Sunday, December 2, 2018

CCM PWANI YATOA AGIZO ZITO KWA WATENDAJI WAKE.

MNEC wa mkoa wa pwani (kushoto) akimsikiliza mwenyekiti wake katika kikao na watendaji wa CCM wilaya zote za mkoa wa Pwani.
......................................................

Na Shushu Joel, Kibaha.
MWENYEKITI wa ccm mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno amewaagiza watendaji wa chama hicho kuacha kufanya kazi kwa mazoe kama walivyokuwa wamezoea miaka ya nyuma.

Watendaji wa Ccm walio wengi wameshindwa kuendana na kasi ya awamu ya tano chini ya mwenyekiti wa taifa Dkt John Pombe Magufuli ambaye pia ni Rais wa Tanzania kwa watendaji wengi kufanya kazi za chama kipindi cjha chaguzi tu.

Akizungumza na watendaji wa mkoa huo mwenyekiti huyo aliwataka watendaji wote kuwajibika kwa wanachama wa chini katika kuwasaidia kutambua sitahiki zao kwani wanachama wa chini wamekuwa wakinyanyaswa na matajili huku viongozi wa chama wakiangalia tu na kushindwa kuwajibika katika kuwasaidia ili waweze kupata haki zao.

 “Watendaji wa chama wamekuwa wajijisahau katika uwajibika wao na kibaya zaidi wamekuwa ni watu wa kuagiza tu huku wakiwa wamekaa ofisini”Alisema

Aliongeza kuwa watendaji wa chama ndio mhimiri mkubwa katika chama hivyo ni lazima watendaji wote katika mkoa wahakikishe wanakuwa ni kiungo kikubwa kati ya uongozi na wanachama wea chini.

 Aidha amewataka watendaji kuwa wabunifu katika kipindi hiki kutokana na kuwa kipindi cha sasa ni kipindi cha siasa ni uchumi kwa kuwaelimisha wanachama juu ya umuhimu wa kuwa na vikundi vilivyosajiliwa katika vyombo husika ili waweze kukopesheka na kujijengea uchumi wao ambao utawatoa katika kipindi cha kuwa omba omba kwa watu.

Kwa upande wake mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa kupitia mkoa wa Pwani (NEC)Haji Jumaa amempongeza mwenyekiti huyo kwa kuona umuhimu wa kukutana na makatibu wote wa mkoa wa Pwani na kuwakumbusha wajibu wao katika utendaji.

Aliongeza kuwa watendaji wakisimama imara katika usimamizi wa mali za chama hali ya ccm itakuwa zaidi ya hapo ilipo sasa.

“Makatibu wanapaswa kuwajibika kwa bidii ili kuhakikisha chama chetu kinazidi kuwa bora kuanzia ngazi za mashina mpaka taifa na hii inawezekana pale kila mmoja atahakikisha anakuwa mkali kwa yule mwenye nia mbaya na chama katika kutumia mali za chama ovyo”Alisema Jumaa.

Aliongeza kuwa zoezi la kuwasajili wanachama wa ccm kwa njia ya kielectronic ni jema kwani liwaongeza mapato ya chama na kukifanya chama kuwa juu zaidi ya hapo kilipo sasa.

Naye katibu wa ccm wilaya ya Kibaha vijijini Janeth Mnyaga ameupongeza uongozi wa ccm mkoa kwa kuwakutanisha na kuwataka kuwajibika katika shughuli zao za usimamizi wa chama katika ngazi za wilaya.

Hivyo aliongeza kuwa elimu iliyotolewa leo kwa watendaji wote iwe endelevu kwani inawapatia motisha katika uwajibikaji na usimamizi wa chama katika ngazi za wilaya.

Makatibu wa CCM mkoa wa Pwani wakimsikiliza mwenyekiti wa mkoa huo akitoa maelezo juu yao.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno aliyesimama akitoa maelekezo kwa watendaji wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment