Tuesday, December 11, 2018

RUVU DARAJANI WALILIA MAZAO YAO

Baadhi ya wakulima katika bonde la Ruvu, kijiji cha Ruvu Darajani kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wakionesha miche ya mipapai iliyokatwa katwa katika mashamba yao, PICHA NA OMARY MNGINDO.
...........................................................


Na Omary Mngindo, Ruvu

WAKULIMA katika Kijiji cha Ruvu Darajani, Kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wameiomba Serikali kuingilia kati vitendo vinavyofanywa na watu wanaojiita wanatoka ofisi inayosimamia bonde la Ruvu wilayani humo, kwa kufyeka mazao waliyoyapanda. 

Wakizungumza na waandishi wa habari katika mashamba yao, wakazi wakijitambilisha kwa majina ya Ally Jeki,  Zaynabu Kikande  Shayo, Ally Jeki na Said Swaiba, walisema kuwa mwishoni mwa wiki wamevamiwa na watu hao waliokatakata mazao kwenye mashamba yao. 

Swaiba alisema kuwa siku ya tukio watu hao walipofika waliwachuku vijana wakaelekea nao kwenye mashamba hayo, kisha kuanza zoezi la kukata mazao pasipokushirikisha viongozi wa Kijiji, kitendo walichokieleza ni cha uonevu, huku wakiomba serikali ikemee jambo hilo. 

"Tunalima bustani nje ya mita 60 wanaodai ni mali yao, lakini cha kusikitisha hivi karibuni wamekuja kuivamia, wamekata mazao yetu ambayo wengi wetu tunayategemea kuendesha familia zetu, wengine tunasomesha kupitia kilimo hiki," alisema Swaiba.

Nae Samir Shayo alilalamika mipapainyake kukatwa baa watu hao ambao walipofika waliambatana na askari waliokuwa na silaha za moto,  kitendo kilichowaogopesha wananchi hao. 

"Kama mnavyoona, shamba langu lipo mbali na mita za 60 lakini hata kama wamechukua mita 100 bado wsingefika hapa, lakini wameamua kutufanya kitendo kibayabsana,  tunaomba serikali ikemee vitendo hivi vya kibabe," alisema Samir. 

Kwa upande wake Mjumbe wa serikali ya Kijiji cha Ruvu Ramadhani Natamani alisema kwamba mwezi wa nne mwaka huu walifika ofisini kwao wakawaeleza wanataka kuweka mipaka ya kuonesha mwisho wa kulimwa, lakini hawakuonekana tena 

"Cha kusikitisha Mtendaji wa Kijiji alipotaka kuwasogelea wajue kinachoendelea, aliambiwa asiwasogelee eneo walilokuwa wanakata mazao ya wakulima,  tunaomba uongozi wa Mkoa uingiliekati suala hili, " alisema Mnyamani.
 
Sehemu ya miche ya mipapai iliyokatwa katwa katika mashamba ya wakulima wa bonde la Ruvu kijiji cha Ruvu Darajani kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani, PICHA NA OMARY MNGINDO.

No comments:

Post a Comment