JK. AFUNGA RASMI TAMASHA LA SANAA BAGAMOYO.
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewapongeza waandaaji wa Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni kwa kuweka utaratibu wa kuwatembeza wageni kwenye vivutio mbalimbali ikiwemo historia ya mji wa Bagamoyo. Dkt. Jakaya alitoa pongezi hizo wakati wa kufunga Tamasha la 40 la kimataifa la sanaa na utamaduni Tarehe 30 Oktoba 2021, katika viwanja vya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambapo alisema historia ya Bagamoyo ni kubwa sana na wananchi wa ndani na nje ya Bagamoyo, na wageni kutoka nje ya nchi wanapaswa kuijua historia hiyo. Alisema kutokana na umuhimu wa historia ya Bagamoyo, imempelekea Rais Samia Suluhu Hassan kufika Bagamoyo wakati wa maandalizi ya filamu ya Royal tour na kwamba hiyo ni heshima kubwa kwa Bagamoyo ambapo wizara husika inapaswa kuendelea kuielezea historia ya Bagamoyo kwa wageni. Aliongeza kwa kusema kuwa, ili wageni waweze kuvutiwa kusikiliza na kuelewa historia hiyo, ni...