Tuesday, December 11, 2018

WAKUU WA MIKOA WAPONGEZA UJENZI WA RELI YA KISASA (STANDARD GAUGE)

Wakuu wa mikoa nchini wameipongeza serikali  kwa ujenzi wa Reli ya kisasa  (standard Gauge) na kusema kuwa, huo ni mradi utakaoleta manufaa katika mapinduzi ya kiuchumi hasa wakati huu serikali inavyojikita katika uchumi wa viwanda.

Wakiongea na Mwandishi wa habari hizi mara baada ya kukagua Mradi huo ambapo wameanzia Morogoro hadi Dar es Salaam wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Reli Tanzania (TRC) Bwana Masanja Kadogosa.

Wamesema fursa nyingi zitapatikana mara baada ya kukamilika kwa Mradi huo mkubwa hapa Tanzania na nchi jirani.

Akizungumzia Mradi huo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa amesema kwa sasa ujenzi huo unaenda kwa kasi ambapo baadhi ya maeneo tayari wameanza kuweka miundombinu ikiwemo ya mataruma na nguzo za umeme.

Kadogosa alitoa wito kwa wananchi walio jirani na Mradi huo kutoa ushirikiano wa kutosha katika kulinda miundombinu hiyo ambayo ni chachu ya kuleta maendeleo ikiwemo upatikanaji wa ajira. 
Wakuu wa mikoa wakipata maelezo kuhusu ujenzi wa Reli ya kisasa

No comments:

Post a Comment