Saturday, May 23, 2020

KAMATI YA ALAT PWANI YAIFAGILIA MIRADI YA UJENZI WA SOKO NA MACHINJIO KIBAHA MJI.

No description available.
Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo wakiwa katika kiwanda cha viuwadudu vya mbu walipofanya ziara katika halmashauri ya mji Kibaha kwa ajili ya kutembnelea na kugagua miradi mbali mbali ya maendeleo.(Picha na Victor Masangu)
 ..........................................

VICTOR MASANGU, PWANI.
 
KAMATI ya jumuiya ya umoja wa serikali za mitaa (ALAT Mkoa wa Pwani imewaagiza watendaji na watumishi wa halmashauri kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano kwa  kuweka mipango madhubuti ambayo itasaidia  kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo ili iweze kukamilika kwa muda uliopangwa bila ya kucheleweshwa kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Hayo yalibainishwa  na Mwenyekiti wa Alat Mkoa wa Pwani  Hatibu Chaulembo wakati wa ziara ya kutembelea miradi mitatu ya kimikakati ikiwemo ujenzi wa machinjio ya kisasa, ujenzi wa soko, pamoja na kiwanda cha kuzalisha dawa ya kuulia mazalia ya mbu  viuwadudu ilivyopo katika halmashauri ya Mji Kibaha na kuongeza kuwa wameridhishwa na hatua ambayo imefikia.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema kwamba serikali ya awamu ya tano imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo hivyo inatakiwa isimamiwe ipasavyo na kukamilika kwa wakati ili kuweza kuwasaidia wanannchi wa maeneo mbali mbali katika Mkoa wa Pwani waweze kupata fursa za ajira na wengine kujiajiri wao wenyewe.

“Sisi kama kamati ya Alat Mkoa wa Pwani tumefanya ziara ya kukagua na kutembelea miradi mitatu ya kimikakati katika halmashauri ya mji Kibaha ikiwemo Soko kubwa la kisasa, ijenzi wa machinjio ya kisasa pamoja na kujionea shughuli mbalin mbali za uzalishaji amabzo zinafanyika katika kiwanda cha viuadudu hivyo kwa pamoja tumerudhishwa na mwenendo mzima japo kuna mambo mengine yanatkiwa yafanyiwe kaza zaidi,”alisema Chaurembo.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Musa Gama ambaye pia ni Katibu wa Alat Mkoa wa Pwani alimshukuru Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli kwa kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miradi mbali mbali ambayo itaweza kusaidia kwa kiwango kikubwa kuwasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi na kuondokana na wimbi la umasikini.

Gama alibainisha kuwa utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo ni njia moja wapo ya kuwaondolea wananchi wimbi la umasikini hivyo juhudi ambazo zinafanywa na serikali ya awamu tano chini ya usimamizi mzuri waRais Dk. John Pombe Magufuli hivyo kumamilika kwa miradi hiyo kutakuwa ni chachu kubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

“Mimi kama Katibu wa Alat Mkoa wa Pwani naweza kusema nimejifunz amambo mbali mbali katika ziara hii amabyo tumeifanya katika halmashauri ya mji wa Kibaha kwani nimeweza kujionea ujenzi wa machinjio makubwa ya kisasa pamoja na soko jipya ambayo hivi vyote kwa pamoja vitaweza kuleta mabadiliko chanya kwa wananchi pindi vitakapokuja kukamilika kw ahiyo ni hatua kubwa sana ambayo imefanyika,”alisema Gama.

Nao baadhi ya wajumbe wa kamati YA Alat Mkoa wa Pwani akiwemo Hamisi Dipakutile, Mshamu Munde pamoja na Jenipher Omolo alisema kwamba serikali ya awamu ya tano imeweza kufanya mambo mengi katika sekta mbali mbali hivyo wana imani kuwa katika siku za usoni miradi hiyo pindi ikikamilika italeta maendeleo makubwa kwa wananchi.
No description available.
Baadhi ya wajumbe wa kamati  ya jumuiya ya umoja wa serikali za mitaa ALAT Mkoa wa Pwani wakiwa wanapata maelekezo ya namna ya  kutengeneza dawa ambayo inauwa mazalia ya mbu katika kiwanda cha viuatilifu kilichopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani. walipofanya ziara ya siku moja kwa ajili ya kujionea  shughuli mbali mbali za miradi ya maendeleo (Picha na Victor Masangu)
 No description available.
Wajumbe wakiwa katika maabara ya kuchanagnyia dawa wakifuatilia maelekezo kwa umakini kutoka kwa mtaalamu wa madawa hayupo pichani walipotembelea kiwanda cha viuadudu vya mbu kilichopo Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani .(Picha na Victor Masangu)
No description available.
Mwonekano wa  baadhi ya wajumbe wa kamati ya Alat Mkoa wa Pwani wakiwa katika chumba amabcho kuna mitambo maalumu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kuchanganyia madawa ya aina mbali mbali ikiwemo dawa kwa ajili ya kuulia mazalia ya Mbu.(Picha na Victor Masangu)
No description available.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ambaye pia ni Katibu wa kamati ya Alat Mkoa wa Pwani Musa Gama akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa wataalamu wa kuchanganya madawa kwa ajili ya kuulia mbu katika kiwanda cha viuadudu walipofanya ziara kwa ajili ya kujionea shughuli mbali mbali.(Picha na Victor Masangu)
No description available.
Baadhi wa wajumbe wa kamati ya Alat Mkoa wa Pwani wakiwa kwa nje ya soko la kisasa ambalo linajengwa Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani mara baada ya kuhitimisha ziara hiyo ya kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo.(Picha na Victor Masangu)
No description available.
Mmoja w awajumbe wa kamati ya Alat Mkoa wa Pwani akiwa katika chumba chenye mitambo ambayo inatumika katika utengenezaji na uzalishaji wa madawa ya kuulia mazalia ya mbu. (Picha na Victor Masangu)
No description available.
Katibu wa Alat Mkoa wa Pwani Musa Gama kati kati akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa ziara ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo katika halmashauri ya Kibaha mji.(Picha na Victor Masangu)