Saturday, December 15, 2018

TFS YAIINGIZIA SERIKALI BILIONI 3.3 MAUZO YA MITI AINA YA MISAJI.

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) imeiingizia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zaidi ya Tshs Bilioni 3.3 kwa Mauzo ya Miti aina ya Misaji (Teak) kutoka katika Shamba la Miti Longuza yenye jumla ya Mita za ujazo 4,912.616.

TFS kwa niaba ya Serikali inasimamia Mashamba 23 ya kupandwa kati yake 13 ndiyo yamefikia viwango vya kuvunwa na mashamba mawili yanavunwa miti aina ya Misaji wakati yanayobaki huvunwa miti aina ya Misindano,mikaratusi na miti ubani (Cyprus).

Aidha, TFS husimamia pia Misitu ya Asili zaidi ya 500 huku iko hakikisha uzalishaji na usambazaji wa Mbegu bora za Miti unafanya mwa Nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Wanunuzi, Bwana Ashok Shanghavi ameuopongeza uongozi wa Shamba la Miti Longuza kwa namna wanavyosimamia Miti yao kitaalam kupelekea ubora wa Miti unaoridhisha wafanyabiashara .

Bwana Ashok ameuomba Uongozi wa TFS Makao Makuu kuhakikisha mashamba yao yote yanajifunza na kusambaza ujuzi huo ili kuwa na ubora unaofanana kwenye Mashamba yote.

No comments:

Post a Comment