Sunday, December 23, 2018

ABDUL SHARIFU ATAKA WAISLAMU WASHIKAMANE

Na Omary Mngindo, Tanga

WAUMINI wa Dini ya Kiislamu hapa nchini, wametakiwa kuendeleza umoja, upendo na mshikamano, katika kuiendeleza dini hiyo ya Mwenyeezimungu.

Ushauri huo umetolewa na Alhaj Abdul Sharifu kutoka Bagamoyo Mkoa wa Pwani, akitoa mawaidha katika hafla ya Dhikri iliyofanyika kwenye Msikiti wa Masjid Az Hall uliopo Kijiji cha Kwenkwale, Halmashauri  ya Mkata, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Aidha Alhaj Sharifu amewaomba viongozi na Waumini wote wa dini hiyo, kukemea vikali matumizi mabaya ya Dufu yaliyoshamiri maeneo nbalimbali, ambapo alisema kuna baadhi yao wanayatumia kwenye ngoma aina ya Viduku.

Wakiongozwa na Mwenyeji wao Alhaj Sheikh Juma na Ma-Alhaj kutoka mikoa mbalimbali waliohudhulia Ziara hiyo, pia Sharifu amewataka waumini hao kurudisha utaratibu uliokuwa unatumiwa na Masheikh ya kutembeleana na kukumbushana mambo yanayoihusu dini hiyo kwani hayo ndio mafundisho ya Mtume Muhammadi Swalallaahu Alayhi Wasalam.

"Waislamu wenzangu kwenye miaka ya hivi karibuni dini yetu inapoteza mwelekeo, inatupasa viongozi tusimame imara katika kuhakikisha dini yetu inarejea katika mstari wake, kuna mtindo unazidi kushika kasi wa dufu kutumika kwenye ngoma ya Viduku," alisema Alhaj Sharifu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Alhaj Juma aliwashukuru Ma-Alhaj, Mashehe na waumini wote kutoka maeneo tofauti waliohudhulia, huku akisema kwamba wamekuwa katika harakati kubwa za kuiendeleza dini, huku akitoa nasaha kwa vijana kutojiingiza katika mambo ya kidunia.

"Masheikh pamoja na juhudi tunazozifanya za kuipogania dini yetu, tunapaswa kuiendeleza umoja, upendo na mshikamano, pamoja na kuhakikisha vijana wetu wanafuata misingi imara ya dini ya kiislamu," alisema Alhaj Juma.

Waumini hao kutoka mikoa mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Tanga, wameshiriki hafla ya Dhikri hiyo nwishoni kwa wiki.

Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa katika hafla hiyo iliyofanyika katika msikiti wa Az hall, uliopo Kijiji cha Kwenkwale, Halmashauri  ya Mkata, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment