Wednesday, October 9, 2019

HALMASHAURI ZATAKIWA KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU

Na Hadija Hassan, Lindi.

Halmashauri zimetakiwa kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu (walemavu) ambao wamepewa mikopo ya asilimia 2 inayotokana na asilimia 10 ya fedha za mapato ya Ndani katika Halmashauri zao kuwatafutia masoko ya uhakika ya bidhaa wanazozizalisha ili kuhakikisha fedha walizokopa wanarejesha kwa wakati.

Wito huo Umetolewa na kiongozi Wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Mzee Mkongea Ally  alipotembelea na kuona kazi mbali mbali za mikono zinazofanywa na vikundi vya wajasiriamali wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi ambavyo vimepewa mikopo ya asilimia 10 kutoka Halmashauri.

Ally, alisema changamoto kubwa wanayokabiliana nayo kundi, hilo ni kushindwa kutangaza bidhaa walizozizalisha ukilinganisha na makundi mengine kama ya vijana na Wanawake jambo ambalo huwafanya kushindwa kurejesha mikopo hiyo kwa wakati.

Alisema Serikali ilivyoamua kutoa mikopo hii ilikuwa na lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi pamoja na kuwawezesha kuondokana na umasikini hivyo ni wajibu wa Halmashauri kusaidia kundi hilo muhimu.

Awali afisa maendeleo ya jamii wa Halmashauri hiyo ya Lindi Grace Mwambe alisema kuwa Halmashauri hiyo ipo msitari wa mbele katika kuwawezesha Wananchi kiuchumi hasa kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Alisema katika kutekeleza maagizo ya Serikali juu ya kukopesha makundi hayo kwa asilimia 10 za fedha zinazopatikana katika mapato ya ndani.

Halmashauri hiyo imeweza kutoa kiasi cha shilingi milioni 27 kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 kwa vikundi 17.

Aidha akiongeza kuwa kati ya vikundi hivyo 17 vilivyopewa mikopo hiyo , vikundi 7 vya vijana, vikundi 8 vya wanawake na 1 cha watu wenye ulemavu

No comments:

Post a Comment