Tuesday, December 11, 2018

BENKI KUU YATAJA FAIDA YA DHAMANA ZA SERIKALI KWA MAENDELEO YA TAIFA.

Mshauri  wa Benki Kuu ya Tanzania BoT tawi la Dodoma akifafanua jambo katika semina hiyo inayoendelea jijini Dodoma.
..................................

WATANZANIA wameshauriwa kushiriki kikamilifu katika minada ya dhamana za Serikali kwani faida zake ni kubwa kwa Taifa ikiwamo kufanya shughuli za maendeleo kwa kutumia fedha zake za ndani.

Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Masoko na Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Alexander Ng’winamila wakati akiwasilisha mada katika mafunzo kwa waandishi wa habari za uchumi na fedha yalioandaliwa na BoT kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuandika habari za fedha na uchumi.

Akizungumza wakati akitoa mada inayohusu uwekezaji katika dhamana za Serikali; faida zake kwa Taifa na wawekezaji ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu kwenye midana ya dhamana za Serikali.

Amesema ametoa ombi kuendelea kuhamasisha kutolewa kwa elimu kwa umma ili waweze kushiriki kikamilifu na hatimaye kuifanya serikali iweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa fedha za ndani.”Ombi letu kwa vyombo vya habari tunaomba muendelee kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa kushiriki kwenye dhamana za Serikali.

Kuna faida nyingi na mojawapo ushiriki wao utawezesha Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za ndani badala ya kwenda kukopa nje ya nchi,”alisema.

Akifafanua zaidi zinazopatikana kwenye dhamana za Serikali ni kusaidia Serikali kugharamia bajeti iwapo kutakuwa na upungufu wa kibajeti, kupata fedha za kuendeshea miradi ya maendeleo , kusimamia ujazi wa fedha katika uchumi, husaidia kudhibiti mfumuko wa bei , huchagia uwepo wa soko la upili na husaidia kuhamasisha utafutaji wa mitaji kwa taasisi zingine.

Pia amesema hutoa fursa za uwekezaji ,hivyo kuwepo kwa ushindani katika uwekezaji mbalimbali na kusaidia kupatikana kwa riba zinazoaminia na soko huku akieleza kwa mwananchi wa kawaida faida
za kushiriki ni nyingi kwani ni sehemu salama kutokana na ukweli kwamba Serikali haitarajiwi kukiuka mategeo ya wadai wake wakati wa malipo.

Ametaja faida nyingine dhamana za Serikali zinahamishika hivyo mwekezaji anaweza kuuza muda wowote.Pia dhamana za Serikali zinaweza kutolewa kama dhamana kwa ajili ya mikipo na faida nyingine ni kwamba dhamana za Serikali zina kiwango cha faida inayoridhisha.”Tunaendelea kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye
dhamana za Serikali kwa maendeleo ya Taifa letu.”

Kuhusu midana ya dhamana za Serikali amesema ipo ya aina mbili ambapo kuna mnada wa muda mfupi ambao ni wa mwaka mmoja na mnada wa dhamana za Serikali wa muda mrefu ambao unaanzia miaka miwili mpaka miaka 20.

Pia amesema ili mwekezaji aweze kushiriki katika minada ya dhamana za Serikali ni lazima awe na akaunti ya uwekezaji katika dhamana za Serikali na kwamba ufunguzi wa akaunti ya dhamana za Serikali hufanyika kupitia kwa mawakala walioidhinishwa ambao huwasilisha.

“Wakati wa kufungua akaunti kuna taarifa muhimu ambazo zinahitaji zikiambatanishwa na kitambulisho halali kinachotambulika na mamlaka za nchi pamoja na namba ya mlipa kodi(TIN) ”amefafanua. 

Ng’winamila amesema fomu za kujiunga zinapatikana kupitia mawakala waliopo nchini pamoja na kwenye tovuti ya Benki Kuu ya Tanzania ambapo ametumia nafasi hiyo kufafanua unapozungumzia dhamana za Serikali kwa lugha rahisi ni kwamba Serikali inakopa kwa wananchi wake.
Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha Benki Kuu ya Tazania Bw. Alexander Nw’winamila akitoa mada ya uuzaji wa Hati Funagani na Amana za Serikali katika semina ya waandishi wa habari za Fedha na Uchumi inayofanyika jijini Dodoma katika tawi la Benki Kuu ya Tanzania BoT Dodoma ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo.
Bi. Zalia Mbeo Meneja Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BoT) akitoa mchango wake katika semina hiyo kuhusu mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada zinazotolewa na wataalam wa Benki Kuu ya Tanzania.
Vick Msima Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki akifuatilia mjadala katika semina hiyo.
Mwanablog kutoka Fullshangweblog Bwana John Bukuku akiwa katika semina hiyo.
Meneja Kutoka Kurugenzi ya Usimamizi wa Sekta ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania BoT akitoa mada kuhus hatua za kuimarisha usimamizi wa Taasisi za fedha.Bw. Nassor Omary.
Baadhi ya wanahabari wakijadiliana jambo katika semina hiyo.

No comments:

Post a Comment