Wednesday, June 10, 2020

Waziri wa nishati ataka wawekezaji kuzalisha vifaa vya kusafirisha gesi hapa nchini





Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani ametoa wito kwa wadau wa viwanda kutengeneza Vifaa vya kusafirisha nishati ya mafuta na gesi hapa nchini dhamira ikiwa ni kuharakisha mchako wa kuanza miradi ya usambazaji lakini pia kupunguza gharama za uzalshaji.

Alisema uhitaji wa mabomba kwa miradi inayoendelea bado ni mkubwa na kwamba hadi sasa mahitaji ya mabomba ya gesi ni kilometa  zisizopungua 2,250 na mita za luku ni 8,000 hadi 10,000 kwa mwaka .

Aidha akizungumzia kasi ya usambazaji wa mabomba ya gesi majumbani, Kalemani alisema kuna mafanikio makubwa yamepatikana ikiwamo usambazaji huo kuongezeka kutoka Kaya 70 hadi kufikia Kaya 1000 kwa Miaka mitatu.

Aliongeza kusema kuwa kuagiza vifaa nje ya nchi kunapoteza mapato ya nchi, agizo alilolitoa linalenga kulinda mapato, uzalishaji wa mabomba koki ,vyuma, nyaya utasaidia  kujenga uchumi wa nchi kupitia sekta ya viwanda ,"Dkt.Kalemani .

Faida ya kuzalisha mabomba nchini itasaidia kuongezeka kwa kasi ya kusambaza gesi na hivyo kuwapa nishati wananchi kwa wakati.

Naye Naibu Waziri wa  Wizara hiyo Stephen Byabato   amesema serikali inaendelea kutekeleza ilani ya kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuendelea kuwaunganisha nishati ya umeme mjini na vijijini.

Alisema Rais Dkt.Magufuli anaamini vijana wana uwezo kiutendaji ndio maana amemteua kumsaidia kutekeleza majukumu ya Wizara hiyo chini ya Waziri Dkt.Kalemani.

Awali akizungumza kwenye Mkutano huo, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Maendeleo la Petroli TPDC Dkt. James Mataragio amesema wanaendelea na ujenzi wa vituo vitano vya kujaza gesi asilia kwenye magari katika mkoa wa dar es salaam huku kukiwa na mpango wa kupeleka nishati hiyo jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel Ateta Na Madereva Wa Malori, Namanga

 
Arusha.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amefanya ziara katika mpaka wa Tanzania na Kenya Namanga Jijini Arusha na kuzungumza na madereva wa malori yanayokwenda Kenya ili kusikiliza changamoto zinazowakumba.

Dkt. Mollel amefanya ziara hiyo leo, ikiwa ni sehemu ya kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazowakumba madereva hao, katika kipindi hiki ambacho Dunia imekumbwa na maambukizi ya homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona.

Dkt. Mollel amesema kuwa, Serikali imeliona tatizo hilo na kuweka wazi kuwa itaongeza kasi katika kuhakikisha inapata suluhu ya changamoto wanazokumbana nazo madereva hao katika eneo la mpaka wa Namanga.

“Nimekuja kuwaambia poleni, lakini Serikali yetu itaenda kwa kasi ya ajabu kuhakikisha kwamba hili tatizo lenu katika mpaka huu linatatuliwa ” alisema.

Aidha, Dkt. Mollel amewataka madereva hao kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho, Serikali inatafuta utatuzi wa changamoto yao, huku akiwapa salamu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli na kusema anawapenda sana.

Mbali na hayo Dkt. Mollel alisema kuwa changamoto hii iliyojitokeza katika mpaka wa Namanga ni suala mtambuka ambalo linahusisha Wizara zaidi ya moja, huku akiweka wazi kuwa suala hili lina uhusiano wa kibiashara na uchumi baina ya nchi hizo.

Nae, dereva wa malori yanayokwenda nchini Kenya Bw. Abdullah Hassan amesema kuwa, kama madereva hawakubaliani na majibu ya vipimo wanavyopewa kutoka Kenya kutokana na vipimo hivyo kuonesha idadi kubwa ya madereva kuwa na ugonjwa wa Corona jambo ambalo sio kweli.

“Tunaishi maisha magumu sana kutokana na hali iliyojitokeza, na kunachosikitisha zaidi, sisi hatukubaliani na vipimo ambavyo tunapimwa upande wa pili.

Kwa upande wake, Japhet Jeremiah alisema kuwa, wamekuwa wakiombwa kiasi cha shilingi 2000 za Kenya ili kuandikiwa kuwa hawana Corona, hali aliyeweka wazi kuwa ni uonevu kwa madereva kutoka Tanzania.

“Sisi kero yetu, tumekuwa tukipima Kenya tumeambiwa tuna Corona, na mimi wiki mbili nilipima nikapewa cheti nina Corona lakini ukweli ni kwamba sina Corona na sijawai tumia dawa yoyote mpaka sasahivi” alisema

MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI LA AFRIKA MASHARIKI KUANZA KARIBUNI




Na Iisac Thadeo

 Kampuni inayosimamia mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki  (EACOP)imefanya kikao na waziri wa Nishati nchini Tanzania Dr.Medard Kalemani kwa lengo la kuitaarifu Serikali maendeleo ya mradi katika eneo la Ziwa Albert nchini Uganda pamoja na maendeleo ya mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki  (EACOP)

Vilevile kampuni ya Total na wizara ya Nishati wamezungumzia mipango ya kuendelea na mazungumzo ya makubaliano ya Serikali husika (wenyeji)wa makubaliano ya wabia /wanahisa,pamoja na makubaliano ya maswala ya Usafirishaji ili kuleta uiano wa makubaliano yote kwa ajili ya kuendelea na maamuzi ya mwisho ya uwekezaji

Kwa upande wake waziri WA Nishati wa Tanzania na kwa niaba ya Serikali ya Tanzania amesema leo ni siku nzuri kwa wenzetu wa Total wametuarifu wamekamilisha majadiliano Kati Yao na Sino kutoka Uingereza na Total wamechukua his a asilimia 67 na nyingine zilizobaki za SINO kwa maana hiyo atakuwa ni mwekezaji mkubwa.

Aidha waziri Kalemani alisema amewaomba Total na kuwataka yote wanayosema wayafanye kwa haraka

Mkutano huo ulifanyika zilipo Ofisi ndogo za wizara ya Nishati jijini Dar es salaam na kuudhuliwa na wadau mbalimbali wa Sekta hiyo kuwepo Katibu mkuu wa wizara hiyo mheshimiwa Zena