RC. PWANI ATOA SIKU 30 WAFUGAJI WALIOHAMIA MKOANI HUMO KUONDOKA.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo, akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Kitonga, kata ya Vigwaza, Halmashauriya Chalinze wilayani Bagamoyo. Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Everist Ndikilo, akizungumza na wananchi katika mkutano huo, waliokaa chini, wa kwanza kulia ni Diwani wa kata ya Vigwaza, Muhsini Baruani, na wa pili ni Mbu nge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete . ................................. Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Everist Ndikilo, ametoa siku 30 kwa wafugaji waliohamia mkoani humo kuondoka baada ya kushamiri kwa migogoro ya wafugaji na wakulima. Kauli hiyo aliitoa katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika kijiji cha Kitonga kata ya Vigwaza katika Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo. Alisema Serikali haiwezi kufum bia macho ikiona ...