Sunday, October 31, 2021

JK. AFUNGA RASMI TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO.

 No description available.

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewapongeza waandaaji wa Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni  kwa kuweka utaratibu wa kuwatembeza wageni kwenye vivutio mbalimbali ikiwemo historia ya mji wa Bagamoyo.

 

Dkt. Jakaya alitoa pongezi hizo wakati wa kufunga Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni Tarehe 30 Oktoba 2021, katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambapo alisema historia ya Bagamoyo ni kubwa sana na wananchi wa ndani na nje ya Bagamoyo, na  wageni kutoka nje ya nchi wanapaswa kuijua historia hiyo.

 

Alisema kutokana na umuhimu wa historia ya Bagamoyo, imempelekea Rais Samia Suluhu Hassan kufika Bagamoyo wakati wa maandalizi ya filamu ya Royal tour na kwamba hiyo ni heshima kubwa kwa Bagamoyo ambapo wizara husika inapaswa kuendelea kuielezea historia ya Bagamoyo kwa wageni.

 

Aliongeza kwa kusema kuwa, ili wageni waweze kuvutiwa kusikiliza na kuelewa historia hiyo, ni vyema wakapatikana watembeza watalii wenye uwezo wa kuelezea historia halisi ya Bagamoyo yenye kueleweka kwakuwa maelezo mazuri yanamvutia msikilizaji na kupata hamu kutaka kujua zaidi.

 

Aidha, alipongeza maandalizi yaliyofanyika katika Tamasha hilo la 40 kwa namna lilivyofana kwa kuwakusanya wasanii mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ambapo kila mmoja alionyesha uwezo wake jukwaani huku wahudhuriaji wakiwa na furaha kutokana na burudani zilizokuwa zikitolewa.

 

Alisema katika nchi yetu swala la utamaduni ni muhimu sana kwakuwa linawarudisha watanzania kwenye burudani zao za asili na kwamba siku zote anaekataa asili yake ni mtumwa.

 

Aliendelea kusema kuwa, kutokana na umuhimu huo ndiomana seikali ya Tanzania kuanzia awamu ya kwanza hadi sasa wizara ya utamaduni ilikuwepo na bado ipo ili watanzania waone umuhimu wa kutunza utamaduni wao.

 

Alisema utamaduni ni kielelezo cha utashi na uhai wa Tanzania hivyo kila panapofanyika Tamasha watanzania wanaendelea kukumbushana na kusisitiza umuhimu wa utamaduni katika jamii yetu na Taifa kwa ujumla.

 

Alisema Rais Samia ameendelea kutambua na kusisitiza umuhimu wa utamaduni kwakuwa utamaduni unabeba ujumbe halisi wa jamii husika kwa kipindi hicho.

No description available.

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, (katikati) Naibu waziri wa Utamaduni , Sanaa na Michezo, Pauline Philipo Gekul, (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge (kulia) wakiangalia vikundi vya sanaa wakati wa kufunga Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni lilifanyika katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Tarehe 30 Oktoba 2021.

No description available.

MATOKEO DARASA LA SABA 2021 HAYA HAPA

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

PSLE-2021 EXAMINATION RESULTS



ARUSHA

DAR ES SALAAM

DODOMA

IRINGA

KAGERA

KIGOMA

KILIMANJARO

LINDI

MARA

MBEYA

MOROGORO

MTWARA

MWANZA

PWANI

RUKWA

RUVUMA

SHINYANGA

SINGIDA

TABORA

TANGA

MANYARA

GEITA

KATAVI

NJOMBE

SIMIYU

SONGWE


Friday, October 29, 2021

TaSUBa KUWA CHUO CHA KIMATAIFA CHA SANAA NA UTAMADUNI.

No description available.

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa akifungua Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Tamaduni Bagamoyo lililofanyika Usiku wa kuamkia  Oktoba 28 hadi 30, 2021 katika viwanja vya Chuo cha Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo(TASUBA) mjini Bagamoyo.

.........................................

 

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amesema wizara yake imekusudia kukibadilisha chuo cha TaSUBa kilichopo Bagamoyo kuwa ni chuo cha Sanaa na Utamaduni cha kimataifa, ili kwenda sambamba na dhamira ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kukuza na kuendeleza Sanaa na Utamaduni hapa nchini.

 

Waziri Bashungwa ameyasema hayo mjini Bagamoyo katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBa) wakati wa kuzindua rasmi Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni ambalo limeanza Tarehe 28 Oktoba 2021 litakalodumu kwa muda wa siku tatu hadi 30 Oktoba 2021.

 

Alisema kutakuwa na maboresho makubwa yatakayofanyika katika chuo cha TaSUBa ili kukidhi viwango na vigezo vya kimataifa katika maswala Sanaa na Utamaduni.

 

Aidha, alisema kuwa, maboresho hayo pia yatahusisha taasisi zinazowasaidia wasanii hapa nchini kama vile Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) na Chama cha hakimiliki Tanzania (COSOTA) ambapo utendaji kazi wa taasisi hizo unapaswa kuwa wa kiwango cha juu ili wasanii waweze kunufaika kupitia kazi zao.

 

Aliongeza kuwa, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo itaendelea kushirikiana na wasanii hapa nchini ili kuhakikisha wasanii wanaboreshewa mazingira yao ya kazi pamoja na kulinda haki zao za msingi katika kazi zao.

 

Alifafanua kuwa, ushirikiano baina wizara na wasanii utasaidia kulinda ajira za wasanii na kazi zao ili waweze kufanya vizuri zaidi na hatimae wao iwe ni chachu ya kuenea ajira kwa vijana wengi walioingia kwenye tasnia ya sanaa.

 

Akizungumzia Tamasha hilo la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni Bagamoyo, Bashungwa alisema ni Tamasha kubwa na la aina yake kuwahi kutokea na kwamba wizara itaendelea kuboresha mazingira ya maandalizi ili kila mwaka Tamasha liongezeke ubora katika macho ya kitaifa.

 

Alitumia nafasi hiyo kuwapongeza viongozi mbalimbali ambao wamfanikisha maandalizi ya Tamasha hilo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakari Kunenge, Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainab Abdallaah, Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbas pamoja Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUB) Dkt. Harbert Makoye.

 

Aidha, alisema kuwa kukamilika kwa Tamasha hilo la 40 ndio mwanzo wa maandalizi ya Tamasha ka 41 na kwamba amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abasi kuanza maandalizi ya Tamasha 41 hapo mwakani.

 

Aliwapongeza pia viongozi wa nchi mbalimbali waliohudhuria Tamasha hilo na kusema kuwa hiyo ndio maana ya kuita Tamasha la kimataifa kwa kukusanya kwake wageni kutoka nchi mbalimbali wakiwemo viongozi na vikundi vya sanaa kutoka katika nchi hizo.

 

Tamasha la 40 la kimataifa la Sanaa na Utamaduni limezinduliwa rasmi Tarehe 28 Oktoba 2021 na linatarajiwa kufungwa tarehe 30 Oktoba 2021 katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni (TaSUBa) ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni Sanaa ni Ajira.