Saturday, October 19, 2019

TAKUKURU YAKAMATA 99 VIONGOZI WA AMCOS LINDI.

NA HADIJA HASSAN, LINDI

TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa (YAKUKURU) Mkoa wa Lindi ImeendeLea kuwakamata viongozi wa vyama vya Msingi (AMCOS) 99 kutoka 51, Wa awali ambao wamehusika katika kudhulumu fedha za Wakulima wa Ufuta wa Mkoa huo.

Ukamatwaji wa viongozi hao ni moja ya utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli alilolitoa oktoba 10 mwaka huu wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi, ambapo aliiagiza TAKUKURU pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kuhakikisha vyama 10 vya Msingi (AMCOS) vinavyodaiwa na wakulima wa ufuta vinawalipa wakulima hao fedha zao kabla ya msimu mpya wa Korosho kuanza.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) Brigedia General John Mbungo alisema kuwa ongezeko la viongozi hao wa Vyama vya msingi limekuja baada ya taasisi yao kuendelea kufanya msako katika baadhi ya vyama vya Msingi (AMCOS) Mkoani humo

"ingawa Taarifa iliyokabidhiwa TAKUKURU na Naibu Waziri wa kilimo Mhe, Hussein Bashe ilikuwa inaonyesha wakulima wa ufuta wamedhulumiwa kiasi cha shilingi milioni 436,869, 982,00 na vyama 10 vya msingi (AMCOS) lakini uchunguzi na ufuatiliaji uliofanywa na TAKUKURU ulibaini kuwepo kwa vyama 31 vya Msingi (AMCOS) Kuwadhulumu wakulima wa ufuta kiasi cha shilingi Bilioni 1,236,363,075.00/=" alisema Mbungo.

Hata hivyo Mbungo alisema kuwa tokea zoezi hilo la kuwakamata viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) oktoba 16, mpaka oktoba 19 tayari kiasi cha shilingi milioni 255,598,194.00 zimerejeshwa katika Ofisi ya TAKUKURU na kwamba fedha hizo zitaanza kulipwa kwa wakulima hao kwa utaratibu utakaopangwa.


Mbungo pia alisema katika kuhakikisha wakulima wote waliodhulumiwa fedha zao wanapata haki zao Taasisi hiyo imeanza zoezi la kutambua, kupiga picha na kukamata Mali za viongozi hao wa AMCOS wanaodaiwa ili ziwe dhamana ya madeni wanayodaiwa na endapo watashindwa kulipa kwa muda waliokubaliana vitu hivyo vitauzwa ili kulipa madeni ya wakulima.


Aidha, alitoa rai kwa viongozi wote wa vyama vya ushirika Nchini vinavyodaiwa na wakulima walipe wakulima hao haraka iwezekanavyo kabla ya TAKUKURU haijawafikia kwani zoezi hilo litakuwa endelevu na kwamba hakutakuwa na chama chochote cha ushirika kinacho daiwa kitakachobaki salama

No comments:

Post a Comment