Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, akiwa katika picha ya pamoja na Mfalme wa Sweden, Carl XVI Gustaf, wakati alipokwenda kumuaga katika Jumba la Kifalme jijini Stockholm, tarehe 19 Machi, 2026 (Picha kwa hisani ya Jumba la Kifalme). ....................................................... Mfalme Carl XVI Gustaf wa Sweden, amemuaga aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Jumba la Kifalme jijini Stockholm, jana tarehe 19 Machi, 2026. Katika mazungumzo yao mafupi, viongozi hao walijadiliana namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili katika sekta za nishati, mazingira, kilimo, utalii, miundombinu, madini na teknolojia. Mfalme Gustaf aliipongeza Tanzania kwa kuweka utulivu nchini na kubuni mipango thabiti ya kutafuta maendeleo na kukuza uchumi wake licha ya changamoto nyingi zinazoikabili dunia nzima hivi sasa. Balozi Matinyi alimshukur...