Monday, December 3, 2018

VIFO 893 VYA KINA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA VYARIPOTIWA MKOANI LINDI 2017/2018.

NA HADIJA OMARY- LINDI

Jumla ya vifo(893) vya akinamama wajawazito na watoto wachanga vimetokea Mkoani Lindi kutokana na sababu mbali mbali  ikiwemo kutokwa na Damu nyingi wakati wa kujifungua kipindi cha January 2017-oktoba 2018 



Hayo yameelezwa na mganga mkuu wa Mkoa wa lindi (RMO) Dkt. John Sijaona, alipokuwa anatoa taarifa ya mkoa huo kwenye uzinduzi wa kampeni ya “jiongeze tuwavushe salama” yenyelengo la kuongeza kasi ya uwajibikaji kwa kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga uliofanyika katika manspaa ya Lindi Mkoani humo



Alisema vifo hivyo vikiwemo na vya watoto wafu vimetokea kwa kipindi cha mwezi januari-disemba 2017 na January-oktoba mwaka 2018



Alifafanua  katika kipindi hicho vifo vya akinamama wajawazito vilikuwa 88 watoto wachanga vilikuwa 449 huku watoto waliozaliwa wakiwa wafu vilikuwa 207

Aidha aliongeza kuwa  kwa kipindi cha mwezi January hadi Disemba mwaka 2017 pekee  akina mama waliofaliki kwa uzazi walikuwa 49 watoto wachanga waliokuwa na siku 1-28 walikuwa 290 huku watoto waliozaliwa wakiwa wafu wakiwa 207



Hata hivyo sijaona aliongeza kuwa katika kipindi cha mwezi January-oktoba mwaka 2018 vifo vya akina mama wajawazito vilikuwa 39 na watoto wachanga waliochini ya siku 1-28 walikuwa 396



Akieleza sabubu zilizochangia vifo hivyo Dk, Sijaona alisema kuwa miongoni mwa sababu zilizopelekea vifo hivyo ni kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua,(PPH) kwa asilimia 31, upungufu wa damu, kuchelewa kufika katika kituo cha Afya na kifafa cha uzazi



Sijaona pia alitaja sababu zilizopelekea vifo kwa watoto wachanga ni pamoja na kushindwa kupumua baada ya kuzaliwa(birthasphyxia) kuzaliwa wakiwanjiti(premuturity) na kupata maambukizi 



Akizungumza baada ya kuzindua kampeni hiyo Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi amesema kuwa ili kampeni hiyo ya “jiongeze Tuwavushe salama” iweze iweze kuleta tija na kufikia malengo yake ni lazima kuwepo na uwajibikaji  kwa kushirikiana na watumishi wa umma katika Nyanja mbali mbali za huduma



Hata hivyo Zambi alisema kuwa vifo vingi vya akinamama wajawazito na watoto wachanga vinaweza kuepukuka kama jamii itashirikiana kwa pamoja katika kuweka na kuongeza jitihada za kudhibiti vifo hivyo


No comments:

Post a Comment