Posts

Showing posts from 2026

KAMATI YA BUNGE (PIC) YAITAKA TANAPA KUBORESHA UWEKEZAJI KATIKA HIFADHI ZA TAIFA.

Image
  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) Agosti 13, 2026, imelielekeza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kuendeleza mikakati ya kuboresha uwekezaji katika maeneo ya Hifadhi za Taifa nchini, Kuboresha miundombinu, na kuongeza mazao mapya ya utalii ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania pamoja na mapato yatokanayo na shughuli za utalii. Maelekezo hayo yametolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Rashid A. Shangazi (Mb) katika kikao kilichofanyika Bungeni Dodoma kikiwa na lengo la kupitia na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa miradi ya uwekezaji katika Hifadhi za Taifa, uhifadhi, utalii pamoja na mikakati ya kuongeza mchango wa sekta ya utalii katika kukuza uchumi wa Taifa. Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Wizara wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Nkoba E. Mabula, viongozi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na Men...

CCM TABORA YATOA MAAGIZO KWA BODI YA TUMBAKU KUMALIZA KERO ZA WAKULIMA

Image
  Na Allan Kitwe, Tabora CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Tabora kimeitaka Bodi ya Tumbaku nchini (TTB) kuja na mikakati thabiti itakayosaidia kumaliza kero za wakulima wa zao hilo Mkoani humo na Mikoa mingine hapa nchini. Agizo hilo limetolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tabora Said Juma Nkumba alipokuwa akizungumza kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa kilichofanyika jana Wilayani Kaliua Mkoani hapa. Amesema kuwa zao la tumbaku ni zao muhimu sana kwa uchumi wa wakazi wa Mkoa huo na Mikoa mingine, lakini limekuwa likikabiliwa na changamoto kadha wa kadha hali ambayo imekuwa ikilalamikiwa mno na wananchi. 'Naipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali ambazo imekuwa ikichukua ili kuhakikisha kilimo kinaboreshwa na masoko ya uhakika yanapatikana’, ameeleza. Komredi Nkumba amedokeza kuwa CCM inajivunia mafanikio makubwa ambayo yameendelea kupatikana katika sekta ya kilimo na sekta nyingine na kuongeza kuwa kero w...

DC NICKSON SIMON: USHIRIKIANO WA SERIKALI NA NGOs NI NGUZO YA MAENDELEO YA WANANCHI

Image
  KIBAHA – Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mhe. Nickson Simon, amezitaka Asasi Zisizo za Kiserikali (NGOs) wilayani humo kuimarisha ushirikiano na Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kuongeza tija na kuleta matokeo chanya kwa wananchi. Akifungua kikao cha mashauriano kati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na wawakilishi wa NGOs kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, DC. Nickson alisema Serikali na NGOs zina lengo moja la kuwaletea wananchi maendeleo, hivyo ni muhimu shughuli na miradi inayotekelezwa iwe na mshikamano na kuendana na vipaumbele vya taifa. Alieleza kuwa ushirikiano huo unaonekana katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu, ambapo Serikali na NGOs zote zinatekeleza miradi ya kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Aliongeza kuwa hali hiyo pia ipo katika sekta za afya, mazingira, haki za binadamu pamoja na uwezeshaji wa makundi maalumu. Katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya aliainisha maeneo muhimu yanayopaswa kupewa kipaumbele na NGOs kwa kuzi...

KAMATI YA UCHUMI UJENZI NA MAZINGIRA BAGAMOYO YAKAGUA MIRADI.

Image
  Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi Ujezi na Mazingira Mhe Amiry Sanday Mpwimbwi leo tarehe 13 Agosti 2026 ameongoza Kamati hiyo kutembelea na kukagua miradi inayoendelea katika Halmashauri ya Mji Bayamoyo  Mwenyekiti wa Kamati ametoa Pongezi kwa uongozi wa kiwanda cha Kamal kinachotengeneza Oil kwa uwekezaji wao katika Halmashauri ya Mji Bagamoyo na kuzalisha Ajira kwa vijana wa Bagamoyo  Pia Mhe Amiry amesema kuwa  changamoto ambazo zimeelezwa na uongozi wa Kamal wamezichukua na watahakikisha wanazifanyia kazi ili kuona zinatatuliwa kwa wakati ili uzalishaji usikwame. Kamati ya Uchumi pia imetembelea na kukagua Maendeleo ya kiwanda cha Sinovest investment limited kilichopo Kata ya Zinga kinachofanya uzalishaji wa nguo ambapo kiwanda hicho pia bado kinaendelea na ujenzi pamoja na ufungaji wa miundombinu kwa ajili ya uzalishaji. Mhe Mwenyekiti ametoa maagizo kwa Afisa Biashara kuhakikisha wanaendelea kusimamia Yale ambayo yanaendelea katika Kiwanda hicho na kuendelea ku...

BAGAMOYO, KAMATI YA ELIMU, AFYA NA MAJI HUDUMA ZA JAMII YAFANYA ZIARA.

Image
  Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu Afya na Maji Mhe Mwanaharusi Jarufu leo tareh 13 Agosti 2026 ameongoza wajumbe wa Kamati hiyo kufanya Ziara katika maeneo yanayotoa Huduma za Kijamii. Mhe. Mwanaharusi Jarufu pamoja na wajumbe wa Kamati hiyo wametembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo kuona huduma zinazotolewa katika Hospitali hiyo na kupatiwa maelezo kuhusu huduma hizo na utaratibu wa utoaji wa huduma hizo. Mhe Jarufu amesema kuwa  suala la uwepo wa changamoto ya ucheleweshaji wa kutoa huduma kwa Wananchi wanaohitaji huduma hasa upande wa maabara ipo haja ya kuona ni namna gani wanabadilika na kuwa na huruma kwa Wananchi hao  Aidha Mhe Mwenyekiti huyo wa Kamati amesisitiza kuweka utaratibu mzuri ambao utamwezesha Mgojwa ambae ameenda hospitali kupata huduma kujua utaratibu uliopo na kupokelewa kwa lugha nzuri pamoja na huduma bora kwa ujumla  Pia Kamati ya Elimu Afya na Maji imetembelea kikundi cha Ufugaji Wanawake Mvuleni kilichopo Kata ya Kisutu kitongoji ch...

DKT. MWIGULU NCHEMBA AREJESHA TABASAMU KWA WANANCHI WATANO, MGOGORO WA ARDHI MTONI KIZINGA

Image
  Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba,  tarehe 11 Agosti 2026, amerejesha tabasamu kwa wananchi watano baada ya kufanikisha maridhiano ya mgogoro wa umiliki wa Kiwanja Na. 2013 na 2014, Kitalu “U”, eneo la Mtoni Kizinga, Manispaa ya Temeke, jijini Dar es Salaam, uliodumu kwa miaka 17 kati ya mfanyabiashara Hersi Warsame Mohamed na wananchi hao. Katika mgogoro huo, wananchi hao wakiongozwa na Bw. Ivan Kihiyo, walimwandikia barua Mheshimiwa Waziri Mkuu wakilalamika kuwa mfanyabiashara Hersi Warsame Mohamed amejimilikisha eneo lao kinyume cha sheria. Wananchi hao walimuomba Waziri Mkuu awasaidie kutatua mgogoro huo. Timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu iliyotumwa na Waziri Mkuu kutatua mgogoro huo, ikiongozwa na Mwenyekiti ambaye pia ni Msaidizi wa Waziri Mkuu – Mahusiano, Asasi za Kiraia na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Bw. Tryphone Mkolokoti, na Katibu wake ambaye pia ni Msaidizi wa Waziri Mkuu – Masuala ya Ardhi, Bw. Senso Magessa, ilifanikiwa kufanikisha maridhiano h...

MAKAMU WA RAIS AMTEMBELEA MAMA FATMA KARUME HOSPITALI.

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemjulia hali, Mama Fatma Karume,Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, ambaye anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Lumumba Zanzibar. Tarehe 13 Agosti 2026.

KAMATI YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAKUTANA NA WATENDAJI WA WIZARA YA MADINI.

Image
  Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Subira Mgalu (Mb), wamekutana na Watendaji wa Wizara ya Madini wakiongozwa na Waziri wake. Mhe. Anthony Mavunde (Mb) Agosti 11, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Bunge. Katika kikao hicho, Kamati imepokea na kujadili taarifa ya Wizara ya Madini kuhusu hali ya sekta ya madini nchini, ikijumuisha uzalishaji, biashara, masoko, uwekezaji, mauzo ya nje na makusanyo ya maduhuli ya Serikali. Baada ya kupokea na kujadili taarifa hiyo, Wajumbe wa Kamati walitoa maoni yao ya kuboresha sekta ya madini nchini kuanzia kwenye uchimbaji, uuzwaji na masuala ya kodi yanayohusika katika biashara ya madini.