Wednesday, October 23, 2019

RC. ZAMBI ATOA MAAGIZO KWA DC MPYA WA NACHINGWEA.

 
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi (kushoto) akimkabidhi ilani ya Uchaguzi ya CCM, Mkuu mpya wa Wilaya ya Nachingwea Hashimu Komba, mara baada ya kumuapisha.
 
Mkuu mpya wa Wilaya ya Nachingwea Hashimu Komba, akila kiapo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
........................................................
Na Hadija Hassan, Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi  Oktoba 23, 2019 amemuapicha Mkuu mpya wa Wilaya ya Nachingwea Hashimu Komba huku akimtaka ahakikisha Mradi wa upanuzi wa soko unakamilika ndani ya mwezi mmoja.

Tukio hilo limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu huyo wa Mkoa wa Lindi kufuatia Mkuu wa Wilaya hiyo uteuzi wake kutenguliwa hivi karibu na Mhe, Rais.

Zambi alisema ni lazima wafanya biashara hao walioacha kutumia eneo hilo la Soko kwa muda mrefu waweze kurejea katika maeneo yao ndani ya mwezi mmoja ili waweze kuendelea na Shughuli zao kama zamani.

Hata hivyo Zambi pia alimtaka Mkuu huyo wa Wilaya kwa kushirikiana na Ofisa mipango na Mkurugenzi mtendaji Mpya wa Halmashauri hiyo HASSAN ABAS RUNGWA kupitia upya matumizi ya fedha katika mradi wa ujenzi wa mabweni mawili ya Shule ya Nachingwea high school kutokana na fedha za mradi huo kuisha kabla ya mradi kukamilika.

Pamoja na mambo mengine Zambi akizungumzia kuhusu stand mpya amemuagiza kamanda wa polisi Mkoa wa Lindi prudensiana protans, amuagize Mkuu wa Polisi Wa wilaya ya Nachingwea kutangaza kuwa magari yote yaliyorudi stand ya zamani kuanzia  oktoba 24 yarudi stand mpya.

"kama alivyosema mhe, Rais kuwa hakuagiza watu warudi Stendi ya zamani bali tunatakiwa kuipangia matumizi stendi hiyo, nikuagize RPC ili tusimpe kazi kubwa huyu Mkuu mpya wa Wilaya muagize OCD wako wa kule awatangazie watu wa kule kwamba kuanzia Tarehe 24 Mgari yote ya abiria yarudi Stendi Mpya" alifafanua Zambi.

Akizungumza Baada ya tukio hilo la kula kiapo Mkuu huyo Mpya wa Wilaya ya Nachingwea, Hashimu Komba alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini na kumteuwa kushika nafasi hiyo huku akiahidi kufanyia kazi maelekezo yote aliyopewa sambamba na kuomba ushirikiano kwa viongozi na watumishi wenzake

No comments:

Post a Comment