Sunday, December 23, 2018

MGALU ACHANGIA MIRADI YA MAENDELEO PWANI.

 Mbunge wa viti maalum mkoani Pwani, Subira Mgalu ameendelea kuchangia miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani.

Mgalu ameweza kuchangia mifuko ya saruji 40 kwaajili ya ujenzi wa Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mtongani na Mlandizi ambapo kata ya Mtongani Mifuko 20 na kata ya Mlandizi mifuko 20.

Subira alitoa mifuko hiyo ya saruji wakati alipokutana na baadhi ya viongozi wa chama ikiwa ni moja ya kazi za kichama na kusema kuwa huo ni wajibu wakena kwamba hatochoka kushiriki kusaidiana kutatua changamoto zilizopo kichama na serikali. 

Katika Ziara aliyoifanya Halmashauri ya Chalinze hapo jana, Subira mgalu alitoa Tenki la kuhifadhia maji katika zahanati ya Msata pamoja na sola itakayowasaidia pindi umeme unapokatika.

Aidha, alifika katika Zahanati ya Pongwe Kiona na kusadia mashuka 10 kwaajili ya vitanda vya wagonjwa.

Katika ziara yake kijiji cha Pongwe kiona Mbunge huyo wa Viti maalum Mkoa wa Pwani, aliweka jiwe la msingi jengo la Zahanati litakalotumika kwaajili ya kinamama kujifungulia.

Subira Mgalu ameahidi kuchangia mifuko ya Saruji katika ujenzi huo ili kuunga mkono juhudi hizo zilizoanzishwa na wananchi.


Diwani wa kata ya Mlandizi Ephrasia Kadala, alisema Hili ulilolitenda ni jambo kubwa kwa wana CCM na wananchi kijumla.

Diwani huyo aliwaomba wadau wengine kujitolea kushirikiana ili kumaliza kero zinazowakabili kichama katika kata hiyo.

Nae Katibu wa Jumuiya ya wanawake (UWT) Kibaha Vijijni Janeth Mnyaga alimshukuru mbunge huyo kuwa bega kwa bega kushiriki nao kwenye shughuli za jumuiya na chama.

Wakati huo huo Subira alitembelea kituo cha afya Mlandizi kujionea hali ya upanuzi wa majengo kwa gharama ya sh. Milioni 400 ambazo zimetolewa na serikali.

Madiwani wa kata ya Msata na Kimange Halmashauri ya Chalinze wamemtaja Subira mgalu kuwa ni mpambanaji asiyechoka na kwamba wanafarijika kuwa na muwakilishi mwenye kujali shida za wananchi katika eneo lake licha ya kuwa na jukumu la kitaifa katika wizara ya nishati.

Mganga mfawadhi wa Zahanati ya Msata Willy John amesema anamshukuru Mbunge huyo wa viti maalum mkoa wa Pwani kwa msaada wa Tenki la kuhifadhia maji na pamoja sola itakayowasaidia kwa shughuli za usiku katika Zahanati hiyo
 
 Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani, Subira Mgalu akikabidhi Tenki la kuhifadhia maji katika Zahanati ya Msata Halmashauri ya Chalinze.
 
Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Pwani, Subira Mgalu, akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa jengo la kina mama Zahanati ya Pongwe Kiona.


No comments:

Post a Comment