Friday, June 8, 2018

TAARIFA KWA UMMA JUMUIA ZA KIDINI NA VYAMA VYA KIJAMII

Ofisi ya Msajili wa Jumuia za Kidini na Vyama vya Kijamii Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inazikumbusha Taasisi zote za Kidini na Vyama vya Kijamii vilivyosajiliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kulipa Ada na Madeni waliyonayo kabla ya tarehe 30/6/2018.

Sheria ya Jumuia, Sura ya 337 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002 (The Societies Act) inayozisajili Jumuia za Kidini na Vyama vya Kijamii inawataka wote waliosajiliwa kulipa ada zao za kila mwaka kwani kutokulipa ada ni kukiuka masharti ya Sheria iliyowasajili.

Jumuia za Kidini na Vyama vya Kijamii vinatakiwa kufika kwenye Ofisi za Msajili wa Vyama vya Kijamii na Taasisi za Kidini ili kuhakiki madeni yao hivyo kuwawezesha kulipa madeni stahiki wanayodaiwa pamoja na ada zao za mwaka huu wa fedha.

Uhakiki wa madeni hayo utahusisha nyaraka mbalimbali kama vile risiti ya mwisho ya malipo, nakala ya Cheti cha Usajili na Taarifa ya Utendaji yenye saini za Viongozi wawili.

Malipo yote yawasilishwe kupitia benki ya NMB Akaunti namba 20110013811 yenye jina MOHA REVENUE COLLECTION.

WAFICHUENI WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI.

Wanafunzi wa shule za Bagamoyo wakiwa kwenye maandamano kuadhimisha wiki ya Elimu.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) Alphonce Amuli, akiongea kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo.
.....................................
Wazazi na walezi wilayani Bagamoyo wametakiwa kutoa ushirikiano ili kuwafichua wale wote wanaowapa mimba wanafunzi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga katika hutuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) Alphonce Amuli wakati wa maadhimisho ya wiki ya Elimu.

Alisema watoto wengi hukatisha masomo kwasababu ya kupewa mimba lakini juhudi za kukomesha vitendo hivyo zinakwama kutokana na wazazi au walezi kutotoa ushirikiano kwa vyombo vya sheria ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Aliongeza kwa kusema kuwa serikali imetunga sheria kali katika kuhakikisha vitendo vya kuwapa mimba wananfunzi vinakomeshwa ili watoto wa kike wapate elimu ambayo ni haki yao ya kikatiba.

Akizungumzia swala la elimu Amuli alisema kufuatia viwanda vinavyoendelea kujengwa wilayani Bagamoyo watoto wanapaswa kupewa elimu itakayowanufaisha katika soko la ajira na ile ya kujiajiri.

Aidha, alisema serikali kwa kutambua umuhimu wa elimu inatoa elimu bure kwa wote na kutoa fedha zitakazosadia upatikanaji wa elimu bure ili kila mtoto apate elimu.

Aliongeza kuwa walimu wakuu wanapaswa kusimamia vizuri fedha za elimu bure ikiwa ni pamoja na kuzipeleka kwenye matumizi stahiki ili lengo la serikali liweze kutimia.

Alisema kufuatia hali hiyo wazazi na walezi jukumu lao ni kuwapeleka watoto shule na kuwasimamia ipasavyo.

Awali akisoma Taarifa ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Afisa Elimu Msingi Peter Fussi alisema kufuatia utoaji wa elimu bure idadi ya wanafunzi  wanaoandikishwa shule za awali na msingi imeongezeka kutoka wanafunzi 25228 mwaka 2017 na kufikia 27508 mwaka 2018.

Hata hivyo fussi alisema Halmashauri ya Bagamoyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa ambapo mahitaji  katika idara ya elimu ya msingi ni vyumba 621 na kwamba vilivyopo ni 292 na hivyo kufanya upungufu wa vyumba vya madarasa ni 329.

Aliongeza kuwa idara ya elimu sekondari mahitaji ni vyumba vya madarasa 162 yaliyopo ni madarasa 124 ambapo pungufu ni madarasa 38.

Wiki ya elimu huadhimishwa kila mwaka ikiwa na lengo la kutoa fursa kwa shule, serikali na wadau mbalimbali kutathmini changamoto zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni  Uwajibikaji wa pamoja kwa elimu bora kwa watu wote.
 
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) Alphonce Amuli akipokea maandamano ya wanafunzi yalipowasili uwanjani.
 Wanafunzi wa Chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM)wakiongoza maandamano katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika uwanja wa majengo Bagamoyo.
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika Bagamoyo Alphonce Amuli akikagua mabanda yaliyoandaliwa na shule mbalimbali kama anavyoonekana pichani akiwa katika banda la shule ya msingi Nianjema ambapo alijionea Teknolojia ya habari na namna ya masomo mengine yanavyofundishwa.

Alphoncee Amuli ni kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu ( ADEM) ambae alimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga.
 
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika Bagamoyo Alphonce Amuli akikagua mabanda yaliyoandaliwa na shule mbalimbali kama anavyoonekana pichani ambapo alijionea namna ya masomo yanavyofundishwa.


Alphonce Amuli ni kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu ( ADEM) ambae alimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga.
Mgeni rasmi katika maadhimisho ya wiki ya elimu yaliyofanyika Bagamoyo Alphonce Amuli akikagua mabanda yaliyoandaliwa na shule mbalimbali kama anavyoonekana pichani ambapo akiwa katika banda la ADEM ambapo alijionea namna ya masomo yanavyofundishwa.

Alphonce Amuli ni kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu ( ADEM) ambae alimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga
Sehemu ya wananfunzi walioshiriki maadhimisho hayo ya wiki ya elimu.
Wanafunzi wa shule ya Mwanamakuka wakionyesha umahiri wao katika maonyesho ya sarakasi

Thursday, June 7, 2018

UMITASHUMTA YAZINDULIWA CHALINZE



Sehemu ya washiriki wa UMITASHUMTA wa Halmashauri ya Chalinze.
 
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwangaakizungumza wakati wa uzinduzi wa UMITASHUMTA wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Said Omari Zikatimu, wa tatu ni Afisa Elimu msingi Zainabu Makwinya na wa mwisho ni Afisa Elimu Taaluma Miriam Kihiyo.
................................................
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga amewataka vijana wa shule za msingi kusoma kwa bidii ili vipaji walivyonavyo wavitumie wakiwa na elimu.

Majid aliyasema hayo wakatai wa uzinduzi wa mashindano ya  Uendeshai wa Michezo ya Taaluma Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) uliofanyika katika viwanja vya shule ya Lugoba Halmashauri ya Chalinze.

Alisema michezo inaibua vipaji kwa watoto lakini ni vyema vipaji hivyo vikatumika sambamba na elimu kwani mwenye elimu hutumia vizuri kipai chake.

Aidha aliwataka walimu kuwasimamia watoto mashuleni katika kuhakikisha wanapata elimu bora sambamba na kudumisha michezo ambayo itawajenga ki afya na ukakamavu wa miili yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Edes Lukoa amewataka vijana wa shule za msingi kuwa na bidii katika michezo ili kukuza vipaji vyao kwaaili ya maendeleo ya baadae.

Alisema wachezaji wakubwa wa michezo mbalimbali duniani wameanza wakiwa wadogo hivyo na wao wasikate tamaa na badala yake waongeze juhudi.

Aidha, aliwataka kuwa na nidhamu kwa walimu wao ili waweze kuelewa kile wananchofundishwa na hatimae kufaulu vizuri katika masomo yao pamoja na michezo.

Awali akisoma Taarifa mbele ya mgeni rasmi Afisa Elimu Taaluma Halmashauri ya Chalinze Miriam Kihiyo alisema Halmashauri ya Chalinze itatoa timu moja itakayoshiriki katika mashindano ya kumtafuta mshindi wa Mkoa.

Alisema michezo itakayoshindaniwa ni Mpira wa miguu, Mpira wa pete, Mpira wa Mikono na Mpira wa wavu.
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Saidi Omari Zikatimu akizungumza katika uzinduzi wa UMITASHUMTA.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Edes Lukoa akizungumza katika uzinduzi wa UMITASHUMTA.

  Afisa Elimu Taaluma wa Halmashauri ya Chalinze Miriam Kihiyo akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Risala.
 
 
  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Edes Lukoa akiwa gorini kwaajili ya kudaka mpira kuashiria uzinduzi wa UMITASHUMTA katika Halmashauri ya hiyo.


 Vijana kutoka timu ya Msata na Chalinze wakichuana katika mechi ya ufunguzi iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Lugoba.

SERIKALI YA BAGAMOYO YAFANYIA KAZI MAOMBI YA WANANCHI KUHUSU MSITU WA ZIGUA.

Kaimu meneja wa TFS Chalinze Jonathan Mpangala (katikati) akiwaonyesha wajumbe wa kamati siasa wilaya ya Bagamoyo mipaka ya msitu wa Zigua katika kijiji cha kwa Mduma.
  
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga wa kwanza kushoto akizungumza na wnanchi katika kijiji cha kwa Mduma.
 ..........................................
Serikali wilayani Bagamoyo imepokea ombi la wnanchi katika kijiji cha Kwa Mduma kata ya Kibindu la kutaka kuongezewa eneo la makazi kutoka msitu wa Zigua.

Kauli hiyo imetolew na Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Majid Mwanga wakati wa ziara ya kukagua mipaka ya Msitu wa Zigua.

Mkuu huyo wa wilaya alisema lengo la ziara hiyo ambayo imewajumuisha kamati ya siasa wilaya ni kupata uelewa wa pamoja kuhusu hitajio la wananchi wa kwa Mduma na kuona namna gani wanaweza kuwasilisha maombi ya wananchi hao ngazi za juu.

Alisema kufuatia ukweli kwamba sehemu wanayodai ni muhimu kwakuwa tayari kuna zahanati ambayo inawahudumia wananchi hao, serikali ya wilaya inachukua ombi hilo na kuwasilisha kw Mkuu wa Mkoa ili kuona namna ya kurekebisha mipaka ya TFS katika kijiji hicho.

Kaimu meneja wa TFS Chalinze Jonathan Mpangala lisema  katika harakati za kuondoa wavamizi ndani ya msitu wa zigua zipo baadhi nyumba kijiji cha kwa Mduma hazikubomolewa kutokana na kusikiliza maoni ya wananchi wa kijiji hicho.

Alisema nyumba hizo ni pamoja Zahanati, nyumba ya Mganga na nyumb 8 za watu binafsi ambapo vikao vimefanyika ngazi ya wilaya ili kuona namna kurekebisha mipaka upande huo wa kijiji cha kwa mduma.

Aliongeza mchakato unaendelea kuanzia ngazi ya kijiji, wilaya nakanda ambapo ofisi ya kanda itawasilisha mapendekezo hayo ngazi Taifa.

Nae Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo Abdu Rashid Zahoro amesema Chama cha Mapinduzi wilaya kitashirikiana na serikali kuona namna bora ya kurekebisha mipaka ya msitu huo.

Alisema CCM wilaya imejionea hali halisi ya malalamiko ya wananchi hao na kwamba wameona haja ya kuwashughulikia malalamiko yao ili eneo hilo libaki kwa makazi ya watu na shughuli za kibinadamu kama watakavyoona inafaa serikali ya kijiji.
  Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bagamoyo Abdu Rashid Zahoro akizungumza na wananchi wa kijiji cha kwa Mduma.
 
Kaimu meneja wa TFS Chalinze Jonathan Mpangala (katikati) akiwaonyesha wajumbe wa kamati siasa wilaya ya Bagamoyo ramani ya msitu wa Zigua katika kijiji cha kwa Mduma.
 
 Wajumbe wa kamati siasa wilaya ya Bagamoyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya, wakati walipotembelea msitu wa Zigua katika kijiji cha kwa Mduma.
 Kaimu meneja wa TFS Chalinze Jonathan Mpangala (wa pili kushoto) akiwaonyesha wajumbe wa kamati siasa wilaya ya Bagamoyo mipaka ya msitu wa Zigua katika kijiji cha kwa Mduma.
 

Tuesday, June 5, 2018

JAFO APIGA MARUFUKU MAMLUKI KUSHIRIKI UMISSETA NA UMITASHUMTA



Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amewataka Wakuu wa Mikoa kuhakikisha kuwa mikoa yao inapeleka wachezaji wanafunzi watakaoshiriki mashindano ya UMISSETA iliyoanza leo katika viwanja vya chuo cha Ualimu Butimba kilichopo jijini Mwanza.

Aidha amewataka waamuzi watakaochezesha mashindano hayo pamoja na yale ya UMITASHUMTA kuhakikisha kuwa wanachezesha michezo hiyo kwa kuzingatia kanuni na sheria bila kuwepo upendeleo ili washindi wa michezo yote wapatikane kwa haki.


Akizungumza  na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Waziri Jafo alieleza kuwa mashindano ya Umoja wa Michezo ya Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) yaliyoanza leo yatafanyika yataendelea hadi hadi Juni 15 mwaka huu.


Mashindano ya UMISSETA yatafuatiwa na michezo ya UMITASHUMTA ambayo yatafanyika katika viwanja hivyo hivyo kuanzia tarehe 17 juni 2018 hadi tarehe 29 juni 2018.


Waziri Jafo alieleza kuwa michezo hiyo inatarajiwa kufunguliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa katika uwanja wa CCM Kirumba hivi karibuni.


Kwa mujibu wa Mhe.jafo, jumla ya wanamichezo 3,360 watashiriki mashindano hayo wakitokea mikoa 28 upande wa Umisseta, 26 Tanzania Bara na miwili ya Zanzibari, huku Umitashuta mikoa 26 ya Tanzania Bara tu.


Kwa upande wa Umisseta michezo itakayochezwa ni pamoja na soka kwa wavulana na wasichana, netiboli kwa wasichana, wavu kwa wasichana na wavulana, mpira wa mikoni, mpira wa kikapu, riadha maalumu(watu wenye ulimavu).


Mingine ni Riadha ya kawaida, mchezo wa bao kwa wavulana, sanaa za maonyesho (kwaya, ngoma, mashairi, ngonjera) na mpira wa meza.