Sunday, October 13, 2019

MVUA YALETA MADHARA KAGERA.

Migomba ikionekana kuanguka baadaa ya mvua iliyoambatana na upepo kunyesha katika wilaya ya Karagwe mkoani Kagera hapo jana Oktoba 12, 2019.
........................................

Na Alodia Dominick, Bukoba.

Mvua za kimbunga zilizonyesha zikiwa zimembatana na upepo mkali zimeezua nyumba sita na mashamba ambayo idadi yake haijafahamika mara moja katika kitongoji cha Misha kata ya Rugu wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.


Diwani wa Kata ya Rugu Adirian Kobushoke amethibitisha kutokea kwa kimbunga hicho na kusema kuwa kimetokea jana Oktoba 12, 2019 majira ya saa tisa alasiri iliponyesha mvua kubwa ikiwa imeambatana na upepo mkali na kusababisha migomba na mikahawa kuanguka chini na nyumba sita kuezuliwa na upepo.


Kobushoke amesema, bwana shamba wa Kata ya Rugu akishirikiana na afisa mtendaji wa Kata hiyo wanafanya tathimini ya migomba na mikahawa iliyoanguka ili kubaini thamani halisi ya hasara iliyowakumba wananchi wa kitongoji cha Misha ni pamoja na thamani ya nyumba zilizoezuliwa na upepo.


"Kimbunga hicho licha ya kuangusha migomba na mikahawa pamoja na kuezua nyumba hakuna madhara mengine yaliyotokea kwa wananchi". Alisema Kobushoke.


Mmoja wapo ambaye nyumba yake imeezuliwa na upepo Vumilia Endrew amesema yeye ana familia ya watu nane, yeye na mkewe naa watoto sita, baada ya nyumba yake kubomoka jana ametoa taarifa katika uongozi wa kitongoji na kijiji pamoja na kata na kupewa turubai ambayo imemsaidia kwa ajili ya makazi tangu jana wakati jitihada nyingine zikiendelea kufanyika.
 
Baadhi ya nyumbazilizo ezuliwa mapaa yake katika kitongoji cha Misha kata ya Rugu wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.

No comments:

Post a Comment