Wednesday, December 5, 2018

DUNDA KINARA WA ELIMU BAGAMOYO

 Diwani wa Kata ya Dunda Dickson Makamba akizungumza katika hfla hiyo.
..................................
Na Omary  Mngindo, Bagamoyo

JUMUIA ya Wazazi wilaya ya Bagamoyo  Mkoa wa Pwani inatarajiwa kuandaa harambee kubwa katika Kata ya Dunda inayolenga kupatikana kwa fedha zilizotumika kumalizia Bweni sekondari ya Kata. 

Mjumbe Kamati ya Utekelezaji jumuia hiyo Wilaya Yahya Msonde, aliyemwakilisha Mwenyekiti wa Jumuia hiyo wilaya Aboubakary Mlawa, katika hafla ya kupongezwa walimu katani humo kwa kufanikisha Kata hiyo kuwa ya kwanza kiwilaya. 

"Nilipopewa taarifa na Mwenyekiti wangu Mlawa kuja kumwakilisha kwenye hafla hii,  nilijiuliza mara milimbiko nini cha kuzungumza,  lakini kwa kuwa nami ni mdau wa elimu siwezi kukosa la kuzungumza,  lakini la kwanza niwasilishe hili la Harambee inayohimizwa ifanyike wiki ya kwanza mwezi Januari, " alisema Msonde. 

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, diwani wa Kata ya Dunda Dickson Makamba alianza kwa kuwapongeza walimu kwa kazi kubwa wanavyoendelea kuifanya katani humo,  akisemaa kwamba huu ni mwaka wa tatu mfululizo kushika nafasi hiyo.

"Niwashukuru walimu kwa kujitoa kikamilifu katika kuhakikisha Kata ya Dunda inaendelea kuwa kinara katika imu, pia wazazi, walezi na wadai mbalimbali wanaoendelea kusaidia katika nyanja tofauti za kuhakikisha elimu inaendelea kuboreshwa katani hapa," alisema Makamba. 

Akizungumzia changamoto ya Bweni kwenye shule ya Kata,  Makamba alisema kuwa kuna juhudi nyingi zinazoendelea kufanyika akiwemo Mwenyekiti wa Jumuia hiyo aliyechangia mabati 100, lengo kuhakikisha wanafunzi wanakaa shuleni. 

"Mbali ya Jumuia pia kuna wadai wengi ambao wamechagia ujenzi wa Bweni akiwemo Mbunge wa Jimbo Dkt.  Shukuru Kuwambwa aliyechanga mifuko 100 ya saruji pamoja na wadau wengi waliojitolea na wengine bado wanaendelea kujitokeza kusaidia elimu katani Dunda, " alisema Makamba.

Mwalimu Mkuu shule ya Mwambao Alpu Mwegeho akitoa shukrani kwa niaba ya walimu wenzake, alitoa kilio cha kucheleweshwa mafao ya walimu hali inayopunguza hamasa ya walimu wilayani humo. 

Mwakilishi wa wazazi Ummy Matata amepongeza juhudi za walimu, huku akisema kwamba kwa miaka mingi suala la ufaulu katani humo halikuwepo, huku akimpongeza Diwani Makamba kwa kushirikisha watu mbalimbali. 

Taarifa ya Walimu katani humo iliyosomwa na Saad Momba mwalimu shule ya Msingi Mwambao inazungumzia changamoto ya ukosefu wa kompyuta hali inayochangia kupunguza uwezo wa wanafunzi katika elimu. 
 
Mjumbe Kamati ya Utekelezaji jumuia ya wazazi Wilaya, Yahya Msonde, ambae alikuwa mgeni rasmi kumuwakilisha Mwenyekiti wa jumuiya hiyo.

 
Mjumbe Kamati ya Utekelezaji jumuia ya wazazi Wilaya, Yahya Msonde,akikabidhi zawadi kwa mwalimu Amina Ally wa shule ya msingi MWASAMA.

 
Mjumbe Kamati ya Utekelezaji jumuia ya wazazi Wilaya, Yahya Msonde,akikabidhi fedha taslimu shilingi laki moja kwa mwalimu 
 
Mjumbe Kamati ya Utekelezaji jumuia ya wazazi Wilaya, Yahya Msonde, akikabidhi zawadi kwa Mwenyekiti CCM kata ya Dunda, Mwinyi Hashim Akida.


No comments:

Post a Comment