Saturday, December 8, 2018

TAKUKURU LINDI YAWAONYA WANAOKWEPA USHAHIDI.

Na hadija Hassan Lindi.

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Lindi, imetoa onyo kwa wananchi,na watumishi wa mkoa huo walio na tabia ya kupeleka Malalamiko Ofisini kwao kisha kukataa kutoa ushahidi wa kumtetea Mhalifu.

Onyo hilo limetolewa na kamanda wa Takukuru mkoani hapa Steveni Chami Jana alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari  Ofisini kwake.

Chami ametoa onyo hilo ,kufuatia watumishi watatu wa Idara ya Afya Katika kituo cha Afya cha Manispaa ya Lindi ,kufika Ofisi ya Taasisi hiyo kulalamikia aliyewahi kuwa Kaimu Mganga Mkuu  wa Manispaa hiyo,Abirahi Rashid Mbingu,kudaiwa kudhurumu fedha za malipo kwa Manesi waliokuwa wamefanya kazi ya ziada.

Alisema kufuatia taarifa hiyo,waliifanyia kazi ikiwemo kukusanya nyaraka zilizotumika kufanyia malipo,kuwaita wale watumishi waliodaiwa kulipwa fedha hizo,ili kutambua iwapo sahihi zilizokuwa zimeonekana ni za kwao na kuzikataa kwamba sio zao na hawajawahi kulipwa.

Chami alisema baada ya taratibu zote za ki-Ofisi kukamilika,mtuhumiwa Mbingu Juni 15/2017,alifikishwa Mahakama ya Wilaya ya Lindi kwa kesi Namba 57/2017,kujibu Shitaka linalomkabiri, lakini ilipofika zamu ya watumishi hao kutoa ushahidi wao,waligeuka na kumtetea mshitakiwa.

“Hawa watumishi ambao hapo awali waliiambia Takukuru hawakuwa wamelipwa fedha za On-Call allowance zilizoonyesha katika orodha ya walipwaji sio zao,lakini walipofika Mahakamani waligeuka na kudai sahihi sio zao fedha wamepata”Alisema Chami.

Aidha kamanda  chami amewataja watumishi  hao ambao wote amedai ni manesi wa Kituo cha Afya cha Manispaa hiyo kuwa ni,Stephen Haji,Mwanahawa Swalehe na Mayila Chikamtenda.

“Ugeugeu uliofanywa na watumishi hawa,kwa makusudi wameamua kumsaidia mtuhumiwa kwa kusema uongo Mahakamani,kitendo ambacho ni kosa la jinai na kinyume na Kifungu cha 102 cha Sheria ya kanuni ya adhabu,Sura ya 16/2002”Alisema Chami.

Alisema kutokana na ugeugeu ulionyeshwa na watumishi hao,Hakimu wa Mahakama ya Mkoa wa Lindi,Liliani Lugalabamo alilazimika kumuachia huru mshitakiwa Abirahi Rashidi Mbingu,baada ya kukosekana kwa ushahidi wa kumtia hatiani.

Hata hivyo,Chami alisema kutokana na kitendo hicho Ofisi ya Takukuru Mkoani Lindi,imewafungulia kesi ya jinai namba 122/2018,watumishi hao watatu kwa kosa la kusema uongo na kukataa kueleza ukweli Mahakamani.

No comments:

Post a Comment