Thursday, October 17, 2019

SHULE YA EMI YAHITAJI MIL. 80 KUJENGA KITUO.

 
Mkurugenzi wa shule ya Thobias Joachim, akisoma taarifa ya shule hiyo mbele ya mgeni rasmi.
 
Mkurugenzi wa shule ya Thobias Joachim, akimkabidhi taarifa ya shule hiyo mgeni rasmi Meneja wa benki ya CRDB Mkoa wa Pwani Rose Kazimoto.
...................................

Na Omary Mngindo, Kibamba.

SHULE ya EMI School iliyopo Kibamba Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, inahitaji zaidi ya shilingi milioni 80 kujenga Kituo Mtaa wa Kongowe, wilaya ya Kibaha mkoani Pwani.

Aidha taarifa ya Mkurugenzi wa shule hiyo Thobias Joachim imetanabaisha kwamba, mbali ya wanafunzi wanaoishi na wazazi, pia inawasomesha watoto wanaoshi kwenye mazingira hatarishi, wanaotokea maeneo mbalimbali.


Taarifa ya Mkurugenzi mbele ya Rose Kazimoto Meneja wa benki ya CRDB Mkoa wa Pwani katika mahafari ya tano tangu kuanzishwa kwake, imeeleza kuwa awali walihitaji milioni 200 kwa ajili ya kununua eneo Mtaa wa Kongowe Kibaha ili wajenge kituo kwa ajili ya kuendeleza watoto kielimu.

"Nitumie fursa hii kuwashukuru wazazi na walezi wa wanafunzi, pia wadau waliojitolea katika kufanikisha upatikanaji wa kiasi cha shilingi milioni 120 kati ya shilingi milioni 200, tayari tumeshanunua eneo Kongowe, sasa tunatafuta fedha kwa ajili ta kuanza ujenzi," ilieleza taarifa ya Mkurugenzi huyo.


Akizungumza na wazazi na walezi wa wanafunzi hao, mgeni rasmi Rose alianza kumpongeza Mkurugenzi Joachim na watumishi wake, kwa kuona umuhimu wa kuwasomesha bure watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi, huku akiwaomba wadau kujitokeza kusaidia juhudi hizo.

"Katika taarifa iliyosomwa na Mwalimu Mkuu imegusia changamoto ya sisi wazazi kutolipa ada, niwaase tuwe tunalipa kwa wakati ili tusikwamishe juhudi zinazofanywa na uongozi wa shule, pia tuache kuwahamisha watoto wetu katika shule kwa kukwepa ada," alisema Rose.

Mwenyekiti wa Kamati ya shule Ramadhani Sinale naye amewaasa wazazi kujitokeza katika kusaidia maendeleo ya shule, huku akieleza kwamba imekuwa mkombozi mkubwa katika eneo hilo kwa kuwapatia elimu safi vijana.

"Pamoja na hayo Changamoto za uendeshaji, miundombinu, kitaaluma tunaendelea kuzitatua, pia ada inatugusa wazazi, anajitahidi kuzitatua, hatuna vifaa vya kufundishia kama kompyuta ambavyo ni muhimu hapa shuleni," alisema Sinale.

No comments:

Post a Comment