Uhuru ni pamoja na eneo la Matumizi ya fedha nyingi yasiyoendana na thamani halisi ya Mradi husika, Miradi kujengwa kinyume na mikataba ya ujenzi na makadilio yaliyopitishwa na wataalamu (BOQ), wakandarasi kushindwa kufuata na kusimamia kanuni za ujenzi zilizoainishwa kwenye BOQ katika baadhi ya Miradi inayojengwa na hivyo kufanya Ubora wa miradi hiyo kutia shaka hasa katika swala la uimara na uwendelevu wa miradi hiyo.


Alizitaja kasoro zingine kuwa ni matumizi ya vifaa duni vya ujenzi katika miradi ya Umma iliyogharimu Fedha nyingi, wahandisi katika baadhi ya halmashauri kutowasimamia vizuri wakandarasi jambo linalotia shaka juu ya utekelezaji wa majukumu ya watumishi hao, Wakandarasi kutomaliza miradi wanayopewa kwa wakati na mamlaka husika kutokuwachukulia hatua za kisheria na kuacha miradi inaendelea kuzagaa bila kukamilika kwa muda mrefu.


Kasoro zingine ni ubora wa miradi usioridhisha kabisa katika baadhi ya miradi ya maji hasa ujenzi wa visima vya juu vya kuhifadhia Maji ambavyo kuta zake zimetapakaa nyufa na kuchakaa kabla ya miradi hiyo kuanza kutumika, udanganyifu unaojificha katika lugha za kitaalam hasa katika miradi ya Maji na Miradi ya Ujenzi.

Hali hiyo inakuwa vigumu kwa viongozi ambao hawana utaalamu kubaini matumizi ya Fedha za Umma zilizotumika vibaya kwa kichaka hicho, vitendo visivyo vya kizalendo vya kufanya makadilio ya ujenzi wa miradi (BOQ) zisizoendana na gharama zilizosokoni zinazofanywa na baadhi ya wahandisi wa Halmashauri katika miradi inayotekelezwa chini ya utaratibu wa “FORCE ACOUNT”.

Hata hivyo Muhagama alizitaja Halmashauri hizo 80 ambazo zilikutwa na miradi yenye kasoro kuwa ni pamojana na mbozi DC, Songwe DC, Ileje DC, Tunduma TC, Sumbawanga DC, Sumbawanga MC, Karagwe DC, Msimbo DC, Mpanda MC, Uvinza DC, Kigoma MC, Buhingwe DC, Kasulu DC, Kibondo DC, Ngala DC, Bukoba MC, Bialamulo DC, na Bukombe DC.

Zingine ni Geita DC, Geita TC, Nyamwale DC, Msalala DC, Kahama TC, Misungwi DC, Sengerema DC, Buchofya DC, Ilemela MC, Kwimba DC, Meatu DC, Itilima DC, Buliadi TC, Bunda DC, Musoma DC, Lorya DC, Talime TC, Talime DC, Longido DC, Mmemo DC, Babati DC, Kiteto DC, Rombo DC, Mwanga DC, Bumbuli DC, Kilindi DC, Handeni DC, Korongwe TC, Muheza DC, Pangani DC, Wilaya ya Kaskazini “A” Unguja , Wilaya ya kati Unguja, kusini “A” Mjini maghalibi.


Ubungo MC, Temeke MC, Kibiti DC, Rufiji DC, Mafya DC, Kibaha DC, Mvomelo DC, Malimi DC, Ifakala TC, Gailoba  DC, Mwapwa DC, Kondoa  TC,  Dodoma CC, Itingi DC, Mkalama DC, Ilamba DC,Igunga DC, Nzega DC, Tabora MC, Chunya MC, Busokelo MC, Kyela DC, Rungwe DC, Iringa DC, Mbaleli DC, Mufindi DC, Iringa MC, Wangig’ombe DC, Njombe DC, Malamba DC, Songea DC, na Nyasa DC

Akisoma risala  ya utii  kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mbele ya Rais Magufuli alisema kuwa mwenge huo wa uhuru mwaka 2019 umekimbizwa kwa umbali wa km 26, 273.94  katika mikoa 31, halmashauri za wilaya 195 kwa siku 195 na kutembelea, kukagua, kufungua na kuzindua miradi ya maendeleo 1,390

Kiongozi huyo wa mbio za  mwenge wa Uhuru  kitaifa Mkongea ally akiwasilisha risara ya utii alimueleza Rais, Magufuli kuwa  kazi ya kupambana na ubadhirifu katika baadhi ya miradi ya maendeleo kwao haikuwa rahisi kutokana na  vikwazo mbali mbali kama vile vitisho pamoja na kejeli zenye lengo la kuwakatisha tamaa zilifanywa na baadhi ya viongozi hao.

Hata hivyo Mkongea aliwaasa viongozi pamoja na wananchi kuendelea kudumisha ushirikiano waliokuwa wanauonyesha wakati mbio za mwenge zilipokuwa zimefika katika maeneo yao kwa kuwa pamoja na mambo mengine dhamira ya mwengi ni kudumisha upendo na mshikamano

Pamoja na mambo mengine Mkongea alimuomba Rais magufuli Kuongeza uwekezaji na ufuatiliaji wa karibu katika miradi ya maji na kuchukuwa hatua stahiki kwa  wale wote wanaobainika kuhujumu, sekta hiyo muhimu kwa ustawi wa  kitaifa.

No comments:

Post a Comment