Wednesday, July 31, 2019

MWENGE WA UHURU 2019, WAKAGUA MIRADI 13 HALMASHAURI YA BAGAMOYO

Image may contain: 4 people, people smiling, people standing, tree, child and outdoor
Mwenge wa uhuru 2019, umehitimisha mbio zake katika Halmashauri ya Bagamoyo, kwa kutembelea miradi 13 na kuzindua miradi 2 ambayo ina thamani ya shilingi Bilioni 4.7
Image may contain: 13 people, including Subira Mgalu, people standing and outdoor
Image may contain: 5 people, people smiling, people standing and outdoor

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya (KUU), Bi Zainabu Mfaume Kawawa, akiongoza wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, (KUU) wabunge wa  Bagamoyo, Chalinze na viti maalum, wakurugenzi wa halmashauri, watumishi wa serikali, viongozi wa CCM pamoja na wananchi kwa ujumla wakati wa kuaga Mwenge wa Uhuru 2019 mara baada ya kumaliza mbio zake halmashauri ya Bagamoyo.
Image may contain: one or more people, crowd, sky and outdoor 
Makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru 2019 kati ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawa na Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama.

WAZIRI MKUU ATAKA MKANDARASI KUTUMIA VIBARUA WA NDANI YA HALMASHAURI

Na Hadija Hassan, Lindi.

Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amemuagiza Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi, M/S National Service Construction Department (SUMA JKT ) kutotumia vibarua wanaotoka nje ya Wilaya hiyo na Badala yake wawatumie Vijana waliopo katika Halmashauri hiyo.


Majaliwa aliitaka agizo hilo kwa Meja Atupele Mwamfupe Jana baada ya kutembelea na kukagua eneo linalojengwa Ofisi hiyo ambapo alisema kuwa katika eneo hilo wapo Vijana wa kutosha wa watakaoweza Kufanya Kazi kwa uweledi katika ujenzi huo.


Hata hivyo Majaliwa alisema ili kuifanya Kazi hiyo iende kwa kasi na kukamilika katika muda uliopangwa Ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za kuwatoa vibarua nje ya Maeneo hayo ni vyema kutumia vibalua waliopo ndani ya Wilaya hiyo.


Awali akisoma taarifa ya Mradi huo Mbele ya Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ya Ruangwa, Andrew Chezue alisema kuwa Mradi huo utagharimu Tsh. Bilioni 3,777,831,596.00 na unasimamiwa na Mtaalamu Mshauri M/S Bureau for Industrial Cooperation (BICO) kwa Mkataba wa Tsh. Milioni 16,205,000.00


Chezue alisema mradi huo umeanza rasmi mwezi Juni Mwaka huu wa 2019, na unatarajiwa kukamilika mwezi juni Mwaka 2020 ambapo lengo lake kubwa ni kuboresha mazingira ya kufanyia Kazi ikiwa pamoja na kuwa na jengo bora na imara ambalo litatumika katika Shughuli Mbali mbali za Kiserikali.


Hata hivyo Chezue alibainisha kuwa Mpaka sasa jumla ya Tsh. Milioni 500,000,000.00 zimeshatolewa na Serikali kuu kwa Mwaka wa fedha wa 2018/2019 ambazo zimetumika kwa kumlipa Mkandarasi kwa ajili ya malipo ya awali (Advance payment), ili aweze Kufanya stadi ya udongo pamoja na kusafisha eneo la mradi.


Nae Meneja wa Kanda ya ujenzi wa Suma Jkt Kanda ya kusini, anaetekeleza mradi huo wa ujenzi wa Ofisi Mpya ya Halmashauri, Meja Atupele Mwamfupe alisema kuwa jengo hilo Litakuwa la ghorofa Moja ambalo  litahusisha vyumba 33 Chini na vyumba 29 Juu pamoja na kumbi mbili za mikutano.


Alisema mpaka sasa Kazi zilizokamilika ni pamoja na usafishaji wa eneo kwa ajili ya ujenzi, upimaji wa sampuli ya udongo, uchimbaji wa kisima cha maji, ukusanyaji wa Vifaa vya ujenzi eneo la Mradi, ujenzi wa uzio kuzunguka eneo la Mradi pamoja na ufyatuaji wa matofali ambao unaendelea ambapo hadi sasa tofali 10,000 zimeshafyatuliwa.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Rashidi Nakumbya aliishukuru Serikali ya awamu ya tano kwa kuipatia Halmashauri hiyo fedha za ujenzi wa Ofisi Mpya na ya kisasa Itakayokuwa na mchango Mkubwa katika kuongeza ufanisi wa Kazi kwa watumishi wa Halmashauri hiyo.


NaKumbya aliongeza kuwa Kutokuwa na Ofisi kubwa katika Halmashauri hiyo hivi sasa kunasababisha mtawanyiko wa baadhi ya Idara kunakotokana na ukosefu wa majengo hali ambayo wananchi hupata shida wanapokwenda kupata huduma.


Hata hivyo alieleza changamoto nyingine kuwa ni kuwepo kwa Msongamano wa watumishi kutumia Chumba kimoja baina ya Wakuu wa Idara na vitengo katika Idara jambo ambalo linapelekea kupunguza ufanisi wa kazi.

Utayarishaji wa eneo la ujenzi ukiwa unaendelea.
 
 Muonekano wa Jengo la Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi litakapokamilika.

PICHA ZOTE NA HADIJA HASSAN. 

WANACHAMA WA YANGA BAGAMOYO WAFANYA USAFI WA MAZINGIRA.

Na Selestian James.

Wanachama wa klabu ya yanga wilayani Bagamoyo wameadhimisha wiki ya wananchi kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali ya mji wa Bagamoyo.

Shughuli hiyo ya usafi imewajumuisha watu wa kada mbalimbali ambao ni wanachama wa yanga wakiongozwa na Diwani wa kata ya Nianjema  iliyopo katika halmashauri ya wilaya Bagamoyo, Abdul Mzee Pyallah ambaye pia ni katibu wa hamasa ya kuchangia Yanga Bagamoyo.

Miongoni mwa sehemu walizofika kufanya usafi ni pamoja na Hospitali ya wilaya ya Bagamoyo.

Shughuli hiyo yenye kauli mbiu "funga kazi kusanya kijiji" ni miongoni mwa hatua muhimu za maadhimisho ya  wiki ya wananchi ambayo ilizinduliwa  visiwani Zanzibar na itafikia kilele mwanzoni mwa mwezi ujao katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

Sambamba na hilo Diwani Pyallah pia amezungumzia uwepo wao tena hospitalini hapo siku ya tarehe tatu  ni kwa ajili ya kutembelea wodi ya watoto na kutoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa.

Aidha, alisema watatembelea kituo cha  watoto waishio katika mazingira magumu kilichopo katika kata ya Nianjema, na ziara hiyo itamalizikia katika gereza la Kigongoni kwa ajili ya kuwaona wafungwa gerezani humo.

Miongoni mwa shughuli walizoweza kufanya ni pamoja na kuchangia damu kwa wagonjwa pamoja na kushiriki na wananchi katika shughuli za kijamii ikiwa vitendo vinavyoakisi makusudio ya wiki ya wananchi.


Kwa upande wao madaktari waliokuwepo katika tukio hilo wameeleza kufurahishwa na hatua hiyo na kuwapongeza huku wakiwaomba kuendeleza utamaduni huo.

Aidha, waliowaomba pia kusaidia kifaa maalum cha kupimia upumuaji wa watoto kwani ni moja ya vifaa vinavyohitajika sana katika utendaji kazi wa hospitalini hapo.
 Wanachama wa Yanga Bagamoyo wakishiriki katika usafi wa mazingira katika hospitali ya wilaya Bagamoyo, ikiwa ni katika kuadhimisha wiki ya wananchi.
Diwani wa kata ya Nianjema  iliyopo katika halmashauri ya wilaya Bagamoyo, Abdul Mzee, akishiriki usafi wa mazingira pamoja na wananchama wengine wa Yanga ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya wananchi.

PICHA ZOTE NA SELESTIAN JAMES.