Wednesday, August 31, 2016

HALMASHAURI YA BAGAMOYO, YAFANIKIWA KUKUSANYA MAPATO MARA KUMI ZAIDI.

Mwenyekiti  wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy, kushoto, na kulia ni Makamo mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Mohamedi Usinga
.................................

Ukusanyaji mapato ya ndani katika Halmashauri ya  Bagamoyo umeongezeka mara  kumi  zaidi ukilinganisha na siku  za nyuma.
Hayo yamebaishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo, Aliy Aliy alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Halmashauri mara baada ya kumaliza kikao cha baraza la madiwani kilichomalizika  leo.

Mwenyeki huyo wa Halmashauri alisema kuwa Halmashauri ya Bagamoyo imejipanga vizuri katika vyanzo vyake vya mapato ili kukusanya mapoto halisi yanayo  kusudiwa na kufikia lengo lililowekwa na Halmashauri katika  kukusanya  mapato ya  ndani.

Aliongeza kuwa utekelezaji  wa miradi  mbalimbali ya  maendeleo unategemea ukusanyaji mzuri wa mapato ambapo kwa namna walivyojipanga wameweza kukusanya  mapato mara  kumi  zaidi ya kawaida.

Akivitaja vyanzo vya mapato ambavyo  wameweza kuvisimamia vizuri  ni  pamoja na Kituo  cha mabasi, Geti  la kukusanya  ushuru  kwa maliasili  sanzale, Ushuru wa samaki pamoja na machimbo ya  Mchanga yaliyo eneo la Kiromo ambapo hivi karibuni  wanatarajia kupeleka nguvu zaidi kwenye ukusanyaji  kodi zamajengo.

Kufuatia Hali hiyo, Mwenyekiti huyo ambae ni Diwani wa kata ya Fukayosi, alisema ana matumaini makubwa kwamba wanaweza kufikia lengo la kukusanya  bilioni 2 na milioni mia nane ili kukidhi  mahitaji ya Bajeti ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2016/17.

Aliongeza kuwa, katika mikakati ya kuhakikisha halmashauri inakusanya  mapato ya kutosha, imeongeza kodi za pango kwa watumishi wanaoishi kwenye nyumba za serikali na kwamba tayari watumishi wa serikali wamepewa mikataba mipya kwaajili ya ongezeko la kodi ya   pango.

Aidha, aliongeza kuwa, katika makusanyo hayo asilimia kumi inarudishwa kwenye kata zinazosimamia  makusanyo hayo ili kata nazo  zifanye  maendeleo yake ya kata ambapo hiyo itakuwa ni motisha  kwa kata kuendelea kukusanya mapato  kwa wingi.

Hata hivyo, Mwenyekiti huyo wa Halmashauri alisema kuwa, licha ya kasi ya ukusanyajiwa  mapato  lakini bado wanaendelea kumthamini mwananchi wa kawaida wa chini anaefanya  biashara ndog ndogo.

Alisema kwa wafanyabiashara ndogondogo ambao hawapo  kwenye fremu hawatalipa kodi kama alivyoagiza Rais wa Jamhuriya  Muungano, vinginevyomtu awe ameweka biashara yake kwenye fremu.

Alitolea mfano wa wauzaji mkaa wa majumbani hawatalipa ushuru  mpaka wawe kwenye fremu na wakaanga chipsi wa mitaani  pia hawatalipa ushuru vinginevyo  awe  anakaangia ndani ya fremu









SERIKALI YA TANZANIA YAENDELEA KUPINGA NDOA ZA JINSIA MOJA.

Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakati wa ufungaji wa kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo.
 

Wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakimsikiliza Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu wakati wa ufungaji wa kikao kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam.
.......................................


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kushikilia msimamo wake wa kupinga ndoa za jinsia moja,kuongeza uwigo wa uhalalishaji wa utoaji mimba,adhabu ya kifo,kuweka sera ya kutonyonga wanaokutwa na adhabu ya kifo na uridhiwaji wa mikataba ya Kimataifa inayozuia masuala ya utesaji kwa kuwa masuala hayo yanaonekana kutoendana na Katiba na Sheria za nchi, Sera,mila desturi na tamaduni za watanzania ikiwa ni sehemu ya mapendekezo 72 yaliyokataliwa na Serikali wakati wa mapitio ya taarifa ya nchi ya ukuzaji na usimamizi wa haki za binadamu.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Mdemu ameyasema hayoleo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga kikao maalumu cha siku mbili cha wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu ambapo ameeleza kuwa Serikali ilipokea jumla ya mapendekezo 227 yaliyotolewa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mwezi Mei 2016 chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review).

Mdemu ameongeza kuwa mapendekezo hayo kwa ujumla yalijikita katika majukumu ya Tanzania kwenye mikataba ya kimataifa ,Mifumo ya kikatiba na kisheria,miundombinu ya kitaasisi ya haki za binadamu ,masula ya kisera,ushirikiano na vyombo vya kikanda na kimataifa,utawala wa sheria,uendeshaji haki,masuala ya kulinda haki za msingi za binadamu kama vile haki ya kuishi,haki ya afya,haki za walemavu,watoto,haki ya habari na kujieleza,afya elimu mazingira haki za watu asilia na wakimbizi.

Hata hivyo, Tanzania ilikubali kutekeleza mapendekezo 130 tu kati ya 227 yaliyokuwa yanahusu mchakato wa Katiba,kuijengea uwezo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuhuisha Sera za nchi ili ziendane na malengo endelevu ya Dunia ,kuandaa taarifa za nchi za utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu na kuziwasilisha kwenye vyombo vya vya umoja wa mataifa kwa wakati.

Vilevile Serikali iliahirisha jumla ya mapendekezo 25 ambayo yalijikita katika marekebisho ya sheria ya Takwimu, 2015, Sheria ya makosa ya mtandao, 2015,ukamilishaji wa Sheria ya Habari, Sheria ya vyombo vya Habari,uandaaji wa mikakati na mipangokazi ya utekelezaji wa msuala ya kuzuia ndoa za utotoni na za kulazimishwa ,upitishaji wa sera mpya mbalimbali ikiwemo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa na usajili wake kuwa bure na masuala ya uchaguzi Zanzibar, kwa lengo la kuyapitia tena kwa kina na kushirikisha zaidi wadau ili hatimaye kuweka msimamo stahiki kabla mapendekezo hayo hayajawasilishwa tena Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa hatua za mwisho za kupitisha rasmi taarifa ya nchi katika kukuza na kulinda haki za Binadamu.

Aidha, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda na kukuza haki za bindamu ikiwa ni pamoja na kupokea hoja na maoni ya wadau ili kuboresha taarifa ya nchi itakayowasilishwa katika Baraza la Haki za Binadamu la umoja wa mataifa kabla au ifikapo tarehe 9 Septemba, 2016 na kuwataka watanzania wote kushiriki ipasavyo katika dhana nzima ya kukuza na kulinda haki za bindamu nchini.

Utaratibu wa Mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review) wa masuala ya haki za binadamu ulianzishwa na Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2006 kwa lengo la kuzifanyia mapitio nchi 192 ambazo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania ikiwa miongoni, kwa lengo la kuangalia utekelezaji wa masuala ya kulinda na kukuza haki za binadamu nchini mwao.

DOTO M. JAMES, ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU WA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw.Doto M.James aliyeteuliwa leo na Rais Dkt John Pombe Magufuli kushika wadhifa huo.