Friday, October 11, 2019

MKONGEA AZINDUA UJENZI WA RADIO NACHINGWEA, AWAASA WANAHABARI.

 
Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa Mzee Mkongea Ally,(katikati) akizungumza na wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha Radio cha Mashujaa fm. wilayani Nachingwea jana Oktoba 10, 2019, kulia ni Mkuu wa wilaya ya hiyo, Rukia Muango, na kushoto ni Meneja wa Mashujaa fm, Zakia Gaspa.
 
Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa Mzee Mkongea Ally, akifungua kitambaa kwenye jiwe la msingi ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi ujenzi wa kituo cha Radio cha Mashujaa fm. wilayani Nachingwea jana Oktoba 10, 2019, anaeonekana kwa mbele akiwa na furaha ni Meneja wa Mashujaa fm, Zakia Gaspa.
PICHA ZOTE NA HADIJA HASSAN. 
..........................................

Na Hadija Hassan, Lindi.


Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru kitaifa Mzee Mkongea Ally, amewataka wanahabari Nchini kuandika habari kwa Kuzingatia weledi pamoja na maadali ya habari.


Mkongea ametoa wito huo jana Oktoba 10, 2019 wakati wa kuzindua mradi wa ujenzi wa kituo cha Radio ya Mashujaa Fm, wilayani Nachingwea Mkoani Lindi uliofanywa na mbio hizo za mwenge.


Alisema vyombo vya Habari na wanahabari kwa jumla wamekuwa na nafasi kubwa katika jamii kwa masuala ya kuelimisha, kuburudisha na hata kuhabarisha hivyo ni vyema kwa wanahabari kuhakikisha habari wanazozitoa ziwa ni zenye uhakika na zisizokuwa na uchochezi.


"Hii ni kwa sababu ulimi wa mwanahabari ukikosea kidogo urekebishaji wake unakuwa na kazi kubwa, hivyo hakikisheni mnafanya kazi kwa uangalifu ili kile ambacho kinafanyika ndicho kinachomfikia mwananchi au mwanajamii" alisisitiza Mkongea.


Awali Meneja wa mashujaa FM, Zakia Gaspa akitoa taarifa ya ujenzi wa mradi wa kituo hicho cha Radio alisema kuwa kituo hicho hadi kukamilika kwake kimeghalimu kiasi cha shilingi milioni 15 Gaspa alisema katika kuhakikisha inasaidiana na Serikali katika mambo mbalimbali ya maendeleo radio yao imekuwa Ikijikita katika shughuli mbali mbali za kijamii ili kuhakikisha wananchi wanashiriki katika shughuli za kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment