Sunday, January 15, 2017

SAMAKI MKUBWA AKUTWA UFUKWENI BAGAMOYO.



Afisa Uvuvi wilaya ya Bagamoyo Aboubakari Mposo, akizungumza na bagamoyokwanzablog.

Samaki mkubwa mwenye  urefu  wa futi 36 na kimo  cha futi  10 amekutwa amekufa kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi katika  Kijiji cha  Kaole wilayani Bagamoyo.

Akizungumza na waandishi wa Habari,  Afia Uvuvi wilaya ya Bagamoyo, Aboubakari Mposo alisema Samaki huyoanajulikana kwa jina la Chongoe ambae sio mara  nyingi kuonekana kwake na kwamba bado haijafahamika kifochake kimesababishwa na nini.

Mposo  aliwataka wananchi wanaoishi karibu na ufukwe wa  Bahari  kutoa  taarifa kwenye  m amlaka zinazohusika mara wanapoona kiumbe wa ajabu ili  wahusika wafanye utafiti na  kubaini  aina ya  kium be hicho na sababu za kifo chake.

Wananchi  katika  Kijiji cha  Kaole  walioshuhudia  samaki huyo wamesema wameona faraja kumuona samaki  mkubwa kama huyo  am b apobaadhiya watu hawakuwahi  kufikiria  kama  baharini  kuna  samaki  mkubwa kama huyo.

Kwa upande wao  wavuvi  wazoefu katika  Pwani ya  Bagamoyo  wamesema kuwa Samaki huyo  aina ya  Chongoe  n diy huyo  anaefahamika pia kwa jina la Nyangumi,   na  kuongeza kuwa samaki huyo hana  shida  hata  pale  anapokuwa mzima na kukutana nae  katika Bahari. 

Kwa mujibu wa wakazi wa Kaole wamesem a  Samaki huyo aligundulika katika ufukwe huo Tarehe  14 jumamosi wakati tayari akiwa am eshakufa na kwamba  haifahamiki alikufa  lini  kwakuwa anaonekana alikufa siku kadhaa zilizopita.


Wananchi mbalimbali waliofika Kwenye ufukwe wa Bahari kijiji cha Kaole wilayani Bagamoyo kujionea Samaki huyo mkubwa.




Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga, kushoto alifika kushuhudia samaki huyo, kulia ni Diwani wa kata ya Dunda, Dicksoni  Makamba.



Wananchi mbalimbali walifika katika eneo hilo la Kaole kushuhudia  samaki huyo.

No comments:

Post a Comment