Tuesday, October 1, 2019

WAZAZI WATAKIWA KUWA KARIBU NA WATOTO WAO.

  Wahitimu wa darasa la saba 2019 katika shule ya Msingi ya Yemen DYCCC iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam wakiwa katika sherehe ya mahafali yao.
 
Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DYCCC, Mohammed Abdallaah Bin Ishaaq, akizungumza katika mahafali hayo.
..................................


Wazazi na walezi wametakiwa kuwa karibu na watoto wao ili watoto waige tabia njema kutoka kwao.


Wito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya DYCCC inayomiliki shule za Yemen DYCCC zilizopo Chang'ombe jijini Dar es laam, Mohammed Abdallaah Bin Ishaaq, alipokuwa akizungumza katika mahafali ya wahitimu wa darasa la saba shuleni hapo.


Alisema njia nzuri ya mtoto kujifunza ni kuwa karibu na mzazi ambapo ataweza kuiga mambo kutoka kwa mzazi badala ya kuiga kutoka kwa watu wengine ambao watakuwa na mila na desturi zao tofauti na zile za familia yako.


Aliongeza kuwa, mzazi anapaswa kuwa karibu na mtoto huku akijenga nae urafiki ili mtoto awe huru kuuliza maswali ya kujifunza na kuiga tabia njema.


Alisema ikiwa mtoto utamkataza kitu fulani kuwa ni haramu au kina madhara, ni vyema ukamtolea ufafanuzi na kuweka wazi madhara ya kitu hicho ili nae awe na elimu juu ya madhara hayo jambo litakalomjengea hofu na kutokufanya kitendo hicho.


Aidha, Mohammed Abdallaah ametahadharisha kuwa, mapenzi ya kuwa karibu na mtoto yasiwe yale ya kumruhusu kufanya kila kitu na badala yake mzazi ndio anatakiwa kutoa muongozo wa kitu gani mwanae afanye na kipi asifanye.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu wa shule za DYCCC, Hassan Akrabi, alisema changamoto iliyopo sasa katika malezi ni kukua kwa teknolojia ya mitandao hali inayopelekea vijana kuinia kwenye mitandao hiyo bila ya kuchagua kilicho kizuri.


Aliongeza kuwa, watoto hawana upambanuzi wa kujua vitu vibaya kulingana na umri wao hivyo wazazi wana wajibu wa kuwasimamia ili kuwaongoza kwenye matumizi katika matumizi ya mitandao ya kijamii.


Alisema kuwa, katika matumizi ya mitandao ya kijamii kuna faida lakini pia yapo madhara mengi ambayo tahadhari isipochukuliwa mapema na wazaz na walezi vijana wengi wataharibika kimaadili.


Akizungumza kwa niaba ya wazazi, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Habibu Suluo amewataka vijana waliohitimu darasa la saba shuleni hapo kuendeleza maadili ya dini ya kiislamu waliyopata shuleni hapo ili wapate radhi za Mwenyezimungu, Subhaanahuwataala  duniani na akhera.


Alisema katika jamii kuna vishawishi vingi hivyo wanapaswa kutumia akili zao kwa elimu waliyopata kukabiliana na vishawishi hivyo na kwamba wao waendelee kuwa mfano wa kuigwa katika jamii.


jumla ya vijana 89 wamehitimu elimu ya msingi shuleni hapo kati yao wavulana ni 43 huku wasichana wakiwa ni 46
 
Mwenyekiti wa Bodi ya elimu shule za DYCCC, Hassan Akrabi, akizungumza katika mahafali hayo.

 Meneja wa shule za Yemen DYCCC zilizopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam, Jamila Awadhi akizungumza katika mahafali hayo.
  Makamu Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Habibu Suluo, akizungumza katika mahafali hayo, kulia ni Mjumbe wa Bodi, Salmeen Aljabry na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule za DYCCC, Hassan Akrabi.
 
 Makamu Mwenyekiti wa bodi ya DYCCC, Mohammed Abdallaah Bin Ishaaq, (kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya shule za DYCCC, Hassan Akrabi (kulia) wakiangalia michezo iliyokuwa ikionyeshwa na vijana wahitimu wa darasa la saba 2019, shule ya msingi Yemen DYCCC.

 
Wahitimu wa darasa la saba 2019 katika shule ya Msingi ya Yemen DYCCC iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam, wakionyesha michezo aina mbalimbali katika sherehe za mahafali yao.
 
Wahitimu wa darasa la saba 2019 katika shule ya Msingi ya Yemen DYCCC iliyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam wakiwa katika sherehe ya mahafali yao.

No comments:

Post a Comment