Tuesday, October 1, 2019

MAHITAJI YA CHAKULA KUONGEZEKA KWA ASILIMIA 60 IFIKAPO MWAKA 2050

 Naibu Waziri wa Kilimo Mh.Omary Mgumba akifungua mkutano wa kuwasilisha kwa Wabia wa Maendeleo mpango kazi wa utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kupunguza Upotevu wa Mazao kwenye mkutano uliofanyika ukumbi wa Kizenga Makumbusho jijini Dar es salaam.
..............................

Inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050 kutakuwa na watu bilioni tisa (9) hivyo mahitaji ya chakula yanakadiriwa kuwa asilimia 60 zaidi ya ilivyo sasa.


Hayo yamesemwa jana septemba 30, 2019 na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Omary Mgumba, katika hutuba aliyoitoa kwenye ufunguzi wa mkutano wa kuwasilisha kwa Wabia wa Maendeleo mpango kazi wa utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kupunguza Upotevu wa Mazao.


Akizungumza katika ufunguzi huo, Mh. Mgumba amesema Mahitaji ya chakula yanakadiriwa kuwa asilimia 60 zaidi ya ilivyo sasa.


“Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Umoja wa mataifa umedhamiria kutokomeza baa la njaa kwa kuhakikisha kuna usalama wa chakula na lishe, kupunguza upotevu wa mazao na kukuza kilimo endelevu ifikapo mwaka 2030”. Alisema Mh. Mgumba.


Aidha, Mh. Mgumba alisema kuwa mkazo umewekwa katika kuongeza uzalishaji wenye tija wa mazao ya chakula ili kufikia malengo endelevu.


” Udhibiti wa upotevu wa mazao ya chakula ni suala muhimu na la kipekee ambapo linapaswa kupewa kipaumbele ili kufikia malengo hayo”. Alieleza Mh. Mgumba.


Pamoja na hayo, Mh. Mgumba alisema kuwa Usalama wa chakula ni moja ya lengo kuu la Wizara ya Kilimo katika kuchochea ukuaji wa Uchumi wa Viwanda ili kutekeleza agenda kuu ya serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mh. Dkt. John Pombe Magufuli.
 Bw. Clespin Josephat Mratibu wa Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu Tanzania (TANIPAC) akizungumza katika mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa Kizenga Makubusho jijini Dar es salaam.

Felix Bachmann Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la HELVETAS akiwasilisha mada katiia mkutano huo.
Naibu Waziri wa Kilimo Mh.Omary Mgumba akwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo  uliofanyika ukumbi wa Kizenga Makumbusho jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment