Saturday, December 8, 2018

NYUMBA 38 ZAEZULIWA MAPAA KWA UPEPO LINDI.

Na Hadija Hassan, Lindi.

Nyumba {38} yakiwemo majengo yanayomilikiwa na Serikali yamebomolewa na kuezuliwa  mapaa, kutokana na upepo mkali (Kimbunga) uliojitokeza mwanzoni mwa wiki hii, Wilaya ya Liwale, Mkoani Lindi,


na kusababisha hasara ambayo bado haijaweza kufaha mika mara moja.


Habari ambazo zimethibitishwa na Serikali ya Wilaya hiyo,inaeleza tukio hilo limetokea mchana wa Disemba 03 mwaka huu,Kata za Nangano na Ngunja.


Wakizungumza na BAGAMOYO KWANZA BLOG ,baadhi ya wananchi akiwemo   Ashura Juma,Rehema Yusufu, Hemedi Ally Kindamba na Mohamedi Omari walisema upepo mkali wa Kimbunga uliovuma siku hiyo,umebomoa baadhi ya majumba pamoja na taasisi za serikali ikiwemo majengo ya shule na hata ghala la kuhifadhia mazao



Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Liwale,Sarah Chiwamba amekiri upepo wa Kimbunga hicho kuharibu Majengo ya Serikali, nyumba za wananchi, nyumba za watumishi pamoja na vyumba vya madarasa na Maabara.

Chiwamba amefafanua kwa kueleza kwamba kati ya Nyumba (38) zilizobomolewa (20) zipo kwenye ubora,zilizojengwa kwa matofari na kuezekwa kwa Bati,wakati (18) zilizosalia zimeizuliwa mapaa,kufuatia wananchi kujiwekea utamaduni wa kuezeka kwa Bati bila ya kupigilia Misumali.


‘’Hizi {18} zimejengwa kwa kutumia tope na Bati zilizoezekwa hazikupigiliwa Misumali,badala yake uziweka tu na kukandamizia vipande vya Miti’’Alisema Chiwamba.


Aidha,ameeleza Kimbunga hicho pia kimeezua paa za vyumba viwili vya Maabara Shule za Sekondari za Nangano na Ngunja, Nyumba mbili zinazotumika kuishi watumishi,Chumba cha Darasa na Choo kwa Shule ya msingi Nangano,pamoja na Ghala la kuhifadhia Mazao la Kata ya Nangano.


Aidha Chiwamba alieleza kuwa kufuatia tukio hilo,zile kaya zilizokumbwa na maafa hayo na kubainika ipo katika hali isiyo mzuri wamesaidiwa Debe moja la Mahindi kila moja na fedha kiasi cha Tsh,5,000/-.


Na kuongeza  kuwa kwa waliathirika zaidi wamepatiwa msaada wa kupatiwa Debe moja-moja la Mahindi na hela kiasi cha Tsh,5,000/-wakati uongozi wa wilaya ukiendelea na taratibu zingine za kuwasaidia wananchi hao.


Hata hivyo Chiwamba Alisema kuwa thamani ya nyumba hizo hazijafahamika. 


‘’Kuhusu kiwango cha hasara kilichopatikana naomba tuwasiliane baada ya siku mbili kupita,kwani wataalamu kwa sasa wapo huko wakitathimini kwanza’’Alisema Chiwamba.

No comments:

Post a Comment