Sunday, October 6, 2019

BIl. 93.8 ZATUMIKA KUIMARISHA MIUNDOMBINU KATIKA SHULE 588 ZA MSINGI NA SEKONDARI.

Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo akizungumza wakati alipokuwa akifungua kikao kati ya wizara hiyo na wahariri wa vyombo vya habari uliofanyika katika taasisi ya NACTE Mwenge jijini Dar es salaam.
..............................



Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo amewapongeza waandishi wa habari kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuhabarisha Wananchi kuhusu masuala ya sekta ya elimu na Serikali kwa ujumla.


Dkt. Leonard Akwilapo ameyasema hayo wakati wa kikao kati ya wahariri wa vyombo vya mbalimbali vya habari na wizara hiyo ambapo alielezea  kiwango cha elimu nchini na kusema kinaendelea vizuri na hatua mbalimbali zinafanyika kuiboresha sekta ya elimu.
Ameongeza kuwa Dira ya wizara ni kuwa na Mtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa, stadi, umahiri, uwezo na mitazamo chanya ili kuweza kuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa.

Dkt. Akwilapo ameongeza kuwa jumla ya shilingi  Bil. 93.8 zimetumika kuimarisha miundombinu katika shule 588 za msingi na sekondari zikiwemo shule kongwe, ambapo serikali imeongeza mikopo ya elimu ya juu kutoka Tzs Bil. 424.7 mwaka 2018/2019 hadi Tzs Bil. 450 mwaka 2019/2020.

Akielezea kuhusu  makusanyo ya madeni ya wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu amesema yameongezeka kutoka Tzs Bil. 21.1 mwaka 2014/2015 hadi Tzs Bil. 183.2 mwaka 2018/2019 ambapo wizara inafanya mapitio ya sera ya elimu ya mwaka 2014 ili kuifanyia maboresho na kuendana na wakati.

Amewaasa viongozi wa sekta ya elimu kushirikiana na waandishi wa habari kwa uwazi ili wananchi wapate taarifa za sekta ya elimu zenye usahihi na kwa wakati.
 Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Dkt. Leonard Akwilapo katikati akimsikiliza Katibu Mtendaji wa NACTE, Dr. Adolf Rutayuga wakati alipokuwa akitoa salamu zake za ukaribisho  katika taasisi hiyo.

 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Bi.Sylivia Lupembe akizungumza na kumkaribisha Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Dkt. Leonard Akwilapo ili kuzungumza na wahariri wa vyombo vya habari.

 Ignas Anthony Chonya Mratibu wa Mradi wa TESP Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akizungumza katika kikao hicho kilichoshirikisha wataalam na wakuu wa vitengo kutoka Wizara hiyo na Wahariri wa vyombo vya habari.
 Mhariri Mkuu wa Clouds Media na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake TAMWA Bi. Joyce Shebe akitoa shukurani zake kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,  Dkt. Leonard Akwilapo kufuatia kikao hicho.
 Makuru Petro Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia akiwasilisha mada ya sera na mipango ya wizara hiyo katika kikao hicho.
 Dkt. Lyabwene Mtahabwa Kamishna wa Elimu akiwasilisha mada kuhusu elimu ya Awali wakati wa kikao hicho.

 Baadhi ya wakuu wa vitengo na wahariri wakifuatilia mjadala huo.

 Picha mbalimbali zikionesha wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali wakiwa katika kikao hicho.

No comments:

Post a Comment