Saturday, December 8, 2018

NYASA MATATANI FEDHA ZA UJENZI WA VITUO VYA AFYA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kushoto) akimkabdihi cheti cha kuhitimu na kufaulu mafunzo ya Uongozi Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe.Christina Mndeme wakati wa kufunga mafunzo ya Uongozi.
....................................

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameinyooshea kidole Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwa hali inayoendelea ya kusuasua kwa Ujenzi wa Vituo vya Afya.

Kutokana na hali hiyo Waziri Jafo amemuagiza Naibu Katibu Mkuu anayeshugulikia Afya Bi. Zainabu Chaula kufuatilia Halmashauri hiyo na kufahamu kwa kina sababu zilizopekea kushindwa kutekeleza ujenzi wa Vituo vya Afya kama walivyoelekezwa.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati wa kufunga mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu  wa Mikoa na Makatibu Tawala yaliyofanyika kwa siku Tano katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo alisema  Fedha za Ujenzi wa Vituo zina miongozo na taratibu zake na kuna muda maalumu wa utekelezaji wa miradi hiyo sasa inakuwaje Halmashauri imekwishapata Fedha halafu hakuna utekekezaji nini kinakwamisha ilihali fedha ipo tayari kwenye akaunti ya Halmashauri husika

“Pale Nyasa kuna tatizo na nataka kufahamu kwa kina sababu zilizosababisha kukwama kwa ujenzi wa kituo cha Afya Timu ya Wataalamu iende huko mara moja ili tuweze kuchukua hatua stahili na kituo cha Afya kijengwa wananchi wapate huduma za Afya”

Aliongeza kuwa Wakuu wa Mikoa mambo haya yanatendeka katika maeneo yenu ya utawala ukiwa kama msimamizi wa shughuli zote za Serikali mnapaswa kufahamu na kuchukua hatua za stahiki na kuhakikisha malengo ya Wizara yanafikiwa.

‘Tusikubali mtu au kundi la watu likarudisha nyuma jitihada zetu za kumletea mtanzania maendeleo, Serikali imetoa fedha nyingi sana kwa ajili ya mwananchi tuzilinde fedha hizo na tusimamje miradi itekelezwe kwa kiwango’ alisema Jafo.

Awali akifunga mafunzo hayo Waziri Jafo aliwapongeza viongozi hao kwa ukomavu wa kiuongozi waliouonyesha wakati wote wa Mafunzo na kuwataka kufanyia  kazi elimu waliyoipata na  kuleta mabadiliko chanya na ya haraka katika jamii wanayoiongoza.

Aidha aliwataka kuongeza Wakuu hao wa Mikoa na Makatibu Tawala kuongeza umakini katika usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ili thamani ya fedha iweze kuonekana.

Akitoa taarifa ya awali Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Prof. Joseph Semboja alisema kuwa viongozi hao wameonyesha kuelewa vizuri  mada zote walizofundishwa na wametoa ushirikiano wa hali ya juu wakati wakati wote wa mafunzo hayo.

Somo kubwa walilopewa viongozi wetu ni namna ya kuwa kiongozi wa kimkakati,  kusimamia rasilimali watu na kuitumia ipasavyo na namna nzuri ya kujijengea sifa binafsi alisema Pro. Semboja.

Makundi muhimu ya viongozi wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa yamekwishapata mafunzo haya kwani  yalianza kutolewa kwa Wakurugenzi wa halmashauri zote Nchini, Wakuu wa Wilaya na kwa kumalizia na Makatibu Tawala Mikoa pamoja na Wakuu wa Mikoa.

No comments:

Post a Comment