Monday, December 3, 2018

WANAUME LINDI WATAKIWA KUWASINDIKIZA WAKE ZAO CLINIC.

NA HADIJA OMARY, LINDI

Mkuu wa Mkoa wa Lindi  Godfrey Zambi awataka wanaume wa Mkoa huo kuhusika moja kwa moja katika kuwasindikiza wenza wao  Clinic  wanapokuwa wajawazito pindi wanapokwenda kupata huduma, Huku akiwataka Wakuu wa wilaya kulisimamia jambo hilo



Zambi ameyasema hayo juzi katika uzinduzi wa Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama” yenyelengo la kuongeza kasi ya uwajibikaji kwa kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga uliofanyika katika manispaa ya Lindi Mkoani humo



Alisema kuna baadhi ya wanaume wa maeneo mengi wanawageuza wanawake wao kama chombo cha kuwapatia wanaume watoto jambo ambalo sio sawa



Alisema ili kuweza kupata takwimu za wanaume wangapi wametekeleza agizo hilo ni muhimu kwa Waganga Wakuu wa Wilaya kuwa na Dafutari la kumbukumbu maalumu  litakaloonyesha ni wanawake wangapi wamekenda clinic na wanaume wao



“ni lazima tuweke kumbukumbu za namna hiyo na kama tunaona mama mjamzito anaudhuria clinic zaidi ya mara tatu au mara nne, mume ajaonekana na mwanaume wake  yupo ila hataki kwenda kwa makusudi , lazima mwanaume huyo afuatwe na serikali tuchukuwe hatua hili ni agizo langu” alisema Zambi



“serikali tupo mahari pote haiwezekani tukawatumia tuu mama zetu kama chombo cha kutuletea watoto wakati sisi wenyewe tunawajibu, ni kazi muhimu ambayo wamepewa na mwenyezimungu  kwahivyo lazima tuwasamini wake zetu ”aliongeza Zambi 

No comments:

Post a Comment