Saturday, December 8, 2018

RADI YAUA MTU MMOJA LINDI

Na Hadija Hassan, Lindi

Radi iliyoambatana na kiasi kichache cha Mvua iliyonyesha mwanzoni mwa wiki hii, Wilaya ya Liwale, Mkoani Lindi, imemuuwa mkazi mmoja wa Kijiji cha Mbuli, Kata ya Kichonda, Salima Kakole {42}.

Habari za uhakika kutoka Kijijini huko na kuthibitishwa na uongozi wa Serikali ya wilaya hiyo,imeeleza kwamba Kalole ameuwawa na Radi hiyo,Disemba 03 mwaka huu, majira ya saa 7-8 mchana.

Baadhi ya mashahidi wa tukio hilo akiwemo  Juma Selema, Kindamba Hemedi na Mwajuma Issaya,walisema kuwa siku ya tukio hill Mvua ndogondogo iliyonyesha ndipo Radi kali iliweza kujitokeza na kumfika Salima Kalole.

Walieleza kwamba wakati Mvua hiyo ikinyesha, Salima Kalole alikuwa amesimama nje ya Nyumba yake huko mashambani, akiendelea kutekeleza majukumu ya kazi zake ndogondogo.

“Mama huyu alikuwa akizifanya kazi zake ndogondogo nje ya Nyumba yake (uwanjani), hivyo Radi ilipopiga ilimfika yeye kisha kumuunguza Hali iliyopelekea   kupoteza Uhai wake Papo happy ”Walieleza Mashuhuda hao.

Mashuhuda hao alieleza  kwamba mwanamke huyo ameacha watoto watatu,wakiwemo wanawake wawili na mwanaume mmoja,mwili wake umezikwa juzi,Disemba 04 mwaka huu,saa 4:0 asubuhi.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo ya Liwale,Sarah Chiwamba,amekili kuuwawa mwanamke huyo kwa Radi iliyokuwa imeambatana na kiasi kidogo cha Mvua iliyokuwa inanyesha kwa siku hiyo.



Chiwamba pia amewaomba wananchi kujiepusha na utamaduni wa kukaa nje,ikiwemo karibu na Miti au uwanjani pale Mvua zinapoendelea kunyesha na badala yake,wawe wanajihifadhi kwenye Nyuumba zao.

No comments:

Post a Comment