Wednesday, December 5, 2018

RIDHIWANI AWALAZA WABUNGE WA UGANDA NA VIATU.

Na Shushu Joel,
MBUNGE wa Tanzania  anayetokea  jimbo la Chalinze mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete amewalaza wabunge wa uganda na viatu mara baada ya kuwachachafya mabeki wa timu hiyo katika mchezo wao wa kwanza katika mashindano ya wabunge yanayoendelea huko nchini Burundi.

Katika mechi hiyo ilichezwa juzi katika uwanja wa amavumbi nchini humo timu ya Bunge la Tanzania ilipoteza mchezo huo kwa kufungwa goli 2 kwa 1.

Akizungumza kwa njia ya simu kutokea nchini Burundi Ridhiwani Kikwete alisema kuwa mchezo huo ulikuwa mziri na wa kuvutia ingawa walipoteza mechi hiyo kwa wabunge walio wengi hawana mazoezi ya kutosha hivyo pumzi uwaishia na kupelekea kuwapatia nafasi wenzetu ambao wanaonekana kuwa na mazoezi ya muda mrefu katika kujiandaa na michezo mbalimbali.

“Tumefungwa na wenzetu wa Uganda lakini kazi wameiona kwani tulifanikiwa kuwashambulia mara kwa mara ingawa bahati haikuwa ya kwetu ila mabeki wamelazwa na viatu kutokana na jinsi walivyochoka kwa mashambulizi ya Bunge la Tanzania”Alisema Kikwete.

Kwa upande wake mbunge wa Sengerema Ezekiel Ngereja alisema kuwa kilichowafungisha ni kutokuwa na mazoezi ya muda mrefu ila kama tungekuwa na pumzi kama alizozionyesha mbunghe mwenzetu wa jimbo la chalinze amabye muda mwingi alionekamna kuwa ni mwiba katika lango la wapinzani wetu.

Aliongeza kuwa kupoteza mechi moja si hoja bali meci zijazo lazima tutashinda kutokana na hali yaliyonayo kambi wabunge wa Tanzania.

“Tunawaomba watanzania wote huko nyumbani waendelee kutuombea ili mechi zijazo tuweze kushinda na kuchukua kombe na kurudi na heshima nyumbani ili wachezaji wetu waweze kujifunza katika mechi zao”Alisema Ngereja.

Akizungumza kwa njia ya simu kaptain wa timu ya bunge la Uganda aliyejitambulisha kwa jina moja la Pentagoni ambaye anacheza nafasi ya kiunga mshambuliaji alisema kuwa ingawa wameshinda kwa gori 2 kwa 1 dhidi ya wapinzao wao wa Bunge la Tanzania ila kazi pevu wameiona kutoka kwa mbunge wa chalinze ambaye alikuwa anawapa shida kubwa kwa jinsi alivyokuwa akicheza katika mechi hiyo.

Aliongeza kuwa timu ya Bunge ya Tanzania iko vizuri sema tu wabunge walio wengi hawafanyi mazoezi hivyo wanakosa pumzi na kupelekea kufungwa lakini mbunge Ridhiwani Kikwete anaonekana anafanya mazoezi sana ndio maana anaonekana kuwa ni msumbufu sana katika kumkaba na kumpora mpira pindi anapokuwa nao.

No comments:

Post a Comment