Wednesday, October 9, 2019

ZAIDI YA WAKAZI MIL.1.9 ARUSHA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA KUPIGA KURA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

Mkuu wa mkoa wa Arusha akipata maelezo namna ga kujiandikisha kwenye daftari la kupiga kura jana Oktoba 09, 2019, ambapo yeye ni mkazi wa eneo hilo.

Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akipata maelekezo namna ya kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura katika kata ya Murieti ambapo yeye ni mkazi wa eneo hilo.
....................................


Na Vero Ignatus,Arusha.

Zaidi ya wakazi milioni 1.9 mkoa wa Arusha wanatarajia kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura la uchaguzi mdogo wa serikali za mitaa ili kuweza kutimiza haki yao ya msingi ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa ajili ya kujiletea maendeleo katika Nyanja zote.


Richard Kwitega ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha amesema kuwa wananchi hao watapiga kura watakuwa na sifa ya umri wa miaka 18 na kuendelea huku wakiwa na sifa za kuwa wakazi wa eneo husika wanakojiandikishia na kupiga kura .


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amefika na kujiandikisha katika daftari la kupiga kura, katika kata ya Muriet ambako ni mwenyeji wa eneo hilo, amesema kuwa serikali imeweka mazingira rafiki kwa watu wote kujiandikisha bila kujali itikadi za vyama vyao wote wanapaswa kushiriki katika zoezi hilo la kujiandikisha.


Msena Bina ni msimamizi wa Uchaguzi jiji la Arusha amesema kuwa vituo vimefunguliwa 154 kwa ajili ya wananchi kujiandikisha hivyo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Jonathan Shana amesema kuwa jeshi hilo litaimarisha hali ya ulinzi na usalama, na kufanya kazi bila kupendelea chama chochote, kama walivyotoa maelekezo kwa Askari kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo.

No comments:

Post a Comment