Saturday, April 27, 2024

ULEGA ZIARANI KUKAGUA MIUNDOMBINU ILIYOATHIRIWA NA MAFURIKO MKURANGA

 

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega  leo Aprili 27, 2024 ametembelea maeneo yalioathiriwa na mafuriko ya maji ya mvua katika jimbo la Mkuranga, mkoani Pwani na kufanya tathimini ni kiasi gani maeneo hayo yameathirika na kuona hatua za kuchukua ili kutatua changamoto hizo.


Katika ziara yake hiyo Mhe. Ulega ameanza kukagua maeneo yaliyoathirika na mafuriko hayo ikiwemo barabara na madaraja katika kata ya Mwandege, Tambani, Vikindu, Mkuranga, Kiparang’anda, Mkamba, Kimanzichana, Nyamato na Lukanga.


Aidha, ametoa rai kwa wananchi wanaokaa katika maeneo hayo yalioathiriwa na mafuriko kuwa na subira wakati serikali ikiendelea kushughulikia changamoto hizo.













MAGAZETI YA LEO TAREHE 27 APRIL 2024.

 























Friday, April 26, 2024

TRA KAGERA YAVUKA LENGO LA UKUSANYAJI KODI.

 

Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Kagera Castro John

Afisa elimu kwa umma TRA Kagera Ruekaza Rwegoshola akitoa elimu ya kodi kwa waandishi wa habari

..............................

Na Alodia Babara,

Bukoba.


Mamlaka ya mapato nchini TRA mkoa wa Kagera imevuka lengo la ukusanyaji wa mapato katika kipindi cha Januari hadi Machi 2024 na kufikia asilimia 107.


Meneja wa mamlaka hayo mkoa wa Kagera Castro John akizumgumza na waandishi wa habari  Aprili 25, 2024 katika kikao kilicholenga kuhamasisha ulipaji kodi wa hiari pamoja na kueleza mafanikio ya ukusanyaji wa kodi kipindi cha Januari hadi Machi, 2024.


"Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Kagera tulipanga kukusanya shilingi bilioni 28.24 lakini tulikusanya shilingi bilioni 30.2 na hivyo kuvuka lengo na kufikia  asilimia 107" amesema John.


John ametolea ufafanuzi wa kodi mpya ya bodaboda ambayo inapaswa kulipwa kwa mwaka elfu 65,000 ambapo kila robo mwaka zinapaswa kilipwa shilingi 16,200 na zinalipwa kwa awamu nne hivyo akawaomba wamiliki wa pikipiki za biashara kulipa kodi hiyo.


Aidha katika mkutano huo amewaomba waandishi wa habari kuendelea kuhamasisha walipakodi kulipa kwa wakati ili kuongeza mapato ya nchi.


Afisa elimu kwa umma  Ruekaza Rwegoshola ameeleza kuwa, kupitia ulipaji kodi serikali imekuwa ikitoa huduma mbalimbali kwa wananchi wake zikiwemo huduma za Afya, maji, ujenzi wa miundombinu ya barabara na vyumba vya madarasa.


Amesema, asilimia 70 ya mapato ya serikali yanatokana na ukusanyaji kodi na kwa mwaka 2023/2024 serikali ilipitisha bajeti ya trioni 44.39 na TRA ilipewa lengo la kukusanya trioni 26.75 hivyo TRA inayo kazi kubwa kuhakikisha  inakusanya kodi.


TaSUBa YAANDAA KONGAMANO LA MUUNGANO.

 

Makamo wa Rais wa Serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Mwikwabe Msafiri (katikati) akizungumza na washiriki katika kongamano hilo, kulia ni Katibu wa Makamo wa Rais, Cinthia Vincent Lwanda na kushoto ni Waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi, Raban Erasto Mbiti.

.....................................

Na Athumani Shomari 

Bagamoyo.


Katika Maadhimisho ya sherehe za miaka 60 ya Muungano, Serikali ya wanafunzi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) imeandaa kongamano la Muungano ambalo limewashirikisha wanafunzi wa chuo hicho na wageni kutoka nje ya chuo.


Katika kongamano hilo lililofanyika tarehe 25 April 2024, mada za muungano ziliwasilishwa na kisha kutoa nafasi kwa washiriki kutoa maoni mbalimbali kuhusu Muungano.


Washiriki hao walisema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao leo unaadhimishwa kwa kutimiza miaka 60 una faida nyingi kwa watanzania wote.


Wamezitaja baadhi ya faida hizo ni pamoja ushirikiano wa wananchi wa bara na visiwani katika mambo mbalimbali.


Wamezungumzia changamoto kadhaa ambazo zinazoukabili muungano ambazo miongoni mwa hizo ni zile zinazohitaji kufanyiwa kazi na Serikali na nyingine ni zinazohitaji uzalendo wa wananchi wa kuyatambua mazuri ya muungano na kutoa maoni kurekebisha kasoro kwa kuzingatia ushirikiano, umoja na dhamira yenyewe ya muungano.


Wamesema wapo watu wanazungumzia kasoro za muungano tu bila ya kutaja faida zilizopo hali ya kuwa faida zake nyingi na kwamba kasoro zinatakiwa kutajwa kwa lengo la kurekebisha na sio kuubeza muungano wenyewe.


Aidha wamesema licha ya faida zilizopo yapo mambo kadhaa ambayo yanahitaji kufanyiwa mapitio kurekebisha kasoro zilizopo ili kila mwananchi afurahie matunda ya muungano.


Wamesema miongoni mwa maeneo yanayohitaji marekebisho ni pamoja na maswala ya kodi kwa pande zote mbili ili kuleta uwiano utakaoleta furaha kwa wananchi wote.


Makamo wa Rais wa Serikali ya wanafunzi chuoni hapo, Mwikwabe Msafiri amesema lengo la kongamano hilo ni kuleta uelewa wa pamoja kwa wanachuo ambao wanaonekana umri wao ni mdogo ukilinganisha na umri wa muungano.


(Nikiangalia naona wote tuliopo hapa umri wetu ni mdogo na umri wa muungano ni mkubwa hivyo ipo haja ya kujadili maswala ya muungano ili tuweke kumbukumbu zetu sawa, Alisema Mwikwabe.


Maadhimisho ya sherehe za muungano huadhimishwa kila mwaka ambapo waka huu muungano wa Tanganyika na Zanziba umetimiza miaka 60.




Washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia mada zilizowasilishwa na watoa mada.


MAGAZETI YA LEO TAREHE 26 APRIL 2024.