Thursday, February 28, 2019

WANAOINGIZA MABINTI WA SHULE GESTI SASA KUKIONA...TGNP YAOMBA MSAADA KWA...

Waziri Kamwelwe asifu utendaji kazi wa Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania




Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi. Isack Kamwele amepongeza utendaji kazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Mhe. Kamwele alitoa pongezi hizo wakati alipotembelea Ofisi za TMA, Ubungo Plaza, Dar es Salaam, tarehe 27 Februari 2019 na alipata taarifa ya utendaji kazi wa mamlaka na kutembelea baadhi ya sehemu za kazi kabla ya kuzungumza na wafanyakazi. Mhe. Kamwele alipokelewa na uongozi na menejiment ya TMA, ikiongonzwa na mwenyekiti wa bodi ya ushauri Dkt. Buruhani Nyenzi na kaimu mkurugenzi mkuu Dkt. Ladislaus Chang’a. Kat

“Nawapongeza TMA kwa umakini na utekelezaji wa majukumu yenu, nakiri kusema ni moja ya taasisi makini kati ya taasisi zilizo chini ya wizara yangu nilizo tembelea”. Alizungumza mhe. Kamwele

Aidha, mhe. Kamwele alisisitiza kuboresha mfumo wa ushirikishwaji wa wadau na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa, akitolea mfano mafuriko yaliyo bomoa barabara eneo la Dumila, kuwa baada ya kufuatilia taarifa za hali ya hewa waligundua TMA ilitoa taarifa hizo siku mbili kabla ya tukio na kuonesha rangi nyekundu yenye kumaanisha tahadhari kwa maeneo ya Kilindi lakini taarifa hiyo haikuwafikia walengwa.

Mhe. Kamwele alimalizia kwa kuahidi kutatua changamoto zinazoikabili TMA zikiwemo uhitaji wa ongezeko la vituo vya hali ya hewa, mitambo ya hali ya hewa, kupatikana kwa jengo la kituo kikuu cha utabiri n.k

Akitoa salamu za shukrani kwa upande wa TMA, mkurugenzi wa ofisi ya TMA Zanzibar, Bw. Mohamed Ngwali alimshukuru mhe. Waziri kwa pongezi sambamba na kutembelea na kuona shughuli zinazofanywa na TMA, na kuahidi kufanyia kazi maelekezo yote aliyoyatoa .

Imetolewa:

Ofisi ya Uhusiano

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)

DC BAGAMOYO ATAKA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA WOTE KURIPOTI SHULE IFIKAPO JUMATATU MACH 04.

Image may contain: one or more people, people standing and outdoor
 Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawa,  akishiriki ujenzi wa vymba vya madarasa shule ya sekondari Pera Halmashauri ya Chalinze, aliyesimama kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Saidi Zikatimu.
............................

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawaamewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanawapeleka shule watoto wote waliofaulu kuingia kidato cha kwanza ifikapo jumatatu ya tarehe 04 Mach 2019.


Mkuu huyo wa wilaya ametoa tamko hilo wakati akizungumza na viongozi wa kata na tarafa katika Halmashauri ya Chalinze na kuwataka viongozi hao wasimamie maagizo hayo.


Tamko hilo limekuja baada ya shughuli za ujenzi wa vyumba vya madarasa zikiendelea wilaya yote ya Bagamoyo lengo likiwa ni kuhakikisha hakuna mwanafunzi atakaekosa masomo kwasababu ya upungufu wa vyumba vya madarasa.


Katika ziara yake hiyo ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa, Mkuu huyo wa wilaya ameshiriki shughuli za ujenzi katika shule ya Sekondari Pera kata ya Pera Halmashauri ya Chalinze ambapo ujenzi wake unaendelea.


Wakati hyuo huo Mkuu huyo wa wilaya Zainabu Kawawa amesema kila mzazi anapaswa kusaini mkataba maalum wa kuthibitisha kuwa mtoto wake atasoma kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne bila ya kukosa.


Katika zoezi hilo la kusaini mikataba amewaagiza maafisa tarafa kusimamia na mzazi au mlezi atakaekwenda kinyume atachukuliwa hatua za kisheria.
Image may contain: 15 people, people smiling, people standing 
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawa, akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa kata na tarafa na wanachi wanaoshiriki ujenzi wa shule ya sekondari Pera Halmashauri ya Chalinze, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Saidi Zikatimu.
  

NAPE APONGEZA KUWASHWA UMEME KIJIJI CHA TULIENI, LINDI.

NA HADIJA HASSAN, LINDI.

Kuzinduliwa kwa Umeme , kupitia mradi wa Umeme Vijijini (REA) katika Kijiji cha Tulieni kata ya Mtua Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Mkoani humo kunaweza kuwa Mwarobaini wa kumaliza changamoto ya upatikanaji wa Maji  inayowakabili wananchi kijijini hapo

Hayo yameelezwa na Mbunge Jimbo la Mtama Nape Nnauye wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa uwashaji wa umeme katika kata hiyo uliofanyika jana katika ofisi za  kijiji cha  Tulieni  na Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji hicho Nape alisema kuwa kutokana na Kijiji  kuwa mlimani wakazi wa maeneo hayo hulazimika kushuka chini (mabondeni) kufuata huduma ya Maji katika mifereji na mito ambayo hata hivyo sio salama kwa afya zao

" Wakati wa Kampeni za uchaguzi mwaka 2015 kijiji hiki kilikuwa na Matatizo Makubwa mawili , moja bara bara ambalo limeshaanza kufanyiwa kazi na wakala wa bara bara mijini na vijijini (TARURA ) kwa kujenga barabra hiyo kwa kiwango cha lami lakini la pili uliposikia akina mama hawa wanapiga Vigere gere hapa tunatatizo kubwa la maji "Alisema Nape

"kutokana na Kijiji hiko kuwa  Mlimani  dawa pekee ya kuyaleta maji huku juu ilikuwa ni Umeme ndio maana tukasema tuanze na Umeme  alafu tuyavute maji kutoka  chini kuyaleta huku juu na awa akina mama waone wako Tanzania mzuri kwa kufungua maji kwenye mabomba" aliongeza Nape

Nape alifafanua kuwa uwekwaji wa umeme katika kijijini hapo kwa kiasi kikubwa utaleta chachu ya kuanzisha mchakato wa kutatua kero ya Upatikanaji wa maji

Akizungumza na Wananchi hao  Naibu Waziri Subira Mgalu  aliwaondoa wasiwasi wanakijiji hao juu ya Upatikanaji wa Maji kwani Serikali ilishaagiza kuzipa kipaumbele Taasisi muhimu kuunganisha umeme  katika maeneo yaliyopitiwa na Miradi ya Umeme Vijijini (REA) kama vile shule, Zahanati , miradi ya maji na Taasisi zingine kama hizo

Hata hivyo Mgalu alimuagiza Meneja wa Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Lindi Mhandisi Felisian Makota Kufikisha Umeme huo mara moja katika chanzo cha Maji Kijijini hapo pindibMchakato huo utakapoanza

Akisoma Taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa usambazaji Umeme Vijijini REA awamu ya tatu mzunguko wa kwanza Meneja wa TANESCO Mkoa wa Lindi Mhandisi Felisian Makota alisema kuwa katika kutekeleza mradihuo kijiji cha Tulieni kimepangiwa kuwa na Wigo wa Msongo wa Umeme K .W  33 ambapo kazi hiyo imekamilika, ujenzi wa Line ndogo kilo mita 2 ambayo mpaka sasa tayari  mkandarasi amejenga kilomita 0.6  pamoja na mashine umba moja ambapo wateja wa awali wanataraji kuwa 14
 Naibu waziri wa Nishati Subira Mgalu (kati kati) na Mbunge Jimbo la Mtama Nape Nnauye (kushoto)
 
Wananchi wa Kijiji cha Tulieni kata ya Mtua Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Mkoani Lindi wakimsikiliza Naibu waziri wa Nishati wakati wa uzinduzi wa kuwasha umeme katika kijiji hicho.


MAGAZETI YA LEO 28 FEB. 2019.

Uzinduzi wa kampeni ya ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili wa kingono wafana dar…viongozi wa dini, jamii yaombwa kumlinda mtoto



 
Maandamano... sehemu ya washiriki katika Kampeni ya ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili wa kingono- “1-5-5 namlinda” yenye kauli mbiu “mlinde mtoto afurahie utoto wake, ujana wake na uzee wake” wakionyesha mabango yao

Mgeni katika shughuli hiyo, Mkuu wa Dawati la kijinsia kutoka makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, DCP  Maria  Nzuki akielezea jambo katika Kampeni hiyo.

Mkurugenzi mtendaji Lilian Liundii akifafanua jambo

Mkurugenzi akiiwa na mgeni rasmi katika kampenii hiyo.
 


Na Selemani Magali
Kampeni ya ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili wa kingono- “1-5-5 namlinda” yenye kauli mbiu “mlinde mtoto afurahie utoto wake, ujana wake na uzee wake” imezinduliwa jana huku viongozi wa kidini na jamii kwa ujumla wakitakiwa kutumia majukwaa yao kuhubri juu ya umuhimu wa kuwalinda watoto dhidi ya vitendo viovu vya ukatili wa kingono, ikisisitizwa kuwa kufanya hivyo kutasaidia kuwalinda watoto.
 Akizungumza katika ufunguzi wa Kampeni hiyo iliyolenga kuamsha Jamii kushiriki katika kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vyote vya Kingono, Mkuu wa Dawati la kijinsia kutoka makao Makuu ya Jeshi la Polisi nchini, DCP  Maria  Nzuki amesema viongozi wa dinii wanayo nafasi ya kupunguza ukatili huo.
“Viongozi wa kiroho wanayo nafasi ya kutokomeza ukatili wa kingono, wao wanawatu wengi na wanaaminika, wakisema jambo waumini wao watalipokea na kulifanyia kazi…basi chukueni na hili mkalifanyie kazi, mara nyingi watu hupendwa kukumbushwa kumbushwa…kumbusheni basi na hili huwenda kukawa na manufaa.” Aliongeza DCP Nzuki.
 Aidha DCP Nzuki amewaomba jamii kuwalinda watoto kwa kutoa taarifa mapema mara tu waonapo ona viashiria vya ukatili wa Kingono, ikiwamo watoto wa shule kuingia quest, kulala katika chumba au nyumba ya msela kisha wakakaa muda mrefu, na matendo yanayofanana na hayo.

Akielezea hali ya ukatilii wa Kingono Tanzania DCP Nzuki amesema kumekuwa na ongezeko ambapo sasa kila sehemu ya yenye wanawake watatu mmoja tayali amewahi kufanyiwa vitendo hivyo, na kuongeza kuwa tatizo ni kubwa linalohitaji nguvu ya pamoja kuliondoa.
 Akizungumzia hatua mbalimbali zinazochukuliiiiwa na Serikali kupambana na hali hiyo, DCP Nzuki amesema kwa upande wa Serikali  kupitia Jeshi la polisi tayari jitihada mbali mbali zinachukuliwa ikiwamo kuweka madawati ya kijinsia katika vituo vya polisi, kuweka vituo vya mkono kwa mkono katika baadhi ya hosptali (one stop centers) pamoja na kuongeza usiri kwa watoa taarifa.
Aidha DCP nzuki amewaka wazazi na walezi wa watoto kufahamu kuwa jukumu la kumlea mototo ni la kwao na wanapaswa kuhakikisha wanamlinda mototo na vitendo vyote vya ukatili wa kingono.
Amesema wazazi wanajukumu la kuwa karibu na watoto wao na kuzungumza madhara ya ukatili wa kingono ambapo itawasaidia watoto kutoa taarifa wakati  wanapofanyiwa vitendo hivyo na watu wasio julikana.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi akielezea kampenii hiyo, amesema Kampeni hii imelenga kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya athari za ukatili wa kingono kwa watoto na umuhimu wa kuwalinda dhidi aina hiyo ya ukatili, kutathmini na kuibua mijadala katika jamii juu ya hali halisi ya ukatili wa kingono, kuhamasisha jamii kuzuia vitendo hivi visitokee na kutoa taarifa mara  waonapo matukio hayo ya ukatili wa kingono kwa watoto ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua stahiki.
Amesema Vitendo hivi vinarudisha nyuma maendeleo ya mtoto na taifa kwa ujumla. Miongoni mwa athari zitokanazo na ukatili wa kingono dhidi ya watoto ni pamoja na watoto kuathirika kisaikolojia, maambukizi ya magonjwa ya zinaa na UKIMWI, mimba za utotoni, na kubwa zaidi ni kuhatarisha ustawi wa taifa na kuchochea uongezeko la vitendo hivi katika jamii.
Ukatili wa Kingono Tanzania bado ni tatiizo sugu, kwa mujibu wa tafitii inaoonyesha kuwa mnamo mwaka 2011, katika wasichana watatu mmoja amefanyiwa na mmoja kati ya wavulana saba wamekutana na ukatili wa kingono kabla ya kutimiza miaka 18.
 Hata hivyo, kulingana na utafiti huo, wengi wa watoto  hawatoi taarifa juu ya vitendo hivyo, wachache wanatafuta huduma  na wachache zaidi wanafanikiwa kupata matibabu au msaada wanapotoa taarifa ya matukio hayo.
 Pia, ripoti iliyotolewa na Kituo cha sheria na haki za binadamu (LHRC) zinaonyesha kuwa matukio ya ukatili wa kingono miongoni mwa watoto  yanaongezeka nchini.
 Kulingana na ripoti hiyo iliyotolewa Juni 2018, wastani wa watoto 394 wamebakwa kila mwezi katika maeneo mbalimbali Tanzania bara, huku ulawiti wa watoto ukiongezeka kutoka  matukio 12 kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2017 hadi matukio 533 kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2018, na mikoa inayoongoza kwa matukio hayo ni Dar es salaam na Iringa.

Ends