Tuesday, October 29, 2019

MBUNGE KAWAMBWA AGAWA MILIONI 31 KWA VIKUNDI BAGAMOYO.

Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, akikabidhi hundi kwa Kudura Selemani kutoka kikundi cha Ushirika.
........................................
 Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, amegawa fedha zaidi ya milioni 31 kwa vikundi na taasisi katika jimbo hilo.

 
Akizungumza mara baada ya kukabidhi fedha hizo Dkt. Kawambwa alisema kuwa, fedha ni zile za mfuko wa jimbo ambazo zipo kisheria na zinatolewa na serikali kwaajili ya kusaidia mambo mbalimbali katika jimbo husika.


Alisema fedha hizo alizogawa ni jumla ya 31, 801,000 ni kwaajili ya kuchochea maendeleo kwa vikundi vya wajasriamali na taasisi ambazo hazipaswi kurudishwa.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi wa jimbo la Bagamoyo, kujiunga katika vikundi ili weweze kuwa na sifa ya kupata fedha za mfuko wa jimbo na zile asilimia kumi zinazotolewa na Halmashauri.


Alisema serikali imetenga fedha kwaajili ya kuwezesha wananchi katika maeneo mbalimbali ambapo ili uweze kupata fedha hizo ni lazima muwe katika kikundi.


Alifafanua kuwa, serikali haiwezi kugawa fedha kwa mtu mmoja mmoja ispokuwa fedha zitatolewa kwa vikundi ili iwe manufaa kwa watu wengi zaidi.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally Issa amewataka wanavikundi na taasisi zilizopata fedha hizo kuzitumia katika malengo yaliyokusudiwa  ili zilete tija kwenye jamii.


Alisema ni kweli fedha hizo hazitarudishwa lakini vikundi vitapitiwa kukaguliwa ili kujiridhisha kuhusu matumizi ya fedha hizo.


Kwa upande wao wanavikundi waliopata fedha hizo wamemshukuru Mbunge Dkt. Kawambwa kwa kupatia kiasi hicho ambacho kitasaidia katika kusukuma maendeleo kwenye maeneo yao.


Walisema serikali ya awamu ya tano imekuwa ikijali watu wa aina zote na ndioamana fedha hizo zimewafikia jambo ambalo hawakulitarajia.
 
Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, akikabidhi hundi kwa Golden Mwenda Magagula kutoka kikundi cha Unjacha.
 
Mbunge wa jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, akizungumza na wana vikundi katika ukumbi wa Halmashauri ya Bagamoyo, kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally Issa, na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya hiyo, Fatuma Omari Latu.


 Kutoka kulia ni Diwani wa viti maalum, Hapsa Kilingo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Ally Issa, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Fatuma Omari Latu, Katibu wa CCM wilaya ya Bagamoyo, Salum Mtelela, na Amina Ramadhani.

Diwani wa kata ya Zinga, Mohamedi Mwinyigogo (kulia) akiwa na Diwani wa viti Maalu, Shumina Rashidi, wakimsikiliza katibu wa Mbunge, Magreth Joseph aliyesimama.




No comments:

Post a Comment