Tuesday, December 4, 2018

MFUMO WA KIELECTRONIC KUITAJIRISHA CCM.

MNEC wa mkoa wa Pwani Haji Jumaa akifafanua jambo mbele ya viongozi wa chama hicho kutoka Taifa na watendaji wa Ccm Mkoa huo juu ya matumizi ya Electronic katika ukusanyaji wa mapato ya chama.
.....................................................

Na Shushu Joel, Kibaha.
KUTOKANA na mabadiliko ya mfumo wa kimawasiliano  kuwa ni makubwa nchini na duniani kumempelekea mjumbe wa halmashauri kuu ya ccm(MNEC) Haji Jumaa kuwaleta wataalam wa mfumo kutoka makao makuu ya ccm ili kuwanoa makatibu wa chama na jumuiya ili waweze kutumia fursa hiyo kwa ajili ya kuwaingiza wanachama wote wa ccm katika mfumo wa kielectronic ili kurahishia utendaji na mawasiliano baina ya wanachama na chama.

Akizungumza na watendaji wa chama hicho mara baada ya utambulisho mjumbe wa mkutano mkuu wa taifa (MNEC) Haji Jumaa  amewataka watendaji wa chama hicho kuhakikisha wanatumia nafasi hiyo ili kuwaelimisha wanachama wetu mabadiliko ya kidunia yaliyopo duniani kwa sasa.

Aliongeza kuwa mfumo huo wa ukusanyaji wa mapato ya chama utasaidia kuongezeka kwa kipato kwa cjhama hicho na kukifanya kuwa chama tajiri duniani kutokana na raslimali zake zilizopo kote nchini.

“Usajili wa wanachama ni mara moja tu kwani pale unapomaliza kujazo fomu za kitambulisho hicho taarifa zako zitakuwa ni kama zile za kitambulisho cha kitaifa”Alisema Jumaa.

Aliongeza kuwa mfumo huu utaondokana na usumbufu uliopo wa kuwa na kadi ya karatasi na nyepesi kuchanika hivyo wanachama wakipata kitambulisho hiki chenye mfano wa kadi za benki kitarahisisha vitu vingi hapa nchini.

Aidha Jumaa aliwataka watendaji wote walioajiliwa na chama kuwa wabunifu katika ukusanyaji wa mapato ili chama hicho kiweze kujiongezea mapato kwani cc mina vyanzo vingi kila maeneo katika nchi hii.

Akitoa mafunzo hayo mkuu wa idara ya uchumu kutoka ccm makao makuu Dkt Seleman Selele amempongeza mjumbe wa mkutano mkuu wa ccm kutokea mkoa wa pwani kwa juhudi zake za kuhakikisha watendaji wote wa chama katika mkoa huo wanapatiwa elimu juu ya umuhimu wa ukusanyaji na uongezaji wa mapato ya chama.

Aliongeza kuwa mfumo uliopo kwa sasa katika ukusanyaji wa mapato ya chama ni wa kisasa na wenye tija kubwa katika ufanikishaji wa maendeleo ya chama.

Aidha Dkt Selele aliwataka watendaji wote wa chama kuendana na mabiliko yaliyopo ndani ya chama kwani lengo la chama hicho ni zuri na lenye maana kubwa kwa wanachama wake.

Mmmoja wa makatibu walioudhuria kikao hicho kutokea katika wilaya ya kibaha vijijini Janeth Mnyaga ameupongeza uongozi wa chama hicho katika ngazi ya mkoa kwa kuona umuhimu wa kuwaleta viongozi wa kitaifa walio bobea katika masuala ya uchumi ili kuwaelekeza jinsi ya kukiongezea chama hicho mapato.

Hivyo amewataka viongozi wenzake kuwa wawazi katika zoezi linaloendelea nchini katika kuorodhesha mali za chama na jinsi zilivyopangishwa .
Wajumbe wa mkutano huo wakisikiliza elimu inayotolewa na wataalam kutoka makao makuu ya ccm juu ya umuhimu wa kutumia mfumo wa electronic katika ukusanyaji wa mapato ya chama hicho.

No comments:

Post a Comment